Ushauri wa Zitto kwa vyama makini vya ushindani

mcubic

JF-Expert Member
Mar 3, 2011
10,306
6,514
Unashangaa ya Mrema ( TLP ) na Cheyo ( UDP )? Kama ni msomaji wa Siasa za Dunia wala hutasumbuka maana NI mambo yamefanyika sana. Hao ndio systemic opposition.
Jambo la muhimu ni kujua kuwa Rais wa sasa sio yule aliyemtangulia na hivyo CCM ya kuanzia Leo haitakuwa CCM iliyoishia Jana. Rais anayeweza kutamka hadharani kuwa ' angewapoteza' watu, tena wanachama wa Chama chake, kwa kuonyesha kutokukubaliana na Maamuzi ya chama ndani ya vikao vya Chama, ni mtu hatari na hivyo mbinu za kushindana naye lazima ziwe tofauti.
Huu ndio wakati wa kujenga Mfumo madhubuti wa Vyama vingi kuliko wakati mwengine wowote katika historia ya Nchi yetu. Nasaha zangu kwa Viongozi wote wa upinzani ni ' tujisomee kwanza '! Tujue mbinu na medani. Pia Sisi tuwe ' more democratic ' kuliko CCM kwa kuruhusu maoni tofauti kwenye Vyama vyetu badala ya kuwa na tabia zile zile za CCM.
Mrema na Cheyo wamekuwa wenyeviti wa Vyama vyao tangu Mwinyi ni Mwenyekiti wa CCM na bado hawaoni haya wala soni kusifia CCM na mfumo wao wa kubadilishana Uongozi. Cheyo alikuwapo Mwinyi alipomkabidhi Mkapa, Mkapa alipomkabidhi Kikwete na Kikwete alipomkabidhi Magufuli! Kote huko alitoa hotuba. Wachambuzi wa Siasa wangechambua hotuba za Cheyo miaka yote hiyo na kumwuliza anajisikiaje!
Uenyekiti wa Magufuli CCM ni faida kwa mfumo wa Vyama vingi kwani Upinzani wa kweli utaimarika. Upinzani wa Hoja na Masuala utaimarika zaidi kuliko wakati mwengine wowote.

Huu ndio wakati wa kusambaza Azimio la Tabora linalohuisha Azimio la Arusha.
 
Unashangaa ya Mrema ( TLP ) na Cheyo ( UDP )? Kama ni msomaji wa Siasa za Dunia wala hutasumbuka maana NI mambo yamefanyika sana. Hao ndio systemic opposition.
Jambo la muhimu ni kujua kuwa Rais wa sasa sio yule aliyemtangulia na hivyo CCM ya kuanzia Leo haitakuwa CCM iliyoishia Jana. Rais anayeweza kutamka hadharani kuwa ' angewapoteza' watu, tena wanachama wa Chama chake, kwa kuonyesha kutokukubaliana na Maamuzi ya chama ndani ya vikao vya Chama, ni mtu hatari na hivyo mbinu za kushindana naye lazima ziwe tofauti.
Huu ndio wakati wa kujenga Mfumo madhubuti wa Vyama vingi kuliko wakati mwengine wowote katika historia ya Nchi yetu. Nasaha zangu kwa Viongozi wote wa upinzani ni ' tujisomee kwanza '! Tujue mbinu na medani. Pia Sisi tuwe ' more democratic ' kuliko CCM kwa kuruhusu maoni tofauti kwenye Vyama vyetu badala ya kuwa na tabia zile zile za CCM.
Mrema na Cheyo wamekuwa wenyeviti wa Vyama vyao tangu Mwinyi ni Mwenyekiti wa CCM na bado hawaoni haya wala soni kusifia CCM na mfumo wao wa kubadilishana Uongozi. Cheyo alikuwapo Mwinyi alipomkabidhi Mkapa, Mkapa alipomkabidhi Kikwete na Kikwete alipomkabidhi Magufuli! Kote huko alitoa hotuba. Wachambuzi wa Siasa wangechambua hotuba za Cheyo miaka yote hiyo na kumwuliza anajisikiaje!
Uenyekiti wa Magufuli CCM ni faida kwa mfumo wa Vyama vingi kwani Upinzani wa kweli utaimarika. Upinzani wa Hoja na Masuala utaimarika zaidi kuliko wakati mwengine wowote.

Huu ndio wakati wa kusambaza Azimio la Tabora linalohuisha Azimio la Arusha.

Sijasahau kwamba siyo muda mrefu sana uliopita, Zitto alikuwa na "project" ya "kuiangamiza" CHADEMA. kwamba kwa kuondoka kwake, CHADEMA ingekufa, maana angeondoka na wengi. pia nakumbuka wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2015, chama cha ACT kilishambulia sana UKAWA. leo anaongelea kujipanga upya kwa upinzani. sina tatizo na kuimarisha demokrasia ndani ya vyama. tatizo langu ni kwamba hizi kelele za demokrasia ndani ya vyama zimeshika kasi baada ya mbinu za Zitto kutekeleza tamaa yake ya madaraka kukwama. na kwa kweli Zitto kwa umri wake na kukosa uzoefu kwake, alipaa kwa kasi sana ndani ya CHADEMA mpaka kufikia cheo alichokuwa nacho. kwa chama kinachotuhumiwa kwa "Ukristo" na "Ukanda", kupanda kwa Zitto ungesema ni muujiza wa karne.

Kwa hiyo, sishangai kwamba UKAWA wanamwangalia Zitto kwa jicho kali. huyo hana tofauti na akina Mrema na Cheyo, ila tu anatumia akili zaidi kufanikisha uroho wake.
 
Sijasahau kwamba siyo muda mrefu sana uliopita, Zitto alikuwa na "project" ya "kuiangamiza" CHADEMA. kwamba kwa kuondoka kwake, CHADEMA ingekufa, maana angeondoka na wengi. pia nakumbuka wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2015, chama cha ACT kilishambulia sana UKAWA. leo anaongelea kujipanga upya kwa upinzani. sina tatizo na kuimarisha demokrasia ndani ya vyama. tatizo langu ni kwamba hizi kelele za demokrasia ndani ya vyama zimeshika kasi baada ya mbinu za Zitto kutekeleza tamaa yake ya madaraka kukwama. na kwa kweli Zitto kwa umri wake na kukosa uzoefu kwake, alipaa kwa kasi sana ndani ya CHADEMA mpaka kufikia cheo alichokuwa nacho. kwa chama kinachotuhumiwa kwa "Ukristo" na "Ukanda", kupanda kwa Zitto ungesema ni muujiza wa karne.

Kwa hiyo, sishangai kwamba UKAWA wanamwangalia Zitto kwa jicho kali. huyo hana tofauti na akina Mrema na Cheyo, ila tu anatumia akili zaidi kufanikisha uroho wake.
Soma mada uielewe.....
 
Sijasahau kwamba siyo muda mrefu sana uliopita, Zitto alikuwa na "project" ya "kuiangamiza" CHADEMA. kwamba kwa kuondoka kwake, CHADEMA ingekufa, maana angeondoka na wengi. pia nakumbuka wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2015, chama cha ACT kilishambulia sana UKAWA. leo anaongelea kujipanga upya kwa upinzani. sina tatizo na kuimarisha demokrasia ndani ya vyama. tatizo langu ni kwamba hizi kelele za demokrasia ndani ya vyama zimeshika kasi baada ya mbinu za Zitto kutekeleza tamaa yake ya madaraka kukwama. na kwa kweli Zitto kwa umri wake na kukosa uzoefu kwake, alipaa kwa kasi sana ndani ya CHADEMA mpaka kufikia cheo alichokuwa nacho. kwa chama kinachotuhumiwa kwa "Ukristo" na "Ukanda", kupanda kwa Zitto ungesema ni muujiza wa karne.

Kwa hiyo, sishangai kwamba UKAWA wanamwangalia Zitto kwa jicho kali. huyo hana tofauti na akina Mrema na Cheyo, ila tu anatumia akili zaidi kufanikisha uroho wake.
Zito wakati wa JK alitulia, mbona sasa Ana maneno mengi. Zito ni mdini
 
Unashangaa ya Mrema ( TLP ) na Cheyo ( UDP )? Kama ni msomaji wa Siasa za Dunia wala hutasumbuka maana NI mambo yamefanyika sana. Hao ndio systemic opposition.
Jambo la muhimu ni kujua kuwa Rais wa sasa sio yule aliyemtangulia na hivyo CCM ya kuanzia Leo haitakuwa CCM iliyoishia Jana. Rais anayeweza kutamka hadharani kuwa ' angewapoteza' watu, tena wanachama wa Chama chake, kwa kuonyesha kutokukubaliana na Maamuzi ya chama ndani ya vikao vya Chama, ni mtu hatari na hivyo mbinu za kushindana naye lazima ziwe tofauti.
Huu ndio wakati wa kujenga Mfumo madhubuti wa Vyama vingi kuliko wakati mwengine wowote katika historia ya Nchi yetu. Nasaha zangu kwa Viongozi wote wa upinzani ni ' tujisomee kwanza '! Tujue mbinu na medani. Pia Sisi tuwe ' more democratic ' kuliko CCM kwa kuruhusu maoni tofauti kwenye Vyama vyetu badala ya kuwa na tabia zile zile za CCM.
Mrema na Cheyo wamekuwa wenyeviti wa Vyama vyao tangu Mwinyi ni Mwenyekiti wa CCM na bado hawaoni haya wala soni kusifia CCM na mfumo wao wa kubadilishana Uongozi. Cheyo alikuwapo Mwinyi alipomkabidhi Mkapa, Mkapa alipomkabidhi Kikwete na Kikwete alipomkabidhi Magufuli! Kote huko alitoa hotuba. Wachambuzi wa Siasa wangechambua hotuba za Cheyo miaka yote hiyo na kumwuliza anajisikiaje!
Uenyekiti wa Magufuli CCM ni faida kwa mfumo wa Vyama vingi kwani Upinzani wa kweli utaimarika. Upinzani wa Hoja na Masuala utaimarika zaidi kuliko wakati mwengine wowote.

Huu ndio wakati wa kusambaza Azimio la Tabora linalohuisha Azimio la Arusha.
Shikamoo Zitto, (Am a lil, older than your butt though brother, sio shikamoo ya kivile o_O)
 
Tunaweza kabisa kumpuuza anayesema ukweli lakini tukakubali ukweli anaosema, hata kama yeye mwenyewe hautendei haki huo ukweli.

Shetani ni baba wa uongo, lakini kama utatokea muujiza ukibahatika kukutana naye na akakuambia uongo ni mbaya utakupeleka jehanamu, msikilize na ukubali lakini usimfuate, kwa sababu anachosema hakitendi...!!!
 
Sijasahau kwamba siyo muda mrefu sana uliopita, Zitto alikuwa na "project" ya "kuiangamiza" CHADEMA. kwamba kwa kuondoka kwake, CHADEMA ingekufa, maana angeondoka na wengi. pia nakumbuka wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2015, chama cha ACT kilishambulia sana UKAWA. leo anaongelea kujipanga upya kwa upinzani. sina tatizo na kuimarisha demokrasia ndani ya vyama. tatizo langu ni kwamba hizi kelele za demokrasia ndani ya vyama zimeshika kasi baada ya mbinu za Zitto kutekeleza tamaa yake ya madaraka kukwama. na kwa kweli Zitto kwa umri wake na kukosa uzoefu kwake, alipaa kwa kasi sana ndani ya CHADEMA mpaka kufikia cheo alichokuwa nacho. kwa chama kinachotuhumiwa kwa "Ukristo" na "Ukanda", kupanda kwa Zitto ungesema ni muujiza wa karne.

Kwa hiyo, sishangai kwamba UKAWA wanamwangalia Zitto kwa jicho kali. huyo hana tofauti na akina Mrema na Cheyo, ila tu anatumia akili zaidi kufanikisha uroho wake.
Huyu ni mtu mnafiki balaa
 
Siasa za Tanzania ni unafiki mtupu ndio umetamalaki si kwa ccm pekee hata vyama vya upinzani.....
............................................................................. . ......

Cheki hii kabla ya lowasa hajaenda chadema CCM walikuwa wakimtetea kuwa si fisadi wakati huo huo chama kikui cha upinzani Tanzania (Chadema) chini ya wilbroad Slaa kwa miaka kadhaa walikuwa wakituhubiria kuwa Lowasa ni fisadi la mafisadi... Wote hatujaisahau ile "LIST OF SHAME"

Unafiki umekuja kujidhihirisha baada ya Lowasa kuhamia chadema kwani wale waliokuwa wakimuita ni mwizi na fisadi Leo wanatuaminisha kuwa ulikuwa ni mfumo na sio yeye !!!!!!!!..... Wale waliokuwa wakimtetea kuwa kuwa sio fisadi (CCM) wanatupasua ngoma za masikio na kutuambia kuwa jamaa huyu alikuwa ni fisadi Wa kutupa... Siamini siasa za Tanzania .
Sijaona siasa za Tanzania zilizo safi kwa maendeleo ya mtanzania zaidi ya kushuhudia siasa uchwara za kutafuta mlo na kutunafikia watanzania.....
Wanasiasa wanafiki wasiokuwa na misimamo na wazandiki ni hatari zaidi ya Bomu la nyuklia.. Kwa sasa tupo katika kipindi cha kushuhudia wanasiasa Wa dizaini hiyo....
 
Unashangaa ya Mrema ( TLP ) na Cheyo ( UDP )? Kama ni msomaji wa Siasa za Dunia wala hutasumbuka maana NI mambo yamefanyika sana. Hao ndio systemic opposition.
Jambo la muhimu ni kujua kuwa Rais wa sasa sio yule aliyemtangulia na hivyo CCM ya kuanzia Leo haitakuwa CCM iliyoishia Jana. Rais anayeweza kutamka hadharani kuwa ' angewapoteza' watu, tena wanachama wa Chama chake, kwa kuonyesha kutokukubaliana na Maamuzi ya chama ndani ya vikao vya Chama, ni mtu hatari na hivyo mbinu za kushindana naye lazima ziwe tofauti.
Huu ndio wakati wa kujenga Mfumo madhubuti wa Vyama vingi kuliko wakati mwengine wowote katika historia ya Nchi yetu. Nasaha zangu kwa Viongozi wote wa upinzani ni ' tujisomee kwanza '! Tujue mbinu na medani. Pia Sisi tuwe ' more democratic ' kuliko CCM kwa kuruhusu maoni tofauti kwenye Vyama vyetu badala ya kuwa na tabia zile zile za CCM.
Mrema na Cheyo wamekuwa wenyeviti wa Vyama vyao tangu Mwinyi ni Mwenyekiti wa CCM na bado hawaoni haya wala soni kusifia CCM na mfumo wao wa kubadilishana Uongozi. Cheyo alikuwapo Mwinyi alipomkabidhi Mkapa, Mkapa alipomkabidhi Kikwete na Kikwete alipomkabidhi Magufuli! Kote huko alitoa hotuba. Wachambuzi wa Siasa wangechambua hotuba za Cheyo miaka yote hiyo na kumwuliza anajisikiaje!
Uenyekiti wa Magufuli CCM ni faida kwa mfumo wa Vyama vingi kwani Upinzani wa kweli utaimarika. Upinzani wa Hoja na Masuala utaimarika zaidi kuliko wakati mwengine wowote.

Huu ndio wakati wa kusambaza Azimio la Tabora linalohuisha Azimio la Arusha.
Siyo Azimio la Tabora sema ni Zimio la Mwandiga
 
Sijasahau kwamba siyo muda mrefu sana uliopita, Zitto alikuwa na "project" ya "kuiangamiza" CHADEMA. kwamba kwa kuondoka kwake, CHADEMA ingekufa, maana angeondoka na wengi. pia nakumbuka wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2015, chama cha ACT kilishambulia sana UKAWA. leo anaongelea kujipanga upya kwa upinzani. sina tatizo na kuimarisha demokrasia ndani ya vyama. tatizo langu ni kwamba hizi kelele za demokrasia ndani ya vyama zimeshika kasi baada ya mbinu za Zitto kutekeleza tamaa yake ya madaraka kukwama. na kwa kweli Zitto kwa umri wake na kukosa uzoefu kwake, alipaa kwa kasi sana ndani ya CHADEMA mpaka kufikia cheo alichokuwa nacho. kwa chama kinachotuhumiwa kwa "Ukristo" na "Ukanda", kupanda kwa Zitto ungesema ni muujiza wa karne.

Kwa hiyo, sishangai kwamba UKAWA wanamwangalia Zitto kwa jicho kali. huyo hana tofauti na akina Mrema na Cheyo, ila tu anatumia akili zaidi kufanikisha uroho wake.
Mkuu pokea shukrani nyingi sana kutoka kwangu binafsi na wale wasiyo na uwezo wa kukupa hizo pongezi huo ndio ukweli kuwa zitto ni mtu wa kuogopwa kama mrema na cheyo hawana tofauti kwenye nafsi zao, tofauti ni elimu tu
 
Back
Top Bottom