Ushauri wa kitaalamu: Misumari ya Bati

linkedIn

Senior Member
Dec 20, 2014
151
55
Habari za asubuhi wanajamvi!
Samahani naomba Kuuliza kwa anayefahamu,

Hivi kuna tatizo gani linaweza kutokea endapo utatumia misumari ya bati za kawaida yaani migongo midogo kuezekea bati za migongo mipana!

Naomba kufahamu hilo!
Nawasilisha!
 
Habari za asubuhi wanajamvi!
Samahani naomba Kuuliza kwa anayefahamu,

Hivi kuna tatizo gani linaweza kutokea endapo utatumia misumari ya bati za kawaida yaani migongo midogo kuezekea bati za migongo mipana!

Naomba kufahamu hilo!
Nawasilisha!
Itategemea na ukubwa wa hiyo migongo pamoja na hali ya hewa ya eneo lilipo jengo lako(mfano kama eneo lina kawaida ya upepo mkali).Kingine ,tunatumia misumari maalumu kwa ajili ya kunakshi paa.likezekwa kwa misumari yenye rangi yake paa huonekana vizuri.Ni vizuri ukawasiliana na fundi wako ili aone kipi kitafaa zaidi kadiri ya mazingira yalivyo
 
Itategemea na ukubwa wa hiyo migongo pamoja na hali ya hewa ya eneo lilipo jengo lako(mfano kama eneo lina kawaida ya upepo mkali).Kingine ,tunatumia misumari maalumu kwa ajili ya kunakshi paa.likezekwa kwa misumari yenye rangi yake paa huonekana vizuri.Ni vizuri ukawasiliana na fundi wako ili aone kipi kitafaa zaidi kadiri ya mazingira yalivyo
Nashukuru sana jakadio kwa ushauri wako!
 
Jakadio
Tunatumia misumari kulingana na kina cha migongo nikimaanisha misumari ya kawaida ina urefu wa mm 75 lakini misumari ya mabati migongo mipana lazima utumie misumari yenye urefu mm 100
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom