Ushauri wa kitaalamu kwa wanaohitaji kulima kibiashara

JBAM

Member
Feb 16, 2012
22
13
Heshima kwenu wanajamvi

Tanzania tumekuwa na sera nyingi za kuendeleza kilimo cha mtanzania (mkulima mdogo mdogo) kwa miaka hamsini sasa. Lakini pamoja na sera nyingi na zenye mvuto masikioni tumeshindwa kufikia lengo kama nchi. Moja ya changamoto kubwa ambayo imekuwa ikisahaulika ni wataalamu wenye uwezo wa kumshauri mkulima kwa wakati sahihi juu ya zao gani aoteshe wapi, aoteshe vipi, lini, udhibiti wa magonjwa na wadudu waharibifu, uhifadhi wa udongo kwa kilimo endelevu na matumizi sahihi ya mbolea. hii imekuwa ni changamoto kwa muda mrefu sasa kwa wakulima wa Tanzania ukilinganisha na baadhi nchi za jirani zilizofanikiwa kuboresha kilimo.

Kwa kutambua changa moto hii tumeanzisha consulting firm ambayo kwa sasa ina ofisi zake mjini Morogoro na Moshi ambapo unaweza kupata ushauri sahihi wa kitaalam kuhusiana na kilimo cha mazao yote yanayostawi katika ukanda wa kitropiki (tropical crops) popote ulipo katika Tanzania. Pia tunatoa huduma ya upimaji udogo ili kutambua mahitaji ya rutuba katika udongo, tunauza mbegu mbali mbali zenye ubora na madawa ya kudhibiti wadudu na magonjwa.

kwa wale wafanyabiashara na wafanyakazi wa sekta nyinginezo (zisizo za kilimo) ambao wangependa kulima kibiashara nafasi ndio hii.

Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuni PM au kutumia simu namba 0653649152.
 
Asante kwa taarifa mkuu. Labda hii inaweza kuwa njia nyingine ya kumkomboa mtanzania anaelima.
Nafikiri ni vema ukaweka na bei zenu yaani consultancy fee itakua njema zaidi

Thanks
 
Asante kwa taarifa mkuu. Labda hii inaweza kuwa njia nyingine ya kumkomboa mtanzania anaelima.
Nafikiri ni vema ukaweka na bei zenu yaani consultancy fee itakua njema zaidi

Thanks

nashukuru mkuu kwa mchango wako. napenda kukuhakikishia kuwa bei zetu ni za kizalendo kabisa kwa ajili ya wakulima wadogo na wajasiriamali wa sekta ya kilimo. gharama hutofautiana kutegemeana na shamba lilipo (mkoa ulipo). tafadhali usisite kuwasiliana nasi kupitia namba hiyo. huduma zetu ni za haraka hakuna ucheleweshaji
 
Kama mmejipanga vizuri na mmeangalia wapi tulipokosea ktkt hiyo miaka 50 ya uhuru basi tunawatakia kila la kheri...

Hofu yangu ni kuwa kwa sera hizi mbovu za kilimo tulizonazo sijui kama malengo yenu yatatimia. Mkulima mdogo ana matatizo mengi sana ambayo utatuzi wake ni wa kisera. Hata mkiniuzia mbegu leo, nitaendaje kulima kwenye shamba langu lile lile ambalo halipapimwa na siwezi kulitumia kama dhamana ili nipate mkopo wa kuliendeshea? Je mvua ikikatiba baada ya mwezi mmoja kuna insurance yoyote ya kumlipa huyu mkulima kwa nguvu na gharama alizotumia? Anyway, karibuni sana.
 
Kama mmejipanga vizuri na mmeangalia wapi tulipokosea ktkt hiyo miaka 50 ya uhuru basi tunawatakia kila la kheri...

Hofu yangu ni kuwa kwa sera hizi mbovu za kilimo tulizonazo sijui kama malengo yenu yatatimia. Mkulima mdogo ana matatizo mengi sana ambayo utatuzi wake ni wa kisera. Hata mkiniuzia mbegu leo, nitaendaje kulima kwenye shamba langu lile lile ambalo halipapimwa na siwezi kulitumia kama dhamana ili nipate mkopo wa kuliendeshea? Je mvua ikikatiba baada ya mwezi mmoja kuna insurance yoyote ya kumlipa huyu mkulima kwa nguvu na gharama alizotumia? Anyway, karibuni sana.

MKUU HONGERA SANA KWA HILI NA HILI LITAWAKOMBOA SANA WAKULIMA WA TANZANIA, MAKE KILIMO CHA KISASA NI MUHIMU SANA KATIKA KUFNIKISHA KILIMO KWANZA.

ILA MKUU KUNA MAHALI MIMI NITATOFAUTIANA NA WEWE KIDODO, ILA NI KATIKA KUJENGA NA SI KUBOMOA MKUU,

1. Mkuu Ni kweli wakulima wengi wamekuwa hawafuati njia za kisasa katika kulima,hilo silipingi, ila mkuu kilimo cha Tanzania kina kabiliwa na changamoto moja kubwa sana nayo ni MASOKO

- Mkuu MASOKO ndo tatizo kubwa kwa wakulima wa Tanzania na kuna wakulima wanajitahidi sana kulima kitalaamu lakini hawajui wapi pa kuuza, ni mefanya kazi na NGOs moja inaitwa Faida Market Linkage company, hii ilikuwa na jukumu la kufanya Market Linkage kati ya wakulima na wanunuzi so ilikuwa ni kama Daraja kati ya watu hao wawili,

Mkuu mfano mzurri ni wakulima wa Machungwa kule Tanga, machungwa yanaozea kwenye miti kipindi cha msimu na hawana pa kuyapeleka na wanalazimika kuuza kwa hasara

Kule Kilimanjaro wakulima wamefikia hatua ya kung'oa kahawa waoteshe mazao mengine kisa ni Masoko

Kule kusini mikoa ya Luvuma wakulima huvuna mahindi ya kufa mtu lakini hawana pa kuyauza na inafikia mahali wanaamua kuuza kwa hasara, mkuu hiyo ni mifna michache,

Wakulima wanaweza lima kisasa kabisa but kama hakuna masoko ya uhakika ni kazi bure mkuu na hii ndo tatizo linalo wavunja moyo wakulima wa Tanzania wengi hukata tamaa ya kulima kwa sababu ya masoko ya mazao,

Mkuu kikubwa cha kwanza kinacho takiwa kufanyika ni kutafuta masoko ya uhakika ya wakulima then ukija na mpango huu utafankiwa sana, na kilimo cha biashara ni kitendo cha mkulima kufanya kilimo sawa sawa na biashara nyingine yoyote ile

Kilimo cha biashara inatakiwa mkulima Aingie shambani huku akijua anaamuuzia nani hayo mazao yake, na si mkulima alime then asubiri walanguzi waje na mafuso mashambani, Kilimo cha kisasa bila kuangalia masoko ni kazi bure mkuu, na kilio cha wakulima wa Tanzania ni masoko ya mazao yao,
Cheki mfano wa kilimo cha Pamba, kwa sasa kinakufa kwa sababu ya msoko, kilimo cha tumbaku kinakufa wa sababu ya masoko

SO MKUU KAMA MNAWEZA JARIBU KUFANYA NA MARKET LINKAGE HII IKIENDA PAMOJA NA HIYO KAZI NYINGINE ITAKUWA VIZURI SANA,
 
Heshima kwenu wanajamvi.
Tanzania tumekuwa na sera nyingi za kuendeleza kilimo cha mtanzania (mkulima mdogo mdogo) kwa miaka hamsini sasa. lakini pamoja na sera nyingi na zenye mvuto masikioni tumeshindwa kufikia lengo kama nchi. Moja ya changamoto kubwa ambayo imekuwa ikisahaulika ni wataalamu wenye uwezo wa kumshauri mkulima kwa wakati sahihi juu ya zao gani aoteshe wapi, aoteshe vipi, lini, udhibiti wa magonjwa na wadudu waharibifu, uhifadhi wa udongo kwa kilimo endelevu na matumizi sahihi ya mbolea. hii imekuwa ni changamoto kwa muda mrefu sasa kwa wakulima wa Tanzania ukilinganisha na baadhi nchi za jirani zilizofanikiwa kuboresha kilimo.

Kwa kutambua changa moto hii tumeanzisha consulting firm ambayo kwa sasa ina ofisi zake mjini Morogoro na Moshi ambapo unaweza kupata ushauri sahihi wa kitaalam kuhusiana na kilimo cha mazao yote yanayostawi katika ukanda wa kitropiki (tropical crops) popote ulipo katika Tanzania. Pia tunatoa huduma ya upimaji udogo ili kutambua mahitaji ya rutuba katika udongo, tunauza mbegu mbali mbali zenye ubora na madawa ya kudhibiti wadudu na magonjwa.

kwa wale wafanyabiashara na wafanyakazi wa sekta nyinginezo (zisizo za kilimo) ambao wangependa kulima kibiashara nafasi ndio hii.

Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuni PM au kutumia simu namba 0653649152.

Habari Mkuu ,tunashukuru kwa wazo lako na jitihada hizo. Hebu nijuze ,unayo mbegu ya Mpunga aina gani na ina sifa gani? na bei zikoje ? nijuze hiyo ili tuone kama tutaweza fanya na huduma muhimu,natamani ungekuwa consultant wangu ktk shughuli hizi za kilimo. Kwa utalamu wako Kitunguu maji kinatoka gunia ngapi zenye ujazo gani wa katika ekari moja? na mbegu unayo lkn, ?
 
The idea is good. Tunaposema wasomi kujiajiri tunamaanisha vitu kama hivi. Traditionaly huduma hizi zimekua zikitolewa na serikali kupitia kwa maafisa ugani, ambao wako wachache, hawana vitendea kazi n.k. Kwa kua kilimo ni biashara we can no longer rely on them.
Msijikite tu kwa wakulima wadogo, lakini pia angalieni jinsi gani mnaweza kufanya kazi na wakulima wakubwa. Kwa mfano they can outsource baadhi ya kazi kwenu.

Pia angalieni how you can help kwenye suala la masoko. Pia NGO na serikali can contract you kufanya kazi fulani fulani kuhusu kilimo. Mnatakiwa pia mjenge mtandao mzuri na taasisi za utafiti za mazao mbalimbali, they can contract you to do some extionsion services.
There are millions ideas, however kwenye ujasiliamali katika biashara ya ushari mnahitaji kuwa competent, mdelive siyo longolongo. Nawatakia kila la kheri
 
Back
Top Bottom