Ushauri wa bure: Madereva wa private cars tembeeni usiku kama unafanya Safari ndefu

Kama upo willing kusumbuliwa njia nzima unatembea mchana tu! Zile kero za kupigwa mkono kila baada ya nusu saa hapana! Mara naomba leseni yako, unampa askari anaondoka nayo mnaanza kutongozana wee mambo ya kijinga sana hayo!

Mie siogopi kutembea usiku kama gari naiamini! Taa ziko poa na brakes ziko poa!
Ila mbona ata mchana ukifata vibao vyao vizuri hawasumbui
 
Ujue kusumbuliwa Kuna kuja pale ukiwa na baby warker lazima traffic wakusumbue lakini kana una drive gari la ukweli ma traffic hawakusimamish hovyo hovyo safiria Ford Ranger , Vx V8, BMW x6, Land cruiser ,etc usumbufu kwa matrafic kusimamishwa unapungua .Tafuteni hela mmiliki gari za ukweli muone Kama mtasumbuka njian.
 
Imekuwa desturi na mazoea kwa madereva wengi wanaoendesha magari yao binafsi kufanya safari zao ndefu muda wa mchana ingawa ni jambo jema ila kwa mtazamo wangu mimi naona ni shida na usumbufu mwingi njiani.

Naongea hivyo kwasababu ndani ya mwezi Machi nilifanya safari ndefu ya kwenda Mwanza na gari yangu. Nakumbuka nilianza safari usiku saa 7 kutoka Dar ili kuepusha usumbufu kwenye kipande cha Dar-Moro (kwa wazoefu wa kipande hiki watakubaliana na mimi). Muda wa mchana nilipata shida na usumbufu na traffic pamoja mabus na fujo zao mpaka naingia Mwanza usiku saa 3.

Mpaka nimeamua kuandika ushauri huu ni kwa madereva wenzangu ni ushuhuda niliouona kwa macho yangu wiki hii.

Jumamosi iliyopita nimefanya safari tena nyingine ya kwenda Mwanza kwa kupanda bus hakika vituko vya madereva wa bus ni noma, hawa jamaa wanatumia barabara watakavyo,wanaovertake watakavyo tena sehemu yeyote ile ilimradi amekupita, yaani zile speed za miaka ile zimerudi tena na traffic hawana la kusema kwasababu jamaa alipigwa tochi mara 5 na bado hakupigwa cheti mpaka tunafika Mwanza.

Dereva wa bus alikuwa anaovertake mpaka malori matano hasa pale akiona mbele yake inakuja gari ndogo yaani utake usitake utasimama tu mpaka amalize kuovertake kumbe jamaa wanatudharau sana mpaka wanatuita wamama wa nyumbani (msemo huu alikuwa anautumia dereva wa bus akiwa anafanya fujo zake).

Nimeshuhudia kwenye vibao vya speed 50 magari madogo wanakatwa na traffic huku bus letu linapita tu tena na mwendo mdundo bila shida tena likiwa speed 102 hata ile alarm ya speed hakuna.

Nawashauri madereva wenzangu tembeeni usiku kuepusha majanga mchana haya mambo ya mchana tuwaachiwe wenye njia yao madereva wa mabus kwasabb kama kuna watu wanaenyoj barabaran ni watu wa mabus tu...Wale wenzangu na mm tusione tabu kuendesha usiku
Tatizo la usiku kuna possibility ya mambo ya kutegeana mawe na kuachiana ngeu na vilema vya mapanga
 
Usiku inatakiwa uwe mzoefu sana na usiwe na papara! Nimeendesha usiku Mara nyingi, kuna changamoto kubwa sana sana!

Nimeshaendesha usiku mzima yaani zaidi ya 13hrs, kuna uchovu unaupata muda Fulani ambapo usipokua makini unapoteza.

My recent driving ilikua Sumbawanga to Morogoro, ilikua safari ndefu na nilipata changamoto za hapa na pale lakini nilisinzia Mara kadhaa na kujikuta nalazimika kusimama na kujinyoosha kidogo.

Kama huna macho mazuri, kuna Wapuuzi wanaendeshea full lights na kuna wengine wamefunga zile crystal lights ambazo ni hatari kwa kweli.

Pia kuna magari mabovu na ajali za hapa na pale, hii safari ya mwisho nilijikuta ghafla ni Lori limebeba container la 40ft limeanguka dakika hio saa kumi asubuhi maeneo ya Iyovi tena kwenye kona!
Lilifunga barabara kabisa na muda ule likawa linakuja tanker la mafuta likaligonga lile tanker.

Ni ajali mbaya ambayo ilitufanya tukae hapo kuanzia saa kumi asubuhi hadi saa nne asubuhi ndio tukaondoka.

Hivyo, kama una papara za kukimbia na kupenda ligi, usiku sio mahali salama! Kwa mtazamo wangu.
Dereva anaye sinzia usiku barabarani huyo ni mtu tu na mambo yake na si dereva wa taaluma kama mimi hapa,usiku ndiyo sichoki na ninakata kilometer za kutosha
 
Habari za miaka BelindaJacob

Kuna safari moja almanusura aliyekuwa anatuendesha agonge tembo Mikumi hiyo, usiku mnene tembo anatoka upande huu anaenda upande wa pili...

Kama sio kumshtua, pengine yule tembo angelituletea balaa, kwanza kwa kujeruhiwa na pili faini ya tembo sio ya kitoto...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nzuri sana, naamini kwema pande zako Watu8

Ndo maana usiku sipendi kusafiri. Imagine jamaa angegonga huyo tembo. Usiku kuna Mengine mkuu.
 
Hahahah mnyama akikatiza humuoni au 😂😂😂
Kuna ile ghafla bin vu, mkuu. Na hii sitasahau kudrive (sikuwa dereva) toka Maputo to Durban, kuna sehemu na vibao vya tahadhari vimewekwa kuwa wanyama kama ng’ombe wanakatiza. Kuna mmoja alitusababishia kizaa zaa, giza halafu mvua. Sitosahau lile tukio.
 
Kuna ile ghafla bin vu, mkuu. Na hii sitasahau kudrive (sikuwa dereva) toka Maputo to Durban, kuna sehemu na vibao vya tahadhari vimewekwa kuwa wanyama kama ng’ombe wanakatiza. Kuna mmoja alitusababishia kizaa zaa, giza halafu mvua. Sitosahau lile tukio.
Mvua kali usiku haifai unaendesha speed 60 tu maximum mpaka pawe clear
 
Kutembea usiku kuna raha yake ila barabara ya Mwanza shinyanga ni mbaya aisee. Kwanza ina matuta kurupushi, pili matuta yake ni yale tuta mrusho. Tuta kama gogo. Safari ya Dom Mwanza unaweza tumia masaa sita mwanza hadi shinyanga ila ukatumia hata manne kutoka shinyanga kwenda Mwanza
 
Back
Top Bottom