Extrovert
JF-Expert Member
- Feb 29, 2016
- 66,989
- 173,601
Ntakufuturu wewe 😂😂😂 shaur lakoKwani kelele ya upepo unasemaje
Najua hulipendi hili neno
Ntakufuturu wewe 😂😂😂 shaur lakoKwani kelele ya upepo unasemaje
Najua hulipendi hili neno
Soon nachukua chuma kama yako...... Then tumeet tufundishane namna ya kuzitunza............Kwani kelele ya upepo unasemaje
Najua hulipendi hili neno
Imenisaidia mara kadhaa. Ni kiasi cha kuwa serious tu; pia ikitegemeana na muonekano wako na usafiri unaotumia. Wengine tuna sura za kikauzu, ukisema kitu unaaminika mara moja.Unafikiri ndio itaku save hio mbinu na wao wanajua ni uongo tu! Wanajuwa wazi unadanganya na hapo ndipo atapoanza kukusumbulia!
Chuma gani? Hebu nidokeze nione kama umeotea!Soon nachukua chuma kama yako...... Then tumeet tufundishane namna ya kuzitunza............
Ila mbona ata mchana ukifata vibao vyao vizuri hawasumbuiKama upo willing kusumbuliwa njia nzima unatembea mchana tu! Zile kero za kupigwa mkono kila baada ya nusu saa hapana! Mara naomba leseni yako, unampa askari anaondoka nayo mnaanza kutongozana wee mambo ya kijinga sana hayo!
Mie siogopi kutembea usiku kama gari naiamini! Taa ziko poa na brakes ziko poa!
Utafika sangapi sasa huko unakoenda? Hujasikia habari ya kubambikiwa makosaIla mbona ata mchana ukifata vibao vyao vizuri hawasumbui
Ukiwa na gari ndogo umbali wa dar to Dodoma waweza simamishwa hata mara 20 kukaguliwa lakini Kama una gari la maana kusimamishwa hupungua Sana , safiria land cruiser hard top uone Kama utasimamishwa sasa ukisafiria spacio and hizo baby warker utasimamishwa kukaguliwa hadi utakomaIla mbona ata mchana ukifata vibao vyao vizuri hawasumbui
Tatizo la usiku kuna possibility ya mambo ya kutegeana mawe na kuachiana ngeu na vilema vya mapangaImekuwa desturi na mazoea kwa madereva wengi wanaoendesha magari yao binafsi kufanya safari zao ndefu muda wa mchana ingawa ni jambo jema ila kwa mtazamo wangu mimi naona ni shida na usumbufu mwingi njiani.
Naongea hivyo kwasababu ndani ya mwezi Machi nilifanya safari ndefu ya kwenda Mwanza na gari yangu. Nakumbuka nilianza safari usiku saa 7 kutoka Dar ili kuepusha usumbufu kwenye kipande cha Dar-Moro (kwa wazoefu wa kipande hiki watakubaliana na mimi). Muda wa mchana nilipata shida na usumbufu na traffic pamoja mabus na fujo zao mpaka naingia Mwanza usiku saa 3.
Mpaka nimeamua kuandika ushauri huu ni kwa madereva wenzangu ni ushuhuda niliouona kwa macho yangu wiki hii.
Jumamosi iliyopita nimefanya safari tena nyingine ya kwenda Mwanza kwa kupanda bus hakika vituko vya madereva wa bus ni noma, hawa jamaa wanatumia barabara watakavyo,wanaovertake watakavyo tena sehemu yeyote ile ilimradi amekupita, yaani zile speed za miaka ile zimerudi tena na traffic hawana la kusema kwasababu jamaa alipigwa tochi mara 5 na bado hakupigwa cheti mpaka tunafika Mwanza.
Dereva wa bus alikuwa anaovertake mpaka malori matano hasa pale akiona mbele yake inakuja gari ndogo yaani utake usitake utasimama tu mpaka amalize kuovertake kumbe jamaa wanatudharau sana mpaka wanatuita wamama wa nyumbani (msemo huu alikuwa anautumia dereva wa bus akiwa anafanya fujo zake).
Nimeshuhudia kwenye vibao vya speed 50 magari madogo wanakatwa na traffic huku bus letu linapita tu tena na mwendo mdundo bila shida tena likiwa speed 102 hata ile alarm ya speed hakuna.
Nawashauri madereva wenzangu tembeeni usiku kuepusha majanga mchana haya mambo ya mchana tuwaachiwe wenye njia yao madereva wa mabus kwasabb kama kuna watu wanaenyoj barabaran ni watu wa mabus tu...Wale wenzangu na mm tusione tabu kuendesha usiku
Hakuna kitu kama hicho tena ni hadith za kale Sana hizoTatizo la usiku kuna possibility ya mambo ya kutegeana mawe na kuachiana ngeu na vilema vya mapanga
Dereva anaye sinzia usiku barabarani huyo ni mtu tu na mambo yake na si dereva wa taaluma kama mimi hapa,usiku ndiyo sichoki na ninakata kilometer za kutoshaUsiku inatakiwa uwe mzoefu sana na usiwe na papara! Nimeendesha usiku Mara nyingi, kuna changamoto kubwa sana sana!
Nimeshaendesha usiku mzima yaani zaidi ya 13hrs, kuna uchovu unaupata muda Fulani ambapo usipokua makini unapoteza.
My recent driving ilikua Sumbawanga to Morogoro, ilikua safari ndefu na nilipata changamoto za hapa na pale lakini nilisinzia Mara kadhaa na kujikuta nalazimika kusimama na kujinyoosha kidogo.
Kama huna macho mazuri, kuna Wapuuzi wanaendeshea full lights na kuna wengine wamefunga zile crystal lights ambazo ni hatari kwa kweli.
Pia kuna magari mabovu na ajali za hapa na pale, hii safari ya mwisho nilijikuta ghafla ni Lori limebeba container la 40ft limeanguka dakika hio saa kumi asubuhi maeneo ya Iyovi tena kwenye kona!
Lilifunga barabara kabisa na muda ule likawa linakuja tanker la mafuta likaligonga lile tanker.
Ni ajali mbaya ambayo ilitufanya tukae hapo kuanzia saa kumi asubuhi hadi saa nne asubuhi ndio tukaondoka.
Hivyo, kama una papara za kukimbia na kupenda ligi, usiku sio mahali salama! Kwa mtazamo wangu.
Nzuri sana, naamini kwema pande zako Watu8Habari za miaka BelindaJacob
Kuna safari moja almanusura aliyekuwa anatuendesha agonge tembo Mikumi hiyo, usiku mnene tembo anatoka upande huu anaenda upande wa pili...
Kama sio kumshtua, pengine yule tembo angelituletea balaa, kwanza kwa kujeruhiwa na pili faini ya tembo sio ya kitoto...
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna ile ghafla bin vu, mkuu. Na hii sitasahau kudrive (sikuwa dereva) toka Maputo to Durban, kuna sehemu na vibao vya tahadhari vimewekwa kuwa wanyama kama ng’ombe wanakatiza. Kuna mmoja alitusababishia kizaa zaa, giza halafu mvua. Sitosahau lile tukio.Hahahah mnyama akikatiza humuoni au 😂😂😂
Mvua kali usiku haifai unaendesha speed 60 tu maximum mpaka pawe clearKuna ile ghafla bin vu, mkuu. Na hii sitasahau kudrive (sikuwa dereva) toka Maputo to Durban, kuna sehemu na vibao vya tahadhari vimewekwa kuwa wanyama kama ng’ombe wanakatiza. Kuna mmoja alitusababishia kizaa zaa, giza halafu mvua. Sitosahau lile tukio.