Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 733
Mimi ni miongoni mwa waTanzania wengi tunaopenda kuangalia filamu zetu za hapa Bongo lakini wengi wetu tunakatishwa tamaa na maudhui ndani ya filamu hizo. Nyingi zimejaa mambo ya anasa, majumba na magari ya kifahari ambayo hayaleti taswira halisi ya Watanzania wa kawaida mabo tuko wengi.
Badala ya kuiga wenzetu wa kule Nigeria ni bora mngekuja na filamu zinazobeba maudhui ya maisha ya kawaida ya Mtanzania hivyo kupiga hatua kwa kupendwa na waTanzania wenyewe pamoja na hata nchi za jirani na ama kwa hakika tutafika mbali. Hebu badilikeni jamani twazipenda sana kazi zenu ila mnaelekea upande ambo si wenyewe la sivyo tutaendelea kuangalia series za nje na soka la Uingereza.
Picha kama hizi hazina mvuto wowote maana hazibebi uhalisia wa maisha yetu
Haya ndio maisha yetu halisi mwaweza tumia maudhi haya na mkauza sana kazi zetu
Badala ya kuiga wenzetu wa kule Nigeria ni bora mngekuja na filamu zinazobeba maudhui ya maisha ya kawaida ya Mtanzania hivyo kupiga hatua kwa kupendwa na waTanzania wenyewe pamoja na hata nchi za jirani na ama kwa hakika tutafika mbali. Hebu badilikeni jamani twazipenda sana kazi zenu ila mnaelekea upande ambo si wenyewe la sivyo tutaendelea kuangalia series za nje na soka la Uingereza.
Picha kama hizi hazina mvuto wowote maana hazibebi uhalisia wa maisha yetu
Haya ndio maisha yetu halisi mwaweza tumia maudhi haya na mkauza sana kazi zetu