Ushauri wa bure kwa serikali juu polisi. Wanachukiwa sana mtaani

Mara nyingi Huwa napendelea kuonekana mjinga ( being underated/ underestimated). Napendelea kujiweka muonekano usiolingana na uwezo wa akili yangu, kipato changu na elimu yangu.

Wiki iliyopita nilijaza fomu la online loss report Kisha nikaenda kituo cha police kuthibitishiwa hiyo loss report ili niende stationery ku print. Yule polisi mhusika akanidai TZS 5,000 ilihali huduma ni bure ukishalipia ile TZS 500 kwa control number. Tangu siku ile (na matukio mengine kwa nyakati tofauti tofauti) polisi nawachukulia ni watu wa hovyo hovyo na nawashauri wamama wasiwe wanawazaa watu wa hovyo hovyo kama polisi wa nchi hii, kama bwana Zero anavyomchukulia Hamza kuwa ni mtu wa hovyo hovyo na kuwashauri wamama wasiwe wanawazaa watu wa hovyo hovyo kama Hamza.

Ushauri:
Serikali kwa upande Wake, inapaswa kuipa thamani stahili idara ya polisi kwa kuwaajiri watu wenye elimu nzuri na utimamu wa akili na siyo miguvu tu bila akili ( power without knowledge is globally agreed to be useless). Kuna maelfu ya graduates wanazitaka hizo kazi nawana uwezo mzuri tu.

Serikali wapeni graduates kozi ya JKT angalau ya miezi mitatu Kisha muwapeleke shule ya polisi, muone mapinduzi chanya katika idara hii muhimu iliyoigeuza taswira ya Tazanzania kuwa Taifa la walalamikaji kando na wao kuishi maisha ya kihayawani.
Mwanangu una hoja yenye mashiko. Wakati wa kuajiri vihiyo umekwishapita.
 
Hii report zamani ulikuwa unaotoa ukiwa nyumban mwenywe sasa ivi wanaminya ila wapate hela ya maji ajabu sana
Zamani ukiweka namba za NIDA unapeta haina haja kwenda kituoni kuthibitisha ila juzi kati ilinigomea si ndio nikaenda kituoni pale Magomeni kuthibithisha.
Ajabu ni kwamba haki ya kuthibitisha amepewa mwenye stationary pale nje ya kituo...........
Anathibitisha na kuprint kabisa then unalipishwa buku 2 kwa loss report moja, nadhani jamaa wana mgao wao humo
 
Chuki zenu kwa Polisi zinawafanya tunaoishi nao mtaani wakifua uniform zao waanike ndani na hata kuzivaa wanavalia vituoni mwao..
 
Mimi hao jamaa siwapendi

Juzi Kati walitaka muuzia kesi mtu wangu wa karibu .

Hao watu siwakubali

At leas masoja hawana nuksi raia ila hao wavaa khaki washenzi sana
 
Mimi pia Mkuu halafu ilikuwa kesi mbaya sana lakini Mwenyezi Mungu mkubwa pale Oyster Bay polisi waliniweka ndani kama masaa matano nikatoka saa moja usiku na kunitaka niripoti pale kila siku asubuhi saa moja hakukuwa na cha maana baada ya one hour wananiambia unaweza kwenda urudi tena kesho saa moja asubuhi. Wakaanza kuomba rushwa na kunitisha kesi ni mbaya sana nikawaambia sina hela ya mchezo. Bahati nzuri ushahidi ukaniweka huru kwamba sikufanya kosa lolote hata kuniambia niko huru hawakuniambia kwa aibu lakini sikuwasikia tena.
Aise,ilikuwaje kisa nini

Ova
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Kuna majizi pale bohari kuu yaliiba madawa ya binadamu wakayaweka majumbani mwao ili kutafuta wateja. Bomu lilipobumburuka kwamba wataenda kusachiwa majumbani wakaamua kwenda kuyaficha madawa hayo kwenye vichaka mbuzi. Jamaa zangu wakayaona yale maboksi na kushangaa mbona yamefungwa vizuri tena kama yamefichwa? Wakaamua kuyafungua na kukuta vidonge kibao. Basi jamaa wakaona pesa hii tuyabebe. Basi wakayebeba tukakutana nao mtaani na kwa kuwa nafahamiana nao tukasalimiana kama washkaji wa karibu. Kumbe wakati nasalimiana nao manjangu yalikuwa yanapita kwenye mkoko wao. Wakaona ile movie na kuamua kugeuza kurudi. Walivyorudi bila hata ya kuuliza wote kwenye mkoko wao kituoni kuandikisha maelezo na polisiccm wakaandika maelezo yao uongo mtupu (baada ya jamaa zangu pale kituoni kuwaambia kuna vidonge na hawajui ni vya nini)?mwanzo mwisho. Baada ya kama masaa machache mimi nikatoka lupango na kuwastua wazazi wa jamaa nao wakatolewa. Jamaa wakanifuata home kuanza kunitisha kesi mbaya sana hii bila michuzi utaozea lupango. Nikawaambia sina pesa ya mchezo maelezo yangu niliyoyaandika ni ukweli MTUPU na jamaa zangu japo sikuwepo walipoyaokuta hayo mabox lakini nawaamini 110%. Basi wakaniambia kila siku saa moja asubuhi uripoti kituoni Oyster Bay polisi.

Nikawa naenda nakaa benchi ikifika saa mbili haya nenda urudi tena kesho saa moja asubuhi. Baada ya siku nne wakaniambia tunajua unapoishi hivyo tukikuhitaji tutakufuata kwako hakuna sababu ya kuja tena. Bahati nzuri yale mabox yakaendelea kuokotwa kwa wingi ná vidonge ni vile vile yamefungwa vizuri kwenye vichaka mbuzi.

Kwa hiyo kuendelea kuokotwa mabox yale ndiyo ikawa salama yetu vinginevyo tulikuwa tumeshabambikiwa kesi mbaya sana.

Aise,ilikuwaje kisa nini

Ova
 
Mkuu umewaza mbali sana, CCM sio wajinga wawapeleke graduates shule ya polisi. graduates yupi atakubali kusimamia wizi WA kura au kukimbia na box la kura? So kupeleka wenye elimu ndogo ndio Namna ya chama tawala kupata kundi la kukilinda.
Kuna walimu wana masters nawajua!! Walichokifanya mwaka jana Mungu awasamehe wajinga wale
 
Graduates wa kwanza kufikiriwa wawe wa sheria. Polisi wetu wengi hawana msingi wa sheria. Polisi bila sheria amani hakuna. Nilishangaa kuambiwa hata IGP aliopo kitaaluma ni mwalimu, nilichoka!

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Kuna sehemu nilisoma kuwa Sirro ni mwanasheria. Nilibaki hoi vile vile!
 
..
20210921_170848.jpg
 
Back
Top Bottom