Kaka umemaliza kila kituNi kweli Mavoko ana uwezo mzuri wa kutunga mashairi mazuri, ushahidi ni wimbo wake wa Ibaki Stori - Niwimbo wenye mashairi mengi sana.
- Lakini nyimbo za aina hiyo haziuzi ulimwenguni licha ya kupendwa hapa Tanzania, Mavoko tayari ana jina hapa bongo na anachokiangalia ni soko kubwa zaidi na kwa sababu huko hawaelewi unaimba nini - huwezi kuimba mashairi kibao kama kwenye Ibaki stori .Ndio maana unaona wameimba wenye mashairi mafupi mafupi tena ni wimbo wa burudani tu "Club Banger "
- Hata Diamond bado ana uwezo huo wa kutunga mashairi kama ya zamani ,ushaidi sikiliza matangazo aliyotengeneza yanavyokiki.
- Lakini kwasababu za kibiashara inatakiwa ubadilike badilike ili uuze maana muziki ni biashara huwezi kukommaa na kitu kwa sifa tu wakati huuzi.