GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,542
- 108,858
1. Mechi yenu ihamisheni kutoka Chamazi na muipeleke kwa Mkapa / kwa Mchina.
2. Fanyeni Kiingilio kiwe Tsh 1,500/ na Wanawake bure.
3. Hakikisheni kila anayeiingia Uwanjani anapewa ama Maziwa madogo au Ukwaju
4. Tafuteni Wasanii wakubwa na wanaokubalika ili wawe pia ni Kivutio.
5. Tengeni Jezi zenu baadhi kisha mzigawe bure ili angalau Uwanjani Siku hiyo rangi zenu zitawale.
6. Wakati wa Mapumziko toeni hata Maji yale madogo bure kabisa kwa Mashabiki watakaoingia Uwanjani.
7. Kama itakuwa ndani ya uwezo wenu tengeni Mabasi ya Kusafirisha Mashabiki katika Wilaya zote Tano za Mkoa wa Dar es Salaam.
Nimesema haya yote nikiwa na sababu moja kubwa tu kwamba hakuna asiyejua na hapa wala tusidanganyane kwamba Mashabiki wengi nchini Tanzania ni wa Simba SC na Yanga SC hivyo ili kuwapata katika Timu zingine pale zinapocheza hasa hii Michuano ya Kimataifa kunahitaji Mbinu kubwa, kali na zenye Ushawishi wa hali ya juu ( kama nilizozitaja hapo juu ) ili Uwanja ujae na pia mshangiliwe. Na najua kwa aina ya Utajiri alionao Mzee Bakhressa ( SS ) hayo yote kama yakiratibiwa vizuri yanawezekana na Azam FC itapata Sapoti Kubwa na nina uhakika itashinda tena kwa idadi Kubwa tu ya Magoli.
Huu ndiyo Uzalendo wangu wa ukweli Kwenu Azam FC kwani nawapendeni kuliko wale Wapuuzi wengine wa Bwawani.
Nawatakieni Maandalizi mema ya Mechi yenu hiyo ya marudiano na najua mtashinda tu kama ambavyo tunaoujua vyema Mpira na Timu ya Mwenyezi Mungu Simba Sports Club nayo itakavyoenda Kushinda Mechi yake ya marudiano Siku ya Jumapili dhidi ya Wamachinga wa Nchumbiji ( Mozambique )
Na kuna Litimu fulani hivi silipendi kweli kweli naliombea Balaa Kubwa ikicheza Jumamosi ili ifungwe na itolewe kabisa.
2. Fanyeni Kiingilio kiwe Tsh 1,500/ na Wanawake bure.
3. Hakikisheni kila anayeiingia Uwanjani anapewa ama Maziwa madogo au Ukwaju
4. Tafuteni Wasanii wakubwa na wanaokubalika ili wawe pia ni Kivutio.
5. Tengeni Jezi zenu baadhi kisha mzigawe bure ili angalau Uwanjani Siku hiyo rangi zenu zitawale.
6. Wakati wa Mapumziko toeni hata Maji yale madogo bure kabisa kwa Mashabiki watakaoingia Uwanjani.
7. Kama itakuwa ndani ya uwezo wenu tengeni Mabasi ya Kusafirisha Mashabiki katika Wilaya zote Tano za Mkoa wa Dar es Salaam.
Nimesema haya yote nikiwa na sababu moja kubwa tu kwamba hakuna asiyejua na hapa wala tusidanganyane kwamba Mashabiki wengi nchini Tanzania ni wa Simba SC na Yanga SC hivyo ili kuwapata katika Timu zingine pale zinapocheza hasa hii Michuano ya Kimataifa kunahitaji Mbinu kubwa, kali na zenye Ushawishi wa hali ya juu ( kama nilizozitaja hapo juu ) ili Uwanja ujae na pia mshangiliwe. Na najua kwa aina ya Utajiri alionao Mzee Bakhressa ( SS ) hayo yote kama yakiratibiwa vizuri yanawezekana na Azam FC itapata Sapoti Kubwa na nina uhakika itashinda tena kwa idadi Kubwa tu ya Magoli.
Huu ndiyo Uzalendo wangu wa ukweli Kwenu Azam FC kwani nawapendeni kuliko wale Wapuuzi wengine wa Bwawani.
Nawatakieni Maandalizi mema ya Mechi yenu hiyo ya marudiano na najua mtashinda tu kama ambavyo tunaoujua vyema Mpira na Timu ya Mwenyezi Mungu Simba Sports Club nayo itakavyoenda Kushinda Mechi yake ya marudiano Siku ya Jumapili dhidi ya Wamachinga wa Nchumbiji ( Mozambique )
Na kuna Litimu fulani hivi silipendi kweli kweli naliombea Balaa Kubwa ikicheza Jumamosi ili ifungwe na itolewe kabisa.