Erick_Otieno
JF-Expert Member
- Mar 28, 2010
- 624
- 1,020
Hodiii mashosti na kaka zangu
Kwanza asanteni kwa ukaribisho mubashara...ati naskia thread yangu ya utambulisho ndio ya kwanza kuwa na replies nyingi hadi 500-600 comments! I was honored.
Hii ni thread yangu ya pili, naomba kuzungumzia/kutoa ushauri kwa waajiri/employers hasa wenye taasisi au makampuni either mapya au yenye muda mrefu kwenye industry husika:
Binafsi naamini ukuaji wa kampuni unachangiwa kwa kiasi kikubwa na wafanyakazi hasa wazalendo, wenye motisha na wajuzi. Lakini wewe kama mwajiri usipojua namna ya kuishi nao na kufanya nao kazi kwakweli taasisi/kampuni yako itakuwa ya kusuasua au maendeleo yake yatakuwa mazito.
Wafanyakazi hukerwa na bosi asiyejua ethics za Human Relation na asiyetambua umuhimu wa wafanyakazi individually. Bosi mwenye kasoro hizi ni yule ambae either biashara sio yake, yaani hajahussle kuwa hapo, au ni ya kurithi, au kapewa nafasi hiyo kwa njia zisizo halali kam vile undugu, rushwa n.k. bila kuzingatia uwezo wake kiuongozi, kikazi na kitaaluma.
Hali hiyo hupelekea bosi huyu kuwa mwenye kiburi, majivuno na kutokujali japo anaweza asioneshe dalili hizi kwa uwazi, hivyo kujikuta anachukiwa na wafanyakazi au kuajiri na kufukuza kila mara, kitu kinachopunguza ufanisi wa kampuni kiutendaji.
Nawashauri waajiri/mabosi msitengeneze gape kati yenu na wafanyakazi na ubosi wenu. Wafanye wafanyakazi waone kuwa na wao ni sehemu ya kampuni, kwamba na wewe ni mfanyakazi unaepaswa kutekeleza majukumu yako kama wao. Na hata kama umeajiri ndugu zako, hakikisha ni wenye taaluma na wanaoheshimu staff wengine bila kubebwa na uhusiano wenu.
Kuwa friendly, mfanyie surprise ya Happy Birthday mfanyakazi wako, wape overtime pale inapobidi, heshimu wafanyakazi wanokuzidi umri, na usionyeshe nguvu ya mamlaka yako hasa unapokwazika.
Mwisho wa siku, staff watakuamini sana na kila mmoja atakuwa ni kama mlinzi wako na mlinzi wa mwenzie, hata wakifikiria kuibia kampuni nafsi zinawasuta, watakuja kazini kumaliza kazi na sio kusubiri muda wa kazi uishe warudi nyumbani.
Ni hayo tu kutoka kwa Husna Husnadat a.k.a The BossLady
Kwanza asanteni kwa ukaribisho mubashara...ati naskia thread yangu ya utambulisho ndio ya kwanza kuwa na replies nyingi hadi 500-600 comments! I was honored.
Hii ni thread yangu ya pili, naomba kuzungumzia/kutoa ushauri kwa waajiri/employers hasa wenye taasisi au makampuni either mapya au yenye muda mrefu kwenye industry husika:
Binafsi naamini ukuaji wa kampuni unachangiwa kwa kiasi kikubwa na wafanyakazi hasa wazalendo, wenye motisha na wajuzi. Lakini wewe kama mwajiri usipojua namna ya kuishi nao na kufanya nao kazi kwakweli taasisi/kampuni yako itakuwa ya kusuasua au maendeleo yake yatakuwa mazito.
Wafanyakazi hukerwa na bosi asiyejua ethics za Human Relation na asiyetambua umuhimu wa wafanyakazi individually. Bosi mwenye kasoro hizi ni yule ambae either biashara sio yake, yaani hajahussle kuwa hapo, au ni ya kurithi, au kapewa nafasi hiyo kwa njia zisizo halali kam vile undugu, rushwa n.k. bila kuzingatia uwezo wake kiuongozi, kikazi na kitaaluma.
Hali hiyo hupelekea bosi huyu kuwa mwenye kiburi, majivuno na kutokujali japo anaweza asioneshe dalili hizi kwa uwazi, hivyo kujikuta anachukiwa na wafanyakazi au kuajiri na kufukuza kila mara, kitu kinachopunguza ufanisi wa kampuni kiutendaji.
Nawashauri waajiri/mabosi msitengeneze gape kati yenu na wafanyakazi na ubosi wenu. Wafanye wafanyakazi waone kuwa na wao ni sehemu ya kampuni, kwamba na wewe ni mfanyakazi unaepaswa kutekeleza majukumu yako kama wao. Na hata kama umeajiri ndugu zako, hakikisha ni wenye taaluma na wanaoheshimu staff wengine bila kubebwa na uhusiano wenu.
Kuwa friendly, mfanyie surprise ya Happy Birthday mfanyakazi wako, wape overtime pale inapobidi, heshimu wafanyakazi wanokuzidi umri, na usionyeshe nguvu ya mamlaka yako hasa unapokwazika.
Mwisho wa siku, staff watakuamini sana na kila mmoja atakuwa ni kama mlinzi wako na mlinzi wa mwenzie, hata wakifikiria kuibia kampuni nafsi zinawasuta, watakuja kazini kumaliza kazi na sio kusubiri muda wa kazi uishe warudi nyumbani.
Ni hayo tu kutoka kwa Husna Husnadat a.k.a The BossLady