Ushauri wa Bure juu ya gari yako

habarini za asubuhi, Natumia gari aina ya HONDA juzi imeniwashia taa ya kuashiria mafuta ya mepungua nikaongeza lakini mpaka sasa bado inawasha tu hiyo taa. Na tatizo jingine ni kama la mwenzangua hapo juu ila mm niweka D (DRIVE) nikikanyaga brake gari inakuwa ina vabrate Ila nikiweka P (parking) inatulia. Naomnbeni msaada
 
Yeah tena niko komfotabo kabisa. Spea naenda kuchonga mwenyewe pale Veta Chang'ombe.
Hahah we kavu sana mzee baba hilo linafaa zaidi porini, nina jamaangu analo moja anavushia magogo ya miti ya mbao lina towing capacity ya ajabu.
 
habarini za asubuhi, Natumia gari aina ya HONDA juzi imeniwashia taa ya kuashiria mafuta ya mepungua nikaongeza lakini mpaka sasa bado inawasha tu hiyo taa. Na tatizo jingine ni kama la mwenzangua hapo juu ila mm niweka D (DRIVE) nikikanyaga brake gari inakuwa ina vabrate Ila nikiweka P (parking) inatulia. Naomnbeni msaada
Msaada wa kwanza anza kutafuta mteja wa hio gari, siku nyingine usinunue gari inayoitwa Honda. Hao fani yao ni pikipiki tu na majenereta kwenye magari hamna kitu ni majanga tu kuanzia RVR, CR-V n.k

Kingine fanya diagnosis ya system ya mafuta
 
Msaada wa kwanza anza kutafuta mteja wa hio gari, siku nyingine usinunue gari inayoitwa Honda. Hao fani yao ni pikipiki tu na majenereta kwenye magari hamna kitu ni majanga tu kuanzia RVR, CR-V n.k

Kingine fanya diagnosis ya system ya mafuta
Mkuu kwa hiyo magari yao ni fake au? na mbona hizi gari zinasifika saana na pia himself nimekaa nayo sana toka 2014 hadi sasa cjaona tatizo lake tofauti na lililojitokeza . Hata ivi majuzi nimeona company yao iki introduce matoleo yao mapya ya honda.
Kama zipo kasoro nisizo zifahamu kwa uelewa wangu hebu nisaidie maana nimetokea kuvutiwa na mateleo yao mapya, kabla sijaanza kufanya negotiate.
 
Mkuu kwa hiyo magari yao ni fake au? na mbona hizi gari zinasifika saana na pia himself nimekaa nayo sana toka 2014 hadi sasa cjaona tatizo lake tofauti na lililojitokeza . Hata ivi majuzi nimeona company yao iki introduce matoleo yao mapya ya honda.
Kama zipo kasoro nisizo zifahamu kwa uelewa wangu hebu nisaidie maana nimetokea kuvutiwa na mateleo yao mapya, kabla sijaanza kufanya negotiate.
Sio fake ila nadhani kuna shida kwenye quality control section. Lisipokusumbua una bahati sana ili likianza shida ndio balaa limeanza, hasa gearbox yao ndio sumbufu zaidi.
 
Dah, huu uzi unadhihirisha kiasi gani watanzania tunaendesha magari mabovu aisee. Magu aangalie namna ya kulegeza kodi watu wanunue gari zikiwa walau na miaka 4 toka zitoke kiwandani.

Hii mitumba ya magari ya miaka 10 iliopita ina tabu sana!
Achs porojo Mkuu weka ujuzi wako hapa ndio ishakuwa tatizo (joke)
 
Tusamehe watanzania tunapenda Toyota tena za miaka kumi
Kama kuna gari nazishangaaga ni gari za 1999 zinazouzwa kwa mbwembwe ati Suzuki Escudo, RAV 4 milango tano , T xxx DQS gari haijapata ajali bei 15.5m like serious 😂😂😂😂😂???

Gari iko kama mtambo ndani wierd looking interiors full of plastics. Tuwaachie kina mangi tu zile gari.
 
Kama kuna gari nazishangaaga ni gari za 1999 zinazouzwa kwa mbwembwe ati Suzuki Escudo, RAV 4 milango tano , T xxx DQS gari haijapata ajali bei 15.5m like serious ???

Gari iko kama mtambo ndani wierd looking interiors full of plastics. Tuwaachie kina mangi tu zile gari.
Hapa naona mpare Mshana Jr atakuja na mbwebwe za BMW wakati kaumbiwa RAV4,.......ila Tanzania in dampo asee na tunapigwa haswaa
 
gari yangu escudo 1993 engine g16a tokea majuzi haipig starter nikipiga inalia "tap tap"
nikajua battery nikaja nikaboost lakin hivo hivo nimepark tokea majuzi natumia bodaboda..
Je inaweza ikawa ni starter
.???

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni contact za kwenye starter zimeisha unatakiwa uzibadili ili kugundua vizuri chukua plies gonga gonga kwenye starter usigonge kwa nguvu gonga pole pole mimi nimezibadili wiki 5 zilizopita gharama yake ni 20,000
 
Ni contact za kwenye starter zimeisha unatakiwa uzibadili ili kugundua vizuri chukua plies gonga gonga kwenye starter usigonge kwa nguvu gonga pole pole mimi nimezibadili wiki 5 zilizopita gharama yake ni 20,000
Nina hii gari 3doors nataka nipige safari km 500 hivi sijui itafika ..
 
Gari ikichemsha:
Usikimbilie kuizima, iache ikae ikiunguruma then fungua boneti. Tafuta kitambaa kizito au kikubwa na maji safi mengi. Ukiwa umeshika kile kitambaa fungua Radiator valve taratibu (usiifungue kwa mara moja kuna mvuke unaweza kukuua) zungusha mpaka mwisho raditor valve then usiiitoe ila uwe unafanya kama kuinua na kurudisha chini taratibu (mantiki nzima ule mvuke upate nafasi ya kutoka).
Utakapoona hakuna mvuke unaotoka tena ndio ondoa sasa huo mfuniko, chukua maji yako uwe unamimina kwenye radiator usiogope kutokota baada ya muda yataacha (maji yawe mengi sio hizi chupa za lita 1).
Maji yakiacha tokota na yakawa yamejaa basi funga mfuniko wako na hakikisha boneti imejilock ndio ondoa gari!.
NB: Gari ikichemsha usikimbilie kuizima!.
Nyongeza kidgo. Na kama ikiwa imezima kabisa, subiri ipoe ndio uanze hizo hatua hapo juu
 
Toyota wish fuel consumption ipo juu sana. Pia asubuhi inavibrate sana, ikiwa parking au reverse inatoa muungurumo wa juu na inavibrate.

Asubuhi inatoa moshi mweupe kwa muda km dakika 15 kisha unakata. Afu muungurumo wake inakuwa kama kuna tundu pahala. Vilevile break inabidi nipump mara tatu,, bila hivyo inafeli na inapiga kellele za vyuma kama vinagongana.

Kingine inakuwa na miss, asubuhi ama kwenye baridi ndo inasikika zaidi.
 
Toyota wish fuel consumption ipo juu sana. Pia asubuhi inavibrate sana, ikiwa parking au reverse inatoa muungurumo wa juu na inavibrate.

Asubuhi inatoa moshi mweupe kwa muda km dakika 15 kisha unakata. Afu muungurumo wake inakuwa kama kuna tundu pahala. Vilevile break inabidi nipump mara tatu,, bila hivyo inafeli na inapiga kellele za vyuma kama vinagongana.

Kingine inakuwa na miss, asubuhi ama kwenye baridi ndo inasikika zaidi.
Moshi mweupe injini ina tstizo fikisha kwa fundi
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom