Ushauri: Viongozi wetu wa kiserikali wapewe taarifa za vikao mapema kuepusha mwendokasi/ajali kutoka na kwenda Dodoma

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,196
25,516
Kwasasa Ofisi zote za kiserikali, achilia mbali Ikulu, zimehalia Dodoma katika utekelezi wa Sheria na agizo la kuhamia Makao Makuu ya nchi Dodoma. Lakini, bado kuna baadhi ya ofisi zinaendelea na huduma ndani ya Dar es Salaam.

Pia, bado kuna vikao mbalimbali vya kiserikali na kichama vinafanyika Dar es Salaam. Katika hilo, safari za viongozi na watumishi wa Serikali kwenda na kutoka Dodoma ni za mara kwa mara. Ni kwa ajili ya kuhudhuria vikao Dodoma au Dar es Salaam; kupeleka nyaraka na kadhalika.

Jana, kwa mfano, Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai alisafiri kutoka Dodoma kuja Dar es Salaam kuhudhuria kikao cha Kamati Kuu ya CCM kinachotajwa kufanyika leo. Msafara wa Spika ulinipita jana jioni maeneo ya Kibaha. Hakika, ulikuwa kasi na 'ulifanya kila linalowezekana' uwahi Dar es Salaam.

Nashauri viongozi wetu wapewe taarifa za vikao au safari mapema ili wasafiri mapema na kwa utulivu. Hii itapunguza mwendo kasi wa viongozi wetu na watumishi wa umma na kuepusha ajali zinazoweza kujitokeza.
 
Mkuu, mwendo mkali sio kwa sababu ya kuchelewa bali ni kwa ajili ya usalama. Kuna watu wanaoweza kutoifahamu kuwepo kwa kikao mapema lakini sio Spika wa Bunge. Aidha, kama kikao kinaanza leo, jana alikuwa na haraka ili kuwahi nini !!
 
Kama Unakumbuka Kikao Cha Madereva Wa Serikali Na Waziri Jafo Yote Yamezungumzwa
Ila Sasa....
Msafara ni tofuati na safari ya kawaida, aidha msafara huwa madereva wanaambiwa mwendo wa kwenda kama ni 120 madereva wote hukanyaga mafuta katika speed hiyo hiyo.
 
Viongozi wa kiswahili walio wengi hatakama wamesoma, hawako smart katika muda na kuheshimu ratiba, ndio maana kila siku wanasafiri kama wanafukuzwa na majambazi.
Kama ni msafara hana jinsi, unakuwa controlled na Security people, Kiongozi hana say, dereva akishaambia msafara utatembea 120km/h ndio utakanyaga wese kiasi hicho muda wote.
 
Kama ni msafara hana jinsi, unakuwa controlled na Security people, Kiongozi hana say, dereva akishaambia msafara utatembea 120km/h ndio utakanyaga wese kiasi hicho muda wote.
Speaker Hana Msafara
Isipokuwa Gari Mbili Security (Escort) Na Yake
 
Bro kama hujui kaa kimya, hakuna dereva anayeambiwa aende speed ngapi
Sinsiga, hupaswi kutumia nguvu kubisha hili, kama hujui unabishana na nani bora uache tu, nimekuwa Mkuu wa Misafara mara nyingi tu. Ninachosema nakijua, Escots na Riders hukubaliana na madereva mwendo wa kutembea, ndo maana unaona magari ya msafara hasa yale yenye viongozi na walinzi wao yanaachana kwa nafasi sawa.
 
Labda wewe ni mgeni katika hii nchi, hata kama kikao kipo siku 7 mbele mwendo wa viongozi wenye misafara nihiyohiyo..Bro hata jambo hili dogo unashindwa kulibaini?
Mkuu, mtu hawezi kufahamu kila kitu, kumbuka kila siku tunajifunza, kuna mambo tumesoma shule, mengine tunakutana nayo maishani, mengine ni maelekezo kutoka kwa Viongozi na mengine ni miongozo ya Kitaifa, ndo maana unaona watu wanasema Spika hana Msafara ilhali Katiba ya JMT inafafanua aina ya Misafara na idadi ya magari yatakayokuwepo.
 
Sinsiga, hupaswi kutumia nguvu kubisha hili, kama hujui unabishana na nani bora uache tu, nimekuwa Mkuu wa Misafara mara nyingi tu. Ninachosema nakijua, Escots na Riders hukubaliana na madereva mwendo wa kutembea, ndo maana unaona magari ya msafara hasa yale yenye viongozi na walinzi wao yanaachana kwa nafasi sawa.
Ni kweli sijui nabishana na nani, lakini kwa misafara ambayo hata mi nimeshiriki tena mingi sana, kama anayefuatwa ni yule kiongozi wa mbele kama ni Pikipiki ya Polisi au kama ni gari tu!! Anyway hizi protocol waendelee nazo maana sio za msingi sana kwa maisha yangu binafsi
 
Maneno kuntu kama hawajakuelewa wasituletee sababu zisizo na mashiko
Magari ya Viongozi wa Kawaida watamwelewa, lakini Msafara una taratibu zake hakuna mtu kutoka nje anaweza kutoa ushauri, kuna watu wamesmea Protocal na Ulinzi wa Viongozi na wanalipwa mishahara kwa kazi hiyo; na kwa taarifa yako ile misafara inakuwa controlled pia na watu wasiokuwa ndani ya huo msafara. Yaani Msafara wa Kiongozi utembee 50 km/h ilhali magari mengine yamesimamishwa.
 
Hii serikali ya kubana matumizi mbona inatapakanya fedha za walipa kodi sana?

Hivi kuna ulazima gani wa kuchoma mafuta na V8 Kilimo kwanza AC Dar mpaka Dodoma kupeleka box la Document? Hapo hapo Perdiem za Dereva na Boss anayepelekwa? Kwani Bombadier za nini,hakuna ndege zinazoenda dodoma mkasafirisha kama kifurushi?

Hivi kwanini wasitumie mkongo wao wa taifa kufanya video conferencing,yanini spika kukimbizana barabarani kuwahi mkutano kwani aliyeanzisha video conferencing alikuwa mpuuzi? watu wengi wanafanya meeting online tena sana tu maana meeting zinazofanyika hazina ulazima wa kuwa wote sehemu moja maana vitu wanavyodiscuss ni oral tu.
 
Mswahili anawahi mazishi tu
Lakini punctuality ni zero.
Huko kukimbia ni kukurupuka tu sio kwa maana ya usalama, mbona tunaona misafara Ulaya ikienda mwendo wa kawaida kwani wanajua ni mda gani watatumia wakiwa wanaongozwa na police kufungua njia.

Sasa wao hata saa haangalii mkanda anafunga nusu saa
Dereva kakaa tangu asubuhi kwenye gari maskini anamsubiria
 
Back
Top Bottom