Ushauri: Ununuaji wa magari

Mwenye uzoefu na gari aina ya Toyota Voltz, uzuri wake na usumbufu wake
Well,

Voltz ilitengenezwa kwa ubia kati ya General motors (GM) ya marekanj na Tpyota (japan)
Hivyo, iliundwa huko marekani na kuwa imported kwenda japan.

Design yake, ime base sana kwenye Toyota Corolla. Kilichowafanya watu wengi kuipenda voltz ni muundo wake wa kipekee haswa ndani

Pia ni gari ambayo, haikuuzwa kwa wingi, ndio maana unakuta hata kupishana nazo mtaani ni mara chache-chache sana.

UTUMIAJI WA MAFUTA

Manual inatumia 12.2km/L
Auto inatumia 11.2km/L

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina option ya kumnunulia wife gari kati ya Toyota Premio new model na Toyota Ractis, mwenye uzoefu wa hizi gari msaada tafadhali
 
Emmanuel S Jonathan,
Kwa Tanzania, spare parts za Honda, Hyundai, Mazda upatikaji wake ni mgumu na hata ukizipata gharama yake ni kubwa. Nachokipenda ni kuwa spare zake bado mchina hajatia mkono wake,hivyo ukizipata na kuziweka ktk gari yako zinadumu kwa muda mrefu sana.
Honda accord zipo za aina tatu tofauti
1. Honda Accord
2. Honda Coup
3. Honda Wagon.

Mfano ukitaka kuagiza 2003 HONDA ACCORD toka Japan.

1552644770309.png


Transmiss ni automatic
Engine Size yake ni 2,350cc
Jumla ya seats ni 5
Milango ni 4
Mafuta ni Petrol

Kama utainunua toka Japan, gharama ya chini kabisa ya kuinunua 2003 HONDA ACCORD ni CIF= $2,475 (zipo zenye bei Zaidi ya hapo,nimekupa bei ya chini kabisaaaaa).
Llakini ukumbuke pia kuwa inabidi utoe gharama ya I=insurance ambayo kwa sasa na kwa sheria mpya inatakiwa kulipiwa Tanzania.

Kwa maana hiyo basi bila "I" bei itakuwa ni C&F=$2,399 hapo ni mpaka inafika bandarini.
Kwa ninavyoona kuhusu Engine size (2,350cc) yake,sio mbaya sana ktk Matumuzi ya mafuta,lakini ni lazima ujipange.
Ni nzuri kwa safari ndefu haichoshi.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom