Zion Daughter
JF-Expert Member
- Jul 9, 2009
- 8,921
- 4,235
Habari zenu ndugu wapendwa wana MMU wote,
Kwa heshima na taadhima naomba kuwashirikisha mambo yangu wawili yanayohusiana na mahusiano kwa ushauri zaidi na majadiliano,
Case no 1..
Kuna kijana anadai ananipenda lakn nimemkatalia kwa sababu haiwezekani kuwa nae (we are not compatible at all at all)..Age much older than him na mambo mengine.Lakini reaction yake ni kuwa yeye kama akifa saa yoyote basi mimi ndio chanzo na kama wakipeleleza watajua mimi ndio chanzo..Nilikuwa nachukulia utani lakn sasa naona huu wimbo wa kufa unazidi..sijaelewa kama anatania tu au yupo serious lakn ninavyomuona akili zake dakika mbili mbele...Asije akafanya kweli afu nikawa sababu... Nishaurini ni handle vipi hii issue.
Case no 2.
Kuna babu mtu mzima above 60 ananing'ang'ania niwe kwenye familia yake kama mke/mkwe.. Ilianza wakati naanza kazi na nikamkuta hapo ofisini.Alikuwa anaonyesha dalili za ku care lakn sikumpa nafasi ya kuropoka... Baadae sijui alikata tamaa au vipi akaoa yani akafunga ndoa na mke aliyekuwa anaishi nae.Baada ya hilo akaja baba mwingine wa hapo ofisini na kunieleza jinsi huyo babu alivyokuwa anajigamba kuwa ni lazima anioe na alinifanyia hata dawa(kwa mganga) iliyoshindikana anyway.Nilimuita na kumuuliza habari hizo mbele ya mleta habari na hakukana/alikubali..Juzi kati kaibuka tena akidai kuwa ni mpango wa Mungu niwe naye...Ndipo nilimuuliza kama ana mpango mke wake afe ndio anioe(ndoa ni mpaka kifo kitenganishe).Alishtuka kwa maneno hayo na akageuza kibao na kusema kuwa kama yeye imeshindikana basi ni LAZIMA mtoto wake anioe.Akaongeza kuwa nitake nisitake lazima niingie kwenye familia yake..Sijamuelewa huyu mzee ana nini na mimi? na anaringia nini.Ninavyomuona ni kama hatanii na anachoongea. Naombeni ushauri na maombi ikiwezekana ili aniwache nipumue...
Kwa heshima na taadhima naomba kuwashirikisha mambo yangu wawili yanayohusiana na mahusiano kwa ushauri zaidi na majadiliano,
Case no 1..
Kuna kijana anadai ananipenda lakn nimemkatalia kwa sababu haiwezekani kuwa nae (we are not compatible at all at all)..Age much older than him na mambo mengine.Lakini reaction yake ni kuwa yeye kama akifa saa yoyote basi mimi ndio chanzo na kama wakipeleleza watajua mimi ndio chanzo..Nilikuwa nachukulia utani lakn sasa naona huu wimbo wa kufa unazidi..sijaelewa kama anatania tu au yupo serious lakn ninavyomuona akili zake dakika mbili mbele...Asije akafanya kweli afu nikawa sababu... Nishaurini ni handle vipi hii issue.
Case no 2.
Kuna babu mtu mzima above 60 ananing'ang'ania niwe kwenye familia yake kama mke/mkwe.. Ilianza wakati naanza kazi na nikamkuta hapo ofisini.Alikuwa anaonyesha dalili za ku care lakn sikumpa nafasi ya kuropoka... Baadae sijui alikata tamaa au vipi akaoa yani akafunga ndoa na mke aliyekuwa anaishi nae.Baada ya hilo akaja baba mwingine wa hapo ofisini na kunieleza jinsi huyo babu alivyokuwa anajigamba kuwa ni lazima anioe na alinifanyia hata dawa(kwa mganga) iliyoshindikana anyway.Nilimuita na kumuuliza habari hizo mbele ya mleta habari na hakukana/alikubali..Juzi kati kaibuka tena akidai kuwa ni mpango wa Mungu niwe naye...Ndipo nilimuuliza kama ana mpango mke wake afe ndio anioe(ndoa ni mpaka kifo kitenganishe).Alishtuka kwa maneno hayo na akageuza kibao na kusema kuwa kama yeye imeshindikana basi ni LAZIMA mtoto wake anioe.Akaongeza kuwa nitake nisitake lazima niingie kwenye familia yake..Sijamuelewa huyu mzee ana nini na mimi? na anaringia nini.Ninavyomuona ni kama hatanii na anachoongea. Naombeni ushauri na maombi ikiwezekana ili aniwache nipumue...