Ushauri unahitajika: Familia tumekwama

Minafikiri tatizo ni nyie familia ya kaka yako, pamoja na huyo mama wa hawarayake kaka yako.

Kwa haukika nyie ndio shida, that's why hili Jambo limekua kubwa kwasababu mnakizungumzia sana na ndio sababu issue ya kakaenu imekua na attention kubwa.

Ebu muacheni kaka yenu na mkewe waamue nini hatma ya maisha na mahusiano yao.

Alafu kakaenu nae ni fala sana, yaani inakuaje aruhusu ndugu zake na mkwe wake aingilie maisha yake..??
 
Yaani bro wako alishindwa kumuhudumia huyo Dada kimya kimya Hadi issue ikajulikana na wife wake!!?.

Kwa ushauri wangu aendelee kumuhudumia huyo Dada kwa Siri pasipo mkewe kujua. Akishajifungua waende kupima DNA kuthibitisha Kama mtoto ni wake kweli.
Skuiz braza apa kwetu DNA n tunapgwa we chukua hata mtoto wa jiran yako ukapme uone majbu uspoletewa mtoto n wako na hil wameamua kulfanya il kuondoa tatzo la watoto kutelekezwa na watoto wa mitaan ndio mana ikienda complain ya kuhus mtoto mkemia anacheza na saikolojia zenu aliekua anahudumia mtoto ndio anashnda iyo turufu labda uende kenya ndiohawana interest na hata ao watoto wa mtaan wa nnch yenu wala ndoa kuharbka za nnchn kwenu unapewa majbu black and whte
 
Tatizo nini sasa hapo? Mwambie akapige tena peku nje aone matokeo yapoje.
 
Mkuu hapo inabidi mfanye kikao cha siri na kaka yako! Kwamba aendelee kumhudumia mjamzito kwa siri, lakini mtoto akizaliwa wakapime vinasaba vya dna!

Ikijabainika mtoto sio wake, basi afanye kama ametoa sadaka! Pia ikibainika mtoto ni wa kwake basi huyo bimkubwa apandishwe cheo, na akikataa na apishe kiti!

Imeshatokea watu wanaenda hospitali na kupewa maelezo ya kitaalamu, kuwa huna tatizo flani lakin akienda upande wa pili analikuta tatizo !
Mnaweza kuwa mmeshikia bango kuwa kaka ndiye mwenye tatizo kumbe tatizo kumbe tatizo lipo kwa bimdada!
 
Umesema kaka yako hana mbegu kwenye manii yake na hospital wameprove hivyo,sasa hii nyumba ndogo inawapelekesha kwa nini?,hata kama kusoma hujui huoni hii picha iko upsdown?
 
Heshima kwenu wakuu. Usipite bila kushauri.

Kuna issue ya kimahusiano inaleta utata kwenye familia.

Tuna kaka yetu mkubwa ameo mwaka wa Saba sasa na hawajabahatika na mkewe kupata mtoto. Familia imewahi wasidia sana kujua nini chanzo cha tatizo mara kadhaa na taarifa rasmi za kitabibu tunayoijua kama familia ndugu yetu ana tatizo la kutokua na mbegu za kiume yaani azoospermia . Hali hii aina uhusiano na kufanya mapenzi na kulizishana bali ni kwamba mwanaume anakua hana mbegu za kiume kwenye manii yake.

Sasa hivi karibuni imeripotiwa case kuwa amempa mdada ujauzito. Brother amekili kuwa amewahi kutembea bila kinga na huyo dada ila hana uhakika kama dada alikua hana jamaa mwingine. Dada huyo amekua akifuatwa na family member akiulizwa kuwa ujauzito ni wa nani ili kuhepusha mgogoro unaoendelea kwenye familia. Mara zote dada amekua akisema hakua na mtu mwingine kipindi icho wanakutana, na ana uhakika kuwa ujauzito ni wa brother.

Mwanzoni brother inaonekana alikua anampa msaada wa kujikimu dada huyo ila baada ya tafaruku kubwa linaloendelea home kasitisha saport ,kwani mkewe amedai yuko tayari kuachika kama kaka etu ataendelea kuwasiliana na huyo dada na kumsaidia. Fujo na kelele kila siku home aziishi na kuitwa familia kutatua mgogoro.

Dada huyo aliyepewa ujauzito alikua amepanga na anafanya shughuri zake ndogo ndogo . Ila ujauzito umekua ukimsumbua ,kutapika kama kote na kila week hospitali, hali iliopelekea kushindwa kujihudumia na amerudi kwa wazazi wake.

Mama wa huyo dada kaleta mashitaka home akitaka kaka yetu aendelee kumsapot huyo dada hadi atakapojifungu ili watatue mgogoro kwa kipimo cha DNA.

Wife wa brother kusikia pendekezo hilo kagoma katu katu kuwa ana uhakika mmewe anabambikiwa mimba na kuwa dada huyo anataka mtu wa kumlelea ujauzito. Kifupi ahamini mmewe kamtungisha mimba dada huyo.

Juzi tu wamerudi hospitali na bado jibu ni lile lile kua kaka hana mbegu za kiume.

Sasa wakuu katika mkasa kama huu

Busara ni nini ?

Kuikana mimba hadi mtoto azaliwe huku unajua kuwa yule dada anateseka na familia yake imekomaa hawana uwezo wa kumtunza mtoto wao ?

Au kaka amsapoti mdada huyo hadi ujauzito ukamilike na kipimo cha DNA kifanyike.

Familia imekwama nini kifanyike kwani vikao haviishi home kila siku

Wakuu ushauri wenu ni upi kwenye kisa kama hiki?
Kama wewe binafsi umeguswa na plight ya huyo "mdada", kamsaidie tu kwa nafsi yako, utapata thawabu kwa Mungu. Vinginevyo mwacheni kaka yenu awe na amani na mkewe. Shemeji yenu amejitoa kisadaka kuendelea kuishi na mume mwenye hiyo uliyosema "azoospermia", bado mnamletea presha za michepuko? Muwe na huruma.
 
Sasa broo kama hana uwezo wa kupachika mimba na kuambiwa hospitali mnachobishana ni nini
Hospitali sio Mungu ndugu,Sara aliyekuwa tasa alimpata Isaka akiwa na miaka 90. Mungu anatenda jambo ambalo mwanadamu analiona haliwezekani. Ushauri wangu kaka aendelee kuihudumia mimba kwa kificho mpaka mtoto azaliwe na baada ya hapo waende kufanya DNA test.
 
Heshima kwenu wakuu. Usipite bila kushauri.

Kuna issue ya kimahusiano inaleta utata kwenye familia.

Tuna kaka yetu mkubwa ameo mwaka wa Saba sasa na hawajabahatika na mkewe kupata mtoto. Familia imewahi wasidia sana kujua nini chanzo cha tatizo mara kadhaa na taarifa rasmi za kitabibu tunayoijua kama familia ndugu yetu ana tatizo la kutokua na mbegu za kiume yaani azoospermia . Hali hii aina uhusiano na kufanya mapenzi na kulizishana bali ni kwamba mwanaume anakua hana mbegu za kiume kwenye manii yake.

Sasa hivi karibuni imeripotiwa case kuwa amempa mdada ujauzito. Brother amekili kuwa amewahi kutembea bila kinga na huyo dada ila hana uhakika kama dada alikua hana jamaa mwingine. Dada huyo amekua akifuatwa na family member akiulizwa kuwa ujauzito ni wa nani ili kuhepusha mgogoro unaoendelea kwenye familia. Mara zote dada amekua akisema hakua na mtu mwingine kipindi icho wanakutana, na ana uhakika kuwa ujauzito ni wa brother.

Mwanzoni brother inaonekana alikua anampa msaada wa kujikimu dada huyo ila baada ya tafaruku kubwa linaloendelea home kasitisha saport ,kwani mkewe amedai yuko tayari kuachika kama kaka etu ataendelea kuwasiliana na huyo dada na kumsaidia. Fujo na kelele kila siku home aziishi na kuitwa familia kutatua mgogoro.

Dada huyo aliyepewa ujauzito alikua amepanga na anafanya shughuri zake ndogo ndogo . Ila ujauzito umekua ukimsumbua ,kutapika kama kote na kila week hospitali, hali iliopelekea kushindwa kujihudumia na amerudi kwa wazazi wake.

Mama wa huyo dada kaleta mashitaka home akitaka kaka yetu aendelee kumsapot huyo dada hadi atakapojifungu ili watatue mgogoro kwa kipimo cha DNA.

Wife wa brother kusikia pendekezo hilo kagoma katu katu kuwa ana uhakika mmewe anabambikiwa mimba na kuwa dada huyo anataka mtu wa kumlelea ujauzito. Kifupi ahamini mmewe kamtungisha mimba dada huyo.

Juzi tu wamerudi hospitali na bado jibu ni lile lile kua kaka hana mbegu za kiume.

Sasa wakuu katika mkasa kama huu

Busara ni nini ?

Kuikana mimba hadi mtoto azaliwe huku unajua kuwa yule dada anateseka na familia yake imekomaa hawana uwezo wa kumtunza mtoto wao ?

Au kaka amsapoti mdada huyo hadi ujauzito ukamilike na kipimo cha DNA kifanyike.

Familia imekwama nini kifanyike kwani vikao haviishi home kila siku

Wakuu ushauri wenu ni upi kwenye kisa kama hiki?
Bunduki ambayo haina risasi inawezaje kuua?kaka yenu anauziwa mbuzi kwenye gunia
 
Sasa wanabishania nini? ushauri wa bure ni kwamba ajaribu tena mchepuko mwingine ili ajue kama mbegu zake zina maruhani ya kuzalisha au la....halafu kama mimba ikitunga apige kimya mpaka mtoto azaliwe then akampime DNA kama ni mtoto wa kwake amfahamishe mkewe ili achague akae au arudi kwao
 
Back
Top Bottom