TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 23,913
- 23,075
Bashe ahimiza vijana kujitokeza kuwania uongozi uchaguzi CCM
Imeandikwa na Halima Mlacha, Nzega; Tarehe: 3rd October 2011 @ 15:30.
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Hussein Bashe amewataka vijana wa chama hicho kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi wa chama hicho utakaofanyika mwakani.
Aliyasema hayo mjini Nzega alipozungumza na vijana wa Kata ya Mwakashanhala na vitongoji vyake ambapo aliwataka kushiriki kwenye ujenzi wa CCM bora itakayokwenda na wakati zaidi.
Aliwaomba vijana hao mwakani katika uchaguzi huo wajitokeze na kugombea nafasi hizo.
"Sisemi muwaondoe kabisa wazee wetu, lakini gombeeni jamani msiogope hizi nafasi kwenye
matawi kule gombeeni ili mwaka 2012 tujenge chama ambacho kitakua na vijana wengi," alisema Bashe.
Alisema bila vijana kujitolea, wataendelea kuwa wapigadebe wakati wanaokaa ndani kufanya
maamuzi ni wengine wasiozifahamu shida wala matatizo ya vijana...........................................................
Source:HabariLeo | Bashe ahimiza vijana kujitokeza kuwania uongozi uchaguzi CCM
USHAURI:
Kwa mvurugano huu wa vijana(UVCCM) na upinzani wa wazi wazi baina ya viongozi na makada wa CCM katika baadhi ya mambo ndani ya chama na serikali, ningependa kumshauri m/kiti wa CCM. Mimi ninamshauri Mwenyekiti wa CCM afuate taratibu za chama kuhairisha uchaguzi wa CCM 2012 kwa mwaka mmoja, ili kwanza kupunguza migongano hii,lengo likiwa wanachama waingie kwenye uchaguzi wakiwa kwa kiwango fulani wamoja. Endapo uchaguzi huu utafanyika katika hali hii ya "misuguano hii mikali" baina ya wanachama, huku baadhi ya viongozi wakipuuza kutatua matatizo halisi yanayokigharimu chama na kudandia matatizo ya ''kupikwa" ambayo yanazidi kukisambaratisha chama, basi Uchaguzi huo utasababisha hali ya mbaya zaidi si kwa chama pekee hata kwa serikali yenyewe.
Imeandikwa na Halima Mlacha, Nzega; Tarehe: 3rd October 2011 @ 15:30.
MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Hussein Bashe amewataka vijana wa chama hicho kujitokeza kwa wingi kwenye uchaguzi wa chama hicho utakaofanyika mwakani.
Aliyasema hayo mjini Nzega alipozungumza na vijana wa Kata ya Mwakashanhala na vitongoji vyake ambapo aliwataka kushiriki kwenye ujenzi wa CCM bora itakayokwenda na wakati zaidi.
Aliwaomba vijana hao mwakani katika uchaguzi huo wajitokeze na kugombea nafasi hizo.
"Sisemi muwaondoe kabisa wazee wetu, lakini gombeeni jamani msiogope hizi nafasi kwenye
matawi kule gombeeni ili mwaka 2012 tujenge chama ambacho kitakua na vijana wengi," alisema Bashe.
Alisema bila vijana kujitolea, wataendelea kuwa wapigadebe wakati wanaokaa ndani kufanya
maamuzi ni wengine wasiozifahamu shida wala matatizo ya vijana...........................................................
Source:HabariLeo | Bashe ahimiza vijana kujitokeza kuwania uongozi uchaguzi CCM
USHAURI:
Kwa mvurugano huu wa vijana(UVCCM) na upinzani wa wazi wazi baina ya viongozi na makada wa CCM katika baadhi ya mambo ndani ya chama na serikali, ningependa kumshauri m/kiti wa CCM. Mimi ninamshauri Mwenyekiti wa CCM afuate taratibu za chama kuhairisha uchaguzi wa CCM 2012 kwa mwaka mmoja, ili kwanza kupunguza migongano hii,lengo likiwa wanachama waingie kwenye uchaguzi wakiwa kwa kiwango fulani wamoja. Endapo uchaguzi huu utafanyika katika hali hii ya "misuguano hii mikali" baina ya wanachama, huku baadhi ya viongozi wakipuuza kutatua matatizo halisi yanayokigharimu chama na kudandia matatizo ya ''kupikwa" ambayo yanazidi kukisambaratisha chama, basi Uchaguzi huo utasababisha hali ya mbaya zaidi si kwa chama pekee hata kwa serikali yenyewe.