Ushauri: Shirikisho la Muziki mchagueni Carola Kinasha kuwa msemaji

superwarkills

Senior Member
Aug 18, 2014
136
83
Carola Daniel A. Kinasha ni mwanamuziki wa Tanzania anayefanya muziki wa Asili na akichanganya na usasa, Mwanamama Carola alizaliwa miaka ya 60 katika kijiji cha Longido.

Alianza kujishughulisha na muziki mnamo miaka ya 80 rasmi ikiwa ni mwaka 1988, akijifunza zaidi kupiga gitaa.

Carola Kinasha ni mwanamuziki ambaye anaamini kuwa ili tasnia ya sanaa ya Tanzania iweze kukua na kujulikana kimataifa ni muhimu kurejesha elimu ya sanaa kwenye shule zetu. Pia kuwa na sehemu za kufanyia shughuli za sanaa kwenye kila kitongoji,."anasema

Amekuwa mwalimu wa muziki na muimbaji wa matamasha ya kimataifa, akiwa pia ni mshiriki wa tunzo mbalimbali ikimo tunzo za MA AFRICA AWARD South Africa mwaka 2002, Carola Kinasha licha ya kuimba pia ni MC wa matamasha mbalimbali likiwemo Tamasha la Sauti za Busara na amekuwa akishiriki washa na makongomano mbali ya muziki yakiwemo yale ya kujadili haki za wanamuziki.

Mwanamama huyu ambaye kabila lake ni mmasai alipata elimu yake ya juu katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, akichukua taaluma ya sanaa na mahusiano ya kimataifa (Bachelor of Arts Degree in International Relations) alifanikiwa kuanzisha bendi yake mwishoni mwa miaka 1980 iliyofahamika kama Kinasha's Shada Band ikiwa na lengo la kutengeneza muziki wa halisi wa Tanzania, amewai kushiriki pia katika wimbo wa mjomba (Mrisho Mpoto)

Carola ana album ya Maono ambayo ni ya pili (2007) kabla ya album ya kwanza ya (UMOJA) iliyotoka mwaka 1997. Corola Kinasha pia ameshiriki filamu mbalimbali ikiwemo Documentary yake iliyotoka 2009 inayofahamika kama "Mwamba ngoma"

Carola Kinasha pia ni mratibu na msimamizi wa tamasha la Music Mayday linalofanyika kila mwaka.

Nadhani huyu kwa maoni yangu ndiye anafaa kuwa msemaji wa shirikisho la muziki, kwa kuwa anaujua muziki, anauishi, na anaufanya muziki.

Shirikisho mchagueni Carola Kinasha.

View attachment 2161201View attachment 2161202View attachment 2161203
 
Matokeo kachaguliwa anayeiga sauti ya Mwalimu Nyerere na hana ujuzi wala elimu yoyote zaidi ya kuwa kuwadi wa kuwakuwadia warembo wa tasnia ya filamu kwa wazee wa mujini, hata muziki hajui ni kitu gani, na huku ndiko Watanzania tulipofikia, usishangae kesho huyu mhuni anakuwa mbunge au DC, kisa anaupiga mwingi na ni mpambe.AIBU SANA hii sasa wenye muziki wanalalamika nae anaaza kuporomosha matusi,huyu hana tofauti nalile jimama lilisema eti yeye anazaa wengine wanakunya, kisa kitoto chake kimemnunulia gari ilihali hata hilo gari hajui kalinunua kwa pesa yake au kahongwa.
 
Wewe unataka mtu serious kwenye mzaha?

Unafikiri hiko cheo ni kitu serious?

Huyo mtu wako anajua kutafuta kick na kupata followers Instagram?

Nchi kama Nigeria kuna msemaji wa wanamuziki? Mbona Diamond kafika alipofika bila shirikisho wala msemaji?

Acha mizaha ya Instagram iendelee
 
Wewe unataka mtu serious kwenye mzaha?

Unafikiri hiko cheo ni kitu serious?

Huyo mtu wako anajua kutafuta kick na kupata followers Instagram?..

Nchi kama Nigeria kuna msemaji wa wanamuziki?..mbona Diamond kafika alipofika bila shirikisho wala msemaji?..

Acha mizaha ya Instagram iendelee
Sijui kwanini kijamaa kimeng'ang'ania
 
Mimi pia nasimama na Steve, Dalali kama dalali.

Kwa msaada wa pasi zake za mwisho nimeshamaliza almost Bongo Movies wote, sasa nataka pasi zake ziendelee hata kule kwenye Bongo Fleva.
 
Msemaji wa wanamuziki anakuwa anasema nini ukiwa Ally Kiba ana msemaji wake, Diamond ana msemaji wake nk?

Vyeo vya kijinga vya watu wa instagykuzolea mademu na followers tu hakina kitu.

Msiwaingize watu Kama Kinasha, Innocent Nganyagwa nk ambao wapo serious kwenye mambo ya kitoto .

Shirikisho lenyewe limeanzishwa kimchongo tu wanamuziki wahusika hawajui kuna kitu kama hicho hapo unaona kabisa ni upuuzi tu.

Kwanza msemaji hana maamuzi yeyote zaidi ya kuangalia watu serious ndio wawe viongozi wa shirikisho hapo ndio itakuwa inaeleweka Ila usemaji hauna chochote hata wakimuweka kingwendu sio ishu hapo wapambane kuweka CEO mwenye shule nzuri, exposure na utaalamu wa muziki.

Otherwise it's wastage of time heri hao uliowataja waendelee na mambo yao tu.
 
Bongo viongozi wako useless, utakuja kushangaa mwisho wa siku wanamuweka Wema Sepetu kuwa msemaji wao bila ridhaa ya wanamuziki. Yaani tuna viongozi very useless sana hapa nchini.
 
Back
Top Bottom