USHAURI: Shirika la reli uzeni mali zote ambazo hazitumiki mathalani Vyuma chakavu

The lost

JF-Expert Member
Jul 3, 2017
2,695
8,209
Nimepita maeneo mbalimbali nimejionea namna shirika la reli limekuwa likitunza mavyuma chakavu kama mabehewa mataruma na makaravati ambayo yamechakaa.

Hivyo nashauri mali hizo ziuzwe kama malighafi kwa viwanda vyetu vya ndani vya kutengeneza material ya chuma (steal industry) ili tuweze kupata bidhaa mpya. Faida ya kufanya hivi.
  • Shirika litapata pesa za kuendeshea mambo yake.
  • Tutakuwa tunatunda mazingira yetu kwa kuruhusu uoto wa asili kumea katika maeneo vilipo vyuma hivyo.
  • Tutatoa ajira kwa watanzania.
  • Tutaongeza uzalishaji wa bidhaa mfano nondo, majenge etc
 
Sikio la kufa halisikii dawa,hata wauze vyuma bado hakutakuwa na la maana.
 
Back
Top Bottom