USHAURI: Serikali iyanunue yale Makontena kwa Bei ya ACACIA ikayauze kwa Bei ya Prof. Mruma

Wadau,

Wote tunafahamu kua kwa sasa kuna mvutano kati ya Serikali (Kamati ya Prof. Mruma) v/s ACACIA ambao ndio wenye makontena 271 yaliyoshikiliwa Mandarini. Kamati ya Prof. Mruma wanasema kua thamani ya madini yaliyoko kwenye kontena moja kwa wastani yana thamani ya zaidi ya Tshs 3Bil wakati Kampni ya ACACIA kupitia kwa Mtendaji wake mkuu wanasema kua kila kontena moja lina thamani ya wastani wa Tshs 300Million tu.

Mi ushauri wangu kwa serikali ni kua iilazimishe kampuni ya ACAIA iwauzie wao serikali kwa bei hiyo ambayo ACACIA wanadai yaani Tshs 300Mil kisha yenyewe ikayauze au ikayasafishe kwa hiyo bei inayodhani kua ndio thamani halisi.

Hapo ina maana serikali itakua imejipatia faida kutokana na haya makontena au dhahabu, lakin pia itakua imejua ukweli yenyewe kua ni kiasi gani hua hawa wenye makampuni ya kuchimba dhahabu wanapataga kutokana na huu mchanga. Nina uhakika serikali haitokosa Tshs 300mil x 271 = Tshs 81.3Billion kulipia haya Makontena,


Ushauri wangu ni huu
 
Back
Top Bottom