Ushauri; Serikali iboreshe OPRAS kwa watumishi wa umma

stigajemwa

JF-Expert Member
Nov 12, 2016
449
430
Opras ni mfumo unaozingatia uwezo wa utendaji wa mtumishi kulingana na malengo aliyowekewa na mwajiri wake.

Hivyo ili kuamini kuwa nchi ina wafanyakazi wenye weledi,uwezo na uzalendo ilibidi serikali iboreshe mfumo wa obras badala ya kuamini katika vyeti.

Ninachokiona kwa sasa ni serikali kuamini katika vyeti kama kipimo cha utendaji kazi kwa watumishi.Dhana hii ni potofu kwani katika nchi zilizoendelea wamefikia hatua ya kuwatunuku shahada ya kwanza ya heshima baadhi ya watu waliofanya vizuri katika nyanja fulani.

Mfano: Kiugunduzi,kiutafiti, katika ujasiliamali yaani wameajiri watu wengi hivyo kuwa msaada kwa taifa.Watu hawa muhimu hutunukiwa shahada ya heshima hata kama hawakupitia elimu ya sekondari.

Hivyo ni vyema waboreshe opras ili tuweze kumwamini mtumishi kupitia utendaji wake kuliko sasa ambapo cheti ndio kinachotukuzwa japo utendaji ni ziro.

Ikiwezekana serikali ibadili mfumo wa upimaji wa uwezo wa mwanafunzi ktk mitihani ili iwe katika level zote wanafunzi wafanye mitihani ya nadharia kwa 50% na vitendo 50% ili tuepukane na kuwa na wahandisi, na Phd holders wenye vyeti lakini kichwani ziro.
 
Opras ni mfumo unaozingatia uwezo wa utendaji wa mtumishi kulingana na malengo aliyowekewa na mwajiri wake
Hivyo ili kuamini kuwa nchi ina wafanyakazi wenye weledi,uwezo na uzalendo ilibidi serikali iboreshe mfumo wa obras badala ya kuamini katika vyeti
Ninachokiona kwa sasa ni serikali kuamini katika vyeti kama kipimo cha utendaji kazi kwa watumishi.Dhana hii ni potofu kwani katika nchi zilizoendelea wamefikia hatua ya kuwatunuku shahada ya kwanza ya heshima baadhi ya watu waliofanya vizuri katika nyanja fulani:mfano, kiugunduzi,kiutafiti, katika ujasiliamali yaani wameajiri watu wengi hivyo kuwa msaada kwa taifa.Watu hawa muhimu hutunukiwa shahada ya heshima hata kama hawakupitia elimu ya sekondari

Hivyo ni vyema waboreshe opras ili tuweze kumwamini mtumishi kupitia utendaji wake kuliko sasa ambapo cheti ndio kinachotukuzwa japo utendaji ni ziro
Ikiwezekana serikali ibadili mfumo wa upimaji wa uwezo wa mwanafunzi ktk mitihani ili iwe katika level zote wanafunzi wafanye mitihani ya nadharia kwa 50% na vitendo 50% ili tuepukane na kuwa na wahandisi, na Phd holders wenye vyeti lakini kichwani ziro

Acha mambo yako wewe, unafanya kazi kwenye utumishi wa umma? Performance appraisal kwa public Services in Tanzania is impossible and it's just another grave of the people's rights. Unapata 40% ya budget how can you really achieve the organizational objectives?

In private sector that's very okay...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom