ushauri please: mama yake demu wangu ameniita nikaweke mambo wazi,kastukia nipo na mwanae

Wild fauna

JF-Expert Member
Apr 22, 2012
461
189
salamu wana jf, nilitokea kumpenda binti mmoja na ninaendelea nae mpaka sasa. Jana mama yake alinipigia simu akanimbia amekua kwenye uchunguz akagundua nina uhusiano na mwanae,pia mwanae amekiri kuwa mie ni mtu wake. Mama huyo kaniambia namweka katika wasiwasi mkubwa kuhusu mwananae. Ananiambia nije nyumbani niweke wazi mbele yake(mama na baba mzazi). Wadau mi nampenda huyo binti yao, je niende kuweka mambo waz? Je nitaenda kueleza nin? Ushauri tafadhali,
 
Nenda tu ukakabidhiwe mali yako unaogopa nini? usiende peke yako lakini mchukuwe na rafiki yako usije ukaambulia ngumi bure!
 
Je ww uko tayari,na km mama mkwe asingekwambia uende ungeenda?ukienda ni ishara kua hata kwenye ndoa yako huyo maza ndie atakua anaamua,kua mwanaume bwana,vijana wa ck hz mbona mnaiangusha sana hii jinsia adim ya kiume?!yan maza mkwe ndio akwambie,akuamulie uende?!
 
Kama anamiliki bastola vaa bullet proof ndo uende,kama wana mshale kunywa kabisa dawa ya kuzuia mshale usiingie ndo uende
Na kama baba yake anakula tigo jiandae uinunulie Bundle ya kabaang
 
salamu wana jf, nilitokea kumpenda binti mmoja na ninaendelea nae mpaka sasa. Jana mama yake alinipigia simu akanimbia amekua kwenye uchunguz akagundua nina uhusiano na mwanae,pia mwanae amekiri kuwa mie ni mtu wake. Mama huyo kaniambia namweka katika wasiwasi mkubwa kuhusu mwananae. Ananiambia nije nyumbani niweke wazi mbele yake(mama na baba mzazi). Wadau mi nampenda huyo binti yao, je niende kuweka mambo waz? Je nitaenda kueleza nin? Ushauri tafadhali,

Umesema ulipigiwa simu ukaweke wazi inamaana hajakwambia kitu gani?
Ila wanataka tu ukatangaze uchumba hakuna lingine.
 
Hadi hapo bado sijaelewa unasita nini wkt unadai unampenda huyo binti. Au upande mwingine labda bado hujamaliza starehe za ujana za kujit n run... Au wengine mnadai "demu wa kuzugia"... Km hujamaliza mambo yako ni bora ukawa muwazi usije mpotezea dada wa watu muda wake, na km upo tayari kuchukua "wholesale" ( jumla) basi funguka huko ukweni tujage kula ubwabwa sie....
salamu wana jf, nilitokea kumpenda binti mmoja na ninaendelea nae mpaka sasa. Jana mama yake alinipigia simu akanimbia amekua kwenye uchunguz akagundua nina uhusiano na mwanae,pia mwanae amekiri kuwa mie ni mtu wake. Mama huyo kaniambia namweka katika wasiwasi mkubwa kuhusu mwananae. Ananiambia nije nyumbani niweke wazi mbele yake(mama na baba mzazi). Wadau mi nampenda huyo binti yao, je niende kuweka mambo waz? Je nitaenda kueleza nin? Ushauri tafadhali,
 
Ila mama kakosa busara kabisa. Sasa yeye kukupigia simu wewe na kukutaka uende ueleze mahusiano yako na binti yake sio taratibu za kiungwana. Mama alitakiwa kumwambia mwanae akushawishi uende home kwao na sio yeye kukupigia simu direct. Sasa kiusalama inatia mashaka unaweza lishwa unga wa ndele ukapotelea hukohuko. Mama anajifanya yeye ni bongo fleva. Kama vipi asubiri posa tu.
 
Huyo binti asingekuwa moyoni mwako wala usingepata muda wa kukaa nakuelezea huku Jf... Usimuogope mama mkwe chukulia ni kama mama yako mzazi,kikubwa atachotaka kujua ni mustakabali wa mahusiano yenu... Nenda tu,itakupa heshima pia kwa kuitikia wito wao. Wakikuambia habari ya kuoa na hauko tayar waeleze tu. Ila usiache kwenda!
 
Mi nikuulize huyo binti amemaliza shule? usije ukawa unatembea na mwanafunzi,na hao wazazi wanaona uchungu wa karo zao.Maana unampotezea muda wa masomo yaani unamtengenezea division 5.
Kama ni mwanafunzi,usiende na uache kabisa mchezo huo vinginevyo utachezea jera.
kama ni binti aliyekwishamaliza shule nenda mkubaliane wakupe mke.
 
Back
Top Bottom