Niambie Tu
Senior Member
- May 29, 2022
- 162
- 272
Habari
Mimi ni kijana mwenye miaka 27 mhitimu wa chuo, nimebahatika kufanya kazi sehemu mbalimbali na pia nimewahi kufanya biashara tofauti tofauti, japo sijawahi kukaa kwa muda mrefu katika biashara.
Nimekuja hapa JF naombeni mawazo yenu.
Iko hivi, Kuna binti nilimpa ujauzito sikuona budi kumuacha wakati mimi niliyesababisha hivyo, nikaamua kuanza kuishi naye na kupeleka posa ukweni mahari itatolewa mbele. Kwa sasa nafanya kazi katika shirika moja ambapo mkataba wangu unaenda kuishia.
Napata changamoto kadhaa ambazo zimenifanya nije humu ndani, sijanikiwa kufanya akiba yoyote hadi sasa. Napata lawama nyingi sana kutoka kwa ndugu, kwa maelezo yao binafsi nimewahi kuishi na mwanamke.
Huyu binti nilimfungulia duka-denge na ndiyo analofanya hadi leo, japo halikui, muda mwingi naona hela natoa mfukoni mwangu.
Hivyo naombeni ushauri wana JF maana naona kwenda kuumbuka. Kiumbe kinapokuja pasipo na maandalizi ya kimaisha, uwezo wa yeye kwenda kujifungua hiyo hela ninayo, mimi ninachoumiza kichwa nitawezaje kuishi na mwanamke na familia ilihali sina kazi kwa sasa.
Kuna muda namchukia na kumuongelea vibaya hadi najisikia vibaya. Nilikuwa nasali ila nimeacha. Nayaogopa maisha ya mbele yangu.
Mimi ni kijana mwenye miaka 27 mhitimu wa chuo, nimebahatika kufanya kazi sehemu mbalimbali na pia nimewahi kufanya biashara tofauti tofauti, japo sijawahi kukaa kwa muda mrefu katika biashara.
Nimekuja hapa JF naombeni mawazo yenu.
Iko hivi, Kuna binti nilimpa ujauzito sikuona budi kumuacha wakati mimi niliyesababisha hivyo, nikaamua kuanza kuishi naye na kupeleka posa ukweni mahari itatolewa mbele. Kwa sasa nafanya kazi katika shirika moja ambapo mkataba wangu unaenda kuishia.
Napata changamoto kadhaa ambazo zimenifanya nije humu ndani, sijanikiwa kufanya akiba yoyote hadi sasa. Napata lawama nyingi sana kutoka kwa ndugu, kwa maelezo yao binafsi nimewahi kuishi na mwanamke.
Huyu binti nilimfungulia duka-denge na ndiyo analofanya hadi leo, japo halikui, muda mwingi naona hela natoa mfukoni mwangu.
Hivyo naombeni ushauri wana JF maana naona kwenda kuumbuka. Kiumbe kinapokuja pasipo na maandalizi ya kimaisha, uwezo wa yeye kwenda kujifungua hiyo hela ninayo, mimi ninachoumiza kichwa nitawezaje kuishi na mwanamke na familia ilihali sina kazi kwa sasa.
Kuna muda namchukia na kumuongelea vibaya hadi najisikia vibaya. Nilikuwa nasali ila nimeacha. Nayaogopa maisha ya mbele yangu.