Ushauri: Nilibadili kozi chuoni pasipo kumtaarifu mwajiri wangu

sir ronga

Member
Nov 25, 2016
90
107
Salaam wana JF,

Kama mada inavyodokeza, mimi niliwahi kuajiriwa serikalini kama mwalimu wa secondary kwa muda wa miaka minne. Baada ya hapo niliomba ruhusa ya kwenda masomoni kujiendeleza. Mara baada ya kufika chuoni, niliamua kubadili kozi na kusoma fani niliyokuwa naipenda hapo awali kwani nilishindwa kuisoma kutokana na changamoto za maisha ikiwemo kukosa ada. Kozi yenyewe ni ya miaka minne.

Mwaka mmoja baadae, nilitakiwa kuwasilisha ripoti kazini ila sikufanya hivyo kwani sikuwa nasomea education. Kila likizo nilikwepa kurudi kituoni kwa sababu mbalimbali. Nikiwa chuo mwaka wa mwisho(wa nne), likapita fagio la Magufuli mshahara ukasimama. Nilihesabika kama mtoro kazini.

Kwasasa nakaribia kuhitimu elimu yangu, na nipo katika mchakato wa kujiajiri na changamoto ni lukuki. Nikakumbuka nilipokuwa kazini nilikuwa mwanachama wa mifuko kadhaa ikiwepo PSPF na CWT na nilikuwa nachangia wastani wa 25,000 kwa mwezi kila mfuko kipindi nasitishiwa mshahara.

Naombeni ushauri katika haya na mengineyo:
1.Naweza kupata stahiki zangu kwa kipindi nilichodumu kazini?
2.Nawezarudi kazini ili hali sikusomea nilichoombea ruhusa?
3.Ikitokea nafasi nyingine ya kuajiriwa serikalini kupitia hii kozi mpya bila tatizo?
4. Ushauri wa ziada wa nini nifanye kuhusu hili.

Ahsanteni.
 
Mkuu rudi kwa Mkurugenzi wako, kwani umepewa barua ya kusimamishwa au kuachishwa kazi? Japo umeiibia Serikali na kuwaacha wanafunzi wanahangaika huku wewe ukijitafutia maslahi yako na kutwanga kodi za wananchi kwa miaka kadhaa...
 
Kozi gani uliyosomea chuoni. Usije kukuta ni Archaeology au BA Kiswahili halafu unauponda ualimu.
 
Ualimu ni wito kweli. Wengi walikuwa wanaachaga ila wanachukua mikopo kwanza ndipo wanasepa ili ikawasaidie huko waendako kama mtaji wa kujiajiri. Sasa wewe ulikosea, ungechukua mkwanja wa kutosha kabla ya kuondoka.

Ushauri:
Ficha cheti chako, Nenda ukajaribu kuomba urudi kazini kama utakubaliwa. Sema uliugua ukichaa na chuo hata hukumaliza. Au sema walikuloga. It's funny but it works 100%
 
Kwa mambo yalivyo magumu sasa hivi ata usijisumbue kurudi!
Wenzenu wakifanya hivyo huwa wanakula dili angalau na mkuu wa shule!
Hiyo mifuko uliyokiwa unachangia huwa wasumbufu sana utazungushwa mpaka utaamua kuacha tu!
 
Imekula kwako, tena kuna uwezekano ukapigwa pingu kama ukimkuta mkurugenzi chizi huko halmashauri ulikoajiriwa.
Watanzania tuko rough sana katika kupanga na kuamua mambo. Hapo huajiriki tena serikalini.
 
Wewe ni staki nataka. Unataka kurudi kazini kufanya nini ihali hukupenda kusomea ualimu? Si uende ukafanye kazi za hiyo fani uliyokuwa unaipenda? Acha kupoteza muda na resources za serikali!
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Ualimu ni wito kweli. Wengi walikuwa wanaachaga ila wanachukua mikopo kwanza ndipo wanasepa ili ikawasaidie huko waendako kama mtaji wa kujiajiri. Sasa wewe ulikosea, ungechukua mkwanja wa kutosha kabla ya kuondoka.

Ushauri:
Ficha cheti chako, Nenda ukajaribu kuomba urudi kazini kama utakubaliwa. Sema uliugua ukichaa na chuo hata hukumaliza. Au sema walikuloga. It's funny but it works 100%
Duh.. eti aliugua ukichaa!!
 
kwa wakurugenzi wa awamu hii na jinsi uongozi wa kibabe... nakuonea huruma sana
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Usiandike bila utafiti.
Hakuna Mwalimu mwenye basic ya Tsh300,000.
Kwa hiki kiwango anachokatwa mshahara wake ni Tsh530,000.
Fanya utafiti ndio uandike hata kama mikono inakuwasha.
duuh ulikua unachangia elfu 25 kwa mwezi PSPF ina maana mshahara ulikua chini ya laki tatu ...duuh kweli kazi ya Ualimu ni wito
 
Usiandike bila utafiti.
Hakuna Mwalimu mwenye basic ya Tsh300,000.
Kwa hiki kiwango anachokatwa mshahara wake ni Tsh530,000.
Fanya utafiti ndio uandike hata kama mikono inakuwasha.

Mwalimu wa cheti anaanza na mshahara wa sh ngapi?
 
duuh ulikua unachangia elfu 25 kwa mwezi PSPF ina maana mshahara ulikua chini ya laki tatu ...duuh kweli kazi ya Ualimu ni wito
Pengine alikuwa na diploma. Kasema alisitishiwa ajira mwaka jana, itakuwa alikuwa anapokea kama laki 5 na kitu au sita
 
Usiandike bila utafiti.
Hakuna Mwalimu mwenye basic ya Tsh300,000.
Kwa hiki kiwango anachoyake hyo elfu 25 a mshahara wake ni Tsh530,000.
Fanya utafiti ndio uandike hata kama mikono inakuwasha.
Kasema alikua anakatwa elfu 25 na inajukikana kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii huwa inakata 10% ya basic salary sasa piga hesabu hapo kwa maelezo yake hyo elfu 25 ni sawa na mshahara wa shilingi ngapi
 
Imekula kwako na kurudi tena Serikalini hata kwa kazi tofauti sahau
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom