Ushauri: Ni sehemu gani nzuri ya kuishi kati ya Tukuyu ama Kyela?

Nenda tukuyu huo mchele wa kyela unafika tukuyu kwa bei ile ile.
Habari wakuu...

Niende moja kwa moja,ni hivi nataka kuhamia MBEYA na lengo langu ni kuishi moja kati ya sehemu nilizotaja hapo juu,"TUKUYU ama KYELA.

LENGO KUU

Kuishi sehemu ambayo sitatumia zaidi ya 2500/= kwa upande wa chakula,na nishibe vizuri tu.Niwe chimbo uko nidundulize walau nikirudi Dar es Salaam nifanye kitu cha maana.

Kwanini Mbeya?
Napenda sana mikoa yenye baridi lakini pia chakula cha kutosha.
Sehemu yenye baridi hakuna matumizi kama ya Feni,Jokofu(Fridge) n.k


Sasa kwanini Tukuyu na Kyela? na si kwingine?

TUKUYU
Kwa utafiti mdogo nilioufanya naskia hii ndo sehemu ambayo huwa na baridi sana kuliko zote mbeya.
Lakini pia kwa mtu kama mimi ninayeenda kuanza maisha vyumba vya 10,000/= mpaka 20,000/= kwa mwezi napata.
Naskia pia kuna ndizi za kutosha.

KYELA
Huku naskia mchele mzuri na mtamu kwa gharama nafuu ndo kwao,pia samaki wazuri watamu kwa gharama nzuri pia wapo wa kutosha.

Wakuu hizi zote ni mbinu za kivita kuona walau kama tunaweza kuyashinda mapambano ya kiuchumi.

Hivo naomba kama kuna anayekaa au aliwahi kuishi sehemu hizo mbili anisaidie uzoefu wake na taarifa kwa kina.

NB
Nataka nikaishi maisha ya hadhi ya chini tu(nipo tayari) ila yenye MALENGO.
Naamini baada ya miaka mitano sintakua mimi yule.

"Tough times never last,but tough people do".
 
Tukuyu ila baridi lake sasa. Kule hakuna jua.
Napenda sana iyo hali.
Labda niwe muwazi tu,huwa nikiwa sehemu za joto Malaria inanionea sana,ila sehemu ya baridi mbu hakuna,hivo hakuna hata haja ya chandarua,maisha yanakua mepesi kiasi fulani.

Pia kwenye baridi hakuna ubishoo,unapigilia mkoti wako mwanzo mwisho....dah sjui ata nisemeje ila napenda sana maisha ya kwenye baridi
 
Tukuyu ila baridi lake sasa. Kule hakuna jua.
Maisha yanaendelea
5b552f9cde24093af9ac3bde5295d595.jpeg
 
Kama Moscow vilee...raha sana.
Hali kama hii upo zako ndani unaangalia mpira ama movie, huku una uhakika wa chakula cha kutosha tena asilia(Natural).....Mungu akupe ninii
Maparachichi na ndizi za kuchoma/kukaanga,maziwa ya mgando lita sh1,000,samaki wa ziwa nyasa wanapatikana kwa wingi boda ya Kasumulu.
Ishi Kk au Kiwira. Kyela maisha ni magumu sana kuyaanza
 
Habari wakuu...

Niende moja kwa moja,ni hivi nataka kuhamia MBEYA na lengo langu ni kuishi moja kati ya sehemu nilizotaja hapo juu,"TUKUYU ama KYELA.

LENGO KUU

Kuishi sehemu ambayo sitatumia zaidi ya 2500/= kwa upande wa chakula,na nishibe vizuri tu.Niwe chimbo uko nidundulize walau nikirudi Dar es Salaam nifanye kitu cha maana.

Kwanini Mbeya?
Napenda sana mikoa yenye baridi lakini pia chakula cha kutosha.
Sehemu yenye baridi hakuna matumizi kama ya Feni,Jokofu(Fridge) n.k


Sasa kwanini Tukuyu na Kyela? na si kwingine?

TUKUYU
Kwa utafiti mdogo nilioufanya naskia hii ndo sehemu ambayo huwa na baridi sana kuliko zote mbeya.
Lakini pia kwa mtu kama mimi ninayeenda kuanza maisha vyumba vya 10,000/= mpaka 20,000/= kwa mwezi napata.
Naskia pia kuna ndizi za kutosha.

KYELA
Huku naskia mchele mzuri na mtamu kwa gharama nafuu ndo kwao,pia samaki wazuri watamu kwa gharama nzuri pia wapo wa kutosha.

Wakuu hizi zote ni mbinu za kivita kuona walau kama tunaweza kuyashinda mapambano ya kiuchumi.

Hivo naomba kama kuna anayekaa au aliwahi kuishi sehemu hizo mbili anisaidie uzoefu wake na taarifa kwa kina.

NB
Nataka nikaishi maisha ya hadhi ya chini tu(nipo tayari) ila yenye MALENGO.
Naamini baada ya miaka mitano sintakua mimi yule.

"Tough times never last,but tough people do".
kyela ndo mpango mzima,2500 kwa msosi mmoja we boss,kwanza utanawiri sana,samaki mbasa,mberere wali ndo nyumbani kwake,beach kama lote,,matema,itungi etc,hutarudi tena mjini.
 
Napenda sana iyo hali.
Labda niwe muwazi tu,huwa nikiwa sehemu za joto Malaria inanionea sana,ila sehemu ya baridi mbu hakuna,hivo hakuna hata haja ya chandarua,maisha yanakua mepesi kiasi fulani.

Pia kwenye baridi hakuna ubishoo,unapigilia mkoti wako mwanzo mwisho....dah sjui ata nisemeje ila napenda sana maisha ya kwenye baridi
Nenda Tukuyu. Green city.
 
15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom