Ryzen
JF-Expert Member
- Dec 6, 2012
- 7,305
- 8,655
Habari za siku ndugu wanafamilia wa JF!, Poleni na Majukumu Mazito ya kifamilia na ya kutafuta Mkate wa Kila siku hasa kwa awamu hii ngumu ya 5.
Naomba nianzie hapa..
Kwanza kabisa mimi ni kijana wa Miaka 28 mwenye elimu ya shahada moja, katika harakati za maisha nilifanikiwa kukutana na binti mmoja miaka takribani 6 iliyopita, Nilitokea kupendana naye sana.
Huyu binti ni mtoto wa kishua ukilinganisha na familia yetu.. mara nyingi amekuwa akinisumbua katika mahusiano yetu(Hakuwahi kuonesha kunicheat).. hasa kwa kutaka breakup za ghafla ambazo anadai mzee wake anamshinikiza aachane na mimi.. huwa natulia anajiachisha kisha anajirudisha (Mapenzi yake kwangu hayakupungua mpaka hivi sasa naandika uzi huu).
sasa kwa kipindi chote tumekuwa tukipanga kuoana.. ila ninachogundua ni kwamba binti yupo tayari kishingo upande.. yaani ananipenda ila akifikiria status ya familia yangu haifanani na ya kwao anarudisha moyo wake nyuma ghafla na hata kutaka kubreakup.. akijisahau hurudisha mapenzi na ananipenda kama kawaida.
Kwa sasa imefika wakati ambao hata mimi nimeanza kuchoka na mwanamke ambaye hatabiriki..leo hivi kesho vile.. nataka nioe, Japo favorite option ni yeye.. Nampenda huyu mwanamke.. ila kigezo cha yeye kuwa kishua na kuonekana kutoridhika na hali ya kwetu kinanipa wasiwasi endapo kama huyu binti ataweza kunivumilia au la..(i'm sure of being financialy free)
Kuna wakati akipitiwa hujisahu na kuropoka kabisa kuwa baba yake hapendi aolewe na mimi na mara kadhaa amemsihi asiwe hata na mahusiano na mimi.. nikiwa naye haya maneno najifanya kuchukulia kirahisi but kiukweli ni maneno mazito.
Ndugu zangu.. mimi kama mtu mzima sasa.. nina uwezo wa kufanya mbinu zozote(Hata kwa Figisu) za kumuoa tu awe mke wangu.. ila je madhara ya kuwa na mke wa aina hii itakuwaje? ..kwa maana sitaki familia isiyo na Amani ...mtu ambaye mzazi wake hataki awe nami.. na kwa kiasi kikubwa hata kama ananipenda ameonesha kumsapoti mzee wake.
Ndugu zangu wanafamilia wa JF tumetofatiana uzoefu achilia mbali kuzidiana mitazamo.. ni matumaini yangu kuna watu wenye uzoefu na matukio ya aina hii.. naombeni mnipe ushauri kwa nyinyi wenye uzoefu..je kuna madhara gani kumuoa mwanamke mwenye situation kama hiyo?.. Je unashauri nimuoe au Niache?.. Je una maoni gani ya kudeal na situation ya aina hii?
Asanteni Sana
Khan
Naomba nianzie hapa..
Kwanza kabisa mimi ni kijana wa Miaka 28 mwenye elimu ya shahada moja, katika harakati za maisha nilifanikiwa kukutana na binti mmoja miaka takribani 6 iliyopita, Nilitokea kupendana naye sana.
Huyu binti ni mtoto wa kishua ukilinganisha na familia yetu.. mara nyingi amekuwa akinisumbua katika mahusiano yetu(Hakuwahi kuonesha kunicheat).. hasa kwa kutaka breakup za ghafla ambazo anadai mzee wake anamshinikiza aachane na mimi.. huwa natulia anajiachisha kisha anajirudisha (Mapenzi yake kwangu hayakupungua mpaka hivi sasa naandika uzi huu).
sasa kwa kipindi chote tumekuwa tukipanga kuoana.. ila ninachogundua ni kwamba binti yupo tayari kishingo upande.. yaani ananipenda ila akifikiria status ya familia yangu haifanani na ya kwao anarudisha moyo wake nyuma ghafla na hata kutaka kubreakup.. akijisahau hurudisha mapenzi na ananipenda kama kawaida.
Kwa sasa imefika wakati ambao hata mimi nimeanza kuchoka na mwanamke ambaye hatabiriki..leo hivi kesho vile.. nataka nioe, Japo favorite option ni yeye.. Nampenda huyu mwanamke.. ila kigezo cha yeye kuwa kishua na kuonekana kutoridhika na hali ya kwetu kinanipa wasiwasi endapo kama huyu binti ataweza kunivumilia au la..(i'm sure of being financialy free)
Kuna wakati akipitiwa hujisahu na kuropoka kabisa kuwa baba yake hapendi aolewe na mimi na mara kadhaa amemsihi asiwe hata na mahusiano na mimi.. nikiwa naye haya maneno najifanya kuchukulia kirahisi but kiukweli ni maneno mazito.
Ndugu zangu.. mimi kama mtu mzima sasa.. nina uwezo wa kufanya mbinu zozote(Hata kwa Figisu) za kumuoa tu awe mke wangu.. ila je madhara ya kuwa na mke wa aina hii itakuwaje? ..kwa maana sitaki familia isiyo na Amani ...mtu ambaye mzazi wake hataki awe nami.. na kwa kiasi kikubwa hata kama ananipenda ameonesha kumsapoti mzee wake.
Ndugu zangu wanafamilia wa JF tumetofatiana uzoefu achilia mbali kuzidiana mitazamo.. ni matumaini yangu kuna watu wenye uzoefu na matukio ya aina hii.. naombeni mnipe ushauri kwa nyinyi wenye uzoefu..je kuna madhara gani kumuoa mwanamke mwenye situation kama hiyo?.. Je unashauri nimuoe au Niache?.. Je una maoni gani ya kudeal na situation ya aina hii?
Asanteni Sana
Khan