Miss Natafuta
JF-Expert Member
- Sep 16, 2015
- 25,557
- 45,827
Nilipata mpenzi huku mkaka moja mzuri tu mwana JF, anaonekana ni mtu mwema japo ana mambo yake flani ila nimempa tu muda hata mimi najijua nina madhaifu yangu. Nina boss wangu, yule mzee ananipenda sana kama binti yake anajua sina mwanaume yoyote ananichukulia kama binti mwenye heshima tu na maskini kwaiyo ananilipia kodi, pocket money za hapa na pale.Tena anataka nikakae kwake inshort napata full sponsorship hapa mjini.
Sasa natamani nimtambulishe huyu mpenzi wangu ili asiwe ananichukulia kirahisi kivile ila naona kama udhamini utakoma. Hajawahi kunitaka kimapenzi na najua anajiheshimu sana wala hatokaa anitake ila nataka kuwa huru na maisha yangu.
Kwa situation hii nifanyeje wadau?
Sasa natamani nimtambulishe huyu mpenzi wangu ili asiwe ananichukulia kirahisi kivile ila naona kama udhamini utakoma. Hajawahi kunitaka kimapenzi na najua anajiheshimu sana wala hatokaa anitake ila nataka kuwa huru na maisha yangu.
Kwa situation hii nifanyeje wadau?