Ushauri: Nataka mtoto wa mdogo wangu nimsomeshe, shangazi yangu anakataa

NIMPENDENANI

JF-Expert Member
Nov 2, 2014
6,114
5,380
Eid Mubarak Waungwana,

Nina jambo linanitatiza kichwa na sijui hata niamue vipi, mtoto wa shangazi yangu amefariki amewacha watoto wa5, lakini kabla ya kufariki mtoto wa shangazi niliongea na Dad kua nimejisikia vibaya kuona hali nilomkuta sasa nikamwambia Dad acha nimchukue huyu mtoto wa kike as niko na watoto wa kike nisingependa kumuona mtoto yule anakulia kwenye mazingira ya ajabu.

Dad kasema sawa, siku ilofatia nika omba shangazi aje Dad na mtoto wa shangazi yangu mkubwa wa yule mgonjwa, nikamuomba mgonjwa kua anipe mtoto nimsaidie kulea na mimi ndio ntakua responsible kwa chochote cha yule mtoto sio yeye tena kuanzia shule na maisha yake yote, masikini hakukataa baada ya 2days akafariki, mimi nikawa nimesha chukua jukumu.

Baada ya mazishi watu wakagawana watoto mimi nikasema huyu mmoja ananitosha, wakabakia wa 4 dad akachukua 2 kids na 2 wakawa kwa bro, sasa jana huyu mtoto mkubwa wa shangazi amekuja anasema amekuja kumchukua huyu binti ninaekaa nae anataka kuishi nae na mtoto yuko shule na wenzie anasema atampeleka shule akajifunze Hotel managemnt.

She is only 18 yrs na mtoto anavalishwa ma baibui anabanwa mtu na shape yake mimi namfunga funga, shangazi nimemwambia hasemi kitu Dad anasema mpe jamani huyu mtoto ataharibika as huyu mtoto wa shangazi watoto wake hakuna hata alomaliza hata la 7 iweje leo akamsomeshe mtoto wa mdogo wake, kwenye issue kama hii wapi niende as huyu binti atapotea nahitaji msaada, sina shida ya wa toto ninao wangu 6 Alhamdulillah ila huyu anahitaji kusoma sio kwenda kumufanya akawa hana maisha najisikia vibaya sana au niwache kama ilivyo? Na je huyu mtoto akishaharibika nani atakua responsible as she is only 18

Nahitaji msaada wenu wa mawazo please.

Hapo nimekupeni kwa ufupi ili nisiwachoshe.
 
Hebu waweke wazi hao ndugu, na ueleze lengo lako ni kumuelimisha
Mkuu wanajua na wanaona huyu mtoto wa shangazi mwehu sanaaa yani kanikeraaa yeye watoto wake wote wameolewa 19yrs 20yrs na wameshaachwa wana randa yeye mwenyewe leo yuko Arusha kesho yuko mwanza hana makazi maalum
anataka kumuharibia maisha tuu..
 
Mmmmh! embu baki na huyo binti umleee, ataenda kugeuzwa ajira auzwe mbele na nyuma roho ije ikusute baadae.
Darling inaniumaaaa kupita kiyasi,nimejiuliza jee ningekua sina mtoto si ningekufa mimi kwa BP? na jengine alimtaka mtoto aende kwake nikamwambia asubiri mpaka afunge shule ndio atakwenda kutembea sasa kaona aje amchukue kabisa wakati namchukua hakusema kamuona sasa ni msichana ndio anaaza kutaka kumfisidi...
 
Kama ako 18 tayari ni mtu mzima.. Mwambieni achague yeye anataka aishi na wewe au la...

Kaa nae ongea nae atakuelewa tuu kama ni mtoto anaejitambua, achague analoona lina faida kwenye maisha yake ya baadae
 
NIPENDEMIE, huo mchanganyiko ni wa hatari. Nimeambulia tu mnayemgombania yuko 18, meaning kisheria anatambulika kama mtu mzima na anaweza kujiamulia nini bora kwake.
kwa hiyo mtoto akisema anataka kuishi mwenye its fine anataka kuishi na mimi its okay au na mamake mkubwa ni sawa?
lakini still bado mdogo na that age atataka all the freedom she wants na ndi mwanzo wa kuharibika..
 
Kama ako 18 tayari ni mtu mzima.. Mwambieni achague yeye anataka aishi na wewe au la...

Kaa nae ongea nae atakuelewa tuu kama ni mtoto anaejitambua, achague analoona lina faida kwenye maisha yake ya baadae
Mrembo she is 18 lakini namchukua same as my Daughter siwezi kusema mtoto wangu she is 18 ndio amekua aamue anachotaka sio sawa yule mamake mkubwa ni muharibifu tuu,shule mbona hakupeleka wanawe? na wakati namchukua mbona hakusema ntamlea mimi? au wale wa4 why asichukue mmoja why huyu nnae lea mie? anajua she will have bright future as nxt year wanakwenda Toronto kusoma sasa hapendi maendeleo ya huyu mtoto thats what i can see,manake silioni..
 
Mkuu wanajua na wanaona huyu mtoto wa shangazi mwehu sanaaa yani kanikeraaa yeye watoto wake wote wameolewa 19yrs 20yrs na wameshaachwa wana randa yeye mwenyewe leo yuko Arusha kesho yuko mwanza hana makazi maalum
anataka kumuharibia maisha tuu..
Tafuta ndugu mwenye busara na mwenye kuheshimika awatolee maamuzi
 
Mkuu pole sana na hongera kwa kujitolea. Lakini huo uandishi wako utachangia kukosa mawazo ya watu wengi, haueleweki vizuri. "...As if..as if... " unatutoa bila bila.
Pole sana mkuu nna hasira kupindukia..
 
You got six kids? Wow..Mungu amekubariki uzazi, hongera sana. The rest of the story sijaelewa vizuri, lemme hear from others.
Alhamdullah yes mara 2 nilijifungua twins ...sorry kama hujaelewa nimeandika kwa hasiraaaaaaaa naona kama nachelewa...
 
Mkuu wanajua na wanaona huyu mtoto wa shangazi mwehu sanaaa yani kanikeraaa yeye watoto wake wote wameolewa 19yrs 20yrs na wameshaachwa wana randa yeye mwenyewe leo yuko Arusha kesho yuko mwanza hana makazi maalum
anataka kumuharibia maisha tuu..
Sasa mbona teyari unafahamu nn kinachofata...we madam ulishachukua jukumu la kumsomesha vp sasa umpe mtu mwingine??halafu huyo ameshakuwa mtu mzima mwelimishe achague mwenyewe inawezekana we unataka asome kumbe mwenzio anawasiliana na huyo shangazi ako aje amchukue akaishi nae..ila na wewe kama miezi uliyekabidhiwa mtoto na marehemu una final say juu ya mtoto..
 
Back
Top Bottom