sibbonnobo
JF-Expert Member
- Aug 24, 2019
- 724
- 877
Wana nzengo ngoja na mimi nitiririke kidogo leo kutokana na masaibu yangu.
Waswahili wanasema "Unaweza kupenda chongo ukaita kengeza au kipendacho roho hula nyama mbichi n.k".
Kwa miaka miwili nimekuwa na demu wangu tulikutana tu kwenye mitandao ikatokea tumependana tukaanza mahusiano, lakini kwa upande wangu hasa ninampenda sana na nilikuwa na nia ya kumfanya mama watoto.
Katika uchunguzi wangu niligundua kuwa amepitia mahusiano mengi sana na wengine walidiriki hata kumfungulia biashara ila zilikufa baadae. Niligundua pia shoga zake ni wadangaji. Hata yeye alikuwa katika hayo mambo.
Kwa kuwa nimependa, nilijaribu sana kumuondoa katika maisha yasiyo na muelekeo na alionyesha kutii hilo japokuwa kuna matukio nilikuwa siyaelewi elewi.
Kilichokuwa kikiniudhi anaweza kuvunja hata appointment na wewe kisa marafiki zake wamemuita. Ukimwambia nikutoe anasema hajisikii ila rafiki zake wakimualika lazima ahudhurie mwaliko. Na akija geto muda mwingi yuko busy anachati. Na hataki kabisa usogelee simu yake.
Cha kushangaza anapenda sana kuchunguza simu yangu na akikuta madudu ni ugomvi sana. Nikiri tu kuwa ni kweli nilikuwa nawapelekea moto wanawake na ni kwa sababu kutolipa kipaumbele suala la kukutana na yeye kimwili akidai tuwe busy na kutafuta hela hayo mapenzi yapo tu.
Kuna wakati nampigia simu usiku yupo viwanja vya starehe bila taarifa ukimuuliza yuko wapi ni ngumu kukupa jibu.
Ni mengi ila najaribu kufupisha. Jana nimemgombeza sana kiasi kwamba kwa hasira kuna maneno mazito niliongea na aka rise issue kwamba nimemkashifu na mwisho wetu ndio huo hataki lolote kutoka kwangu.
Shida inakuja kati ya moyo na akili zangu. Nikifikiri kwa kina akili inasema huyu si mwanamke wa kuwa nae ila moyo bado unampenda sana. Nifanyeje??
Naomba niishie hapo. Kwenu wakuu.
Waswahili wanasema "Unaweza kupenda chongo ukaita kengeza au kipendacho roho hula nyama mbichi n.k".
Kwa miaka miwili nimekuwa na demu wangu tulikutana tu kwenye mitandao ikatokea tumependana tukaanza mahusiano, lakini kwa upande wangu hasa ninampenda sana na nilikuwa na nia ya kumfanya mama watoto.
Katika uchunguzi wangu niligundua kuwa amepitia mahusiano mengi sana na wengine walidiriki hata kumfungulia biashara ila zilikufa baadae. Niligundua pia shoga zake ni wadangaji. Hata yeye alikuwa katika hayo mambo.
Kwa kuwa nimependa, nilijaribu sana kumuondoa katika maisha yasiyo na muelekeo na alionyesha kutii hilo japokuwa kuna matukio nilikuwa siyaelewi elewi.
Kilichokuwa kikiniudhi anaweza kuvunja hata appointment na wewe kisa marafiki zake wamemuita. Ukimwambia nikutoe anasema hajisikii ila rafiki zake wakimualika lazima ahudhurie mwaliko. Na akija geto muda mwingi yuko busy anachati. Na hataki kabisa usogelee simu yake.
Cha kushangaza anapenda sana kuchunguza simu yangu na akikuta madudu ni ugomvi sana. Nikiri tu kuwa ni kweli nilikuwa nawapelekea moto wanawake na ni kwa sababu kutolipa kipaumbele suala la kukutana na yeye kimwili akidai tuwe busy na kutafuta hela hayo mapenzi yapo tu.
Kuna wakati nampigia simu usiku yupo viwanja vya starehe bila taarifa ukimuuliza yuko wapi ni ngumu kukupa jibu.
Ni mengi ila najaribu kufupisha. Jana nimemgombeza sana kiasi kwamba kwa hasira kuna maneno mazito niliongea na aka rise issue kwamba nimemkashifu na mwisho wetu ndio huo hataki lolote kutoka kwangu.
Shida inakuja kati ya moyo na akili zangu. Nikifikiri kwa kina akili inasema huyu si mwanamke wa kuwa nae ila moyo bado unampenda sana. Nifanyeje??
Naomba niishie hapo. Kwenu wakuu.