Biashara ya Duka la Rejareja: Ushauri, Mchanganuo, Changamoto na Namna ya Kutunza Kumbukumbu

Asante sana feity na wadau wengine mliochangia na mtakaoendelea kuchangia. Naamini kweli inaweza ikawa sijawaza vyema sana na ndio maana tunashirikishana wadau kupata mawazo pevu na mbadala, najua huku wako wadau wengi wenye ujuzi, ufahamu, uelewa na moyo wa kusaidia na kushauri. asanteni.
 
Mkuu Ibravo,
Kwanza kabisa nikukaribishe humu maana unaonekana umejiunga humu this month hivyo you are still junior member, kwa kifupi humu kuna changamoto nyingi na shauri nyingi ambazo hata nyingine zinaweza kukukatisha tamaa kabisa au hata kujuta kuwa hivi nani alikushauri kuingia humu na ku-post threads za hovyo hovyo (wachangiaji wengine wanaweza kuziona hivyo), leo nikupe changamoto moja juu ya hii thread uloleta hapa:

Ibravo, sina nia ya kukukatisha tamaa juu ya mpango wako wa kuanzisha biashara ya duka hilo kwa capital hiyo ambayo umebahatika kuipata, ila to be honest nimeshangazwa na kusikitishwa na wazo hili kutoka kwako (msomi/graduate mtarajiwa). Naomba niseme wazi kuwa elimu unayosoma haijakusaidia chochote na nadhani ulikuwa unapoteza muda huko au labda ulikosea fani ulokuwa unasomea, wapo vijana wengi wanaenda vyuoni kusoma kwa mkumbo tu bila kujua anakwenda kusomea nini hasa. Lakini nadhani hapa ni uelewa wako tu ndo maana una wazo la kujiajiri, vinginevyo ningekulaumu kwa namna tofauti.

Nina imani watajitokeza wana JF wengi ambao wakisoma mchango wangu huu hawatanielewa, ila acha tu niseme ulonilazimisha kusema hasa baada ya kusoma uzi wako Ibravo.

Hata kama tunasema UJASIRIAMALI, inawezekanaje MSOMI/GRADUATE mtarajiwa unatoka chuoni unapewa mtaji wa mil 1, then unakurupuka na wazo la kufungua duka la kuuza UNGA, MCHELE n.k (UCHUUZI)? hivi hapa tutasema shule/elimu imekusaidia??? Na hapa niseme kuwa kama vijana wengi mnaenda vyuoni mnalipa fees huko miaka 2,3-4 nakuendelea, mnamaliza mnakuja na mawazo ya namna hii huku mitaji ya kiasi hiki mnabahatika kupata then niseme wazi kuwa elimu itakuwa haijawasaidia. Haya ni mawazo MGANDO, mtu unataka kufanya kitu kwa mazoea tu kwa kuwa watu wanafanya, huu si UJASIRIAMALI, ujasiriamali ni uwezo wa kubaini fursa kulingana na mtaji ulionao.

Nafurahia sana na watu wanaokuja humu kuuliza ili wapate mawazo kutoka kwa wachangiaji wanaJF great thinkers, wengine wanaenda mbali zaidi kwa kutamka kiasi (initial capital) alichonacho na anaomba ashauriwe afanye shughuli gani, watu wanatoa ushauri ktk shauri hizo wanasema AKILI YA KUAMBIWA, CHANGANYA NA ZAKO, then unapata shughuli ya kufanya. Ibravo nimesema sina lengo la kukukatisha tamaa ila nakueleza tu ya moyoni, wewe umeleta hapa wazo ambalo tayari unalo kichwani ndo maana watu wameshindwa kukushauri ila nina imani wengi wamekushangaa GRADUATE mtarajiwa unaleta wazo la namna hii hapa. Shughuli unayotaka kufanya hata ambaye hajasoma anafanya tu, ni UCHUUZI huo. Nilitegemea msomo uje na wazo tofauti kabisa kwa mtaji huohuo kwa kuwa kwa mjasiriamali wa kweli mil. 1 ni mtaji tosha tu.

Baada ya kukueleza haya sasa nakupa wazo, unaweza kulichukua au ukaliacha integemea kama umenielewa au utaniona nimeku-dis sana; Kwanza kabisa kwa kuwa umesoma inabidi uwe na mawazo mchemko si mgando, inabidi uwe tayari kutoka mjini kwa kuwa kwa wazo lako ulilo nalo unaonekana unaishi ama unataka kuishi mjini tu, kwa mjasiriamali hili halimfungi kwa namna yoyote.

Pili inabidi uondokane na mawazo ya biashara hizi za UCHUUZI, jaribu kufikiria mawazo ya ki-uzalishaji zaidi, (kilimo, ufugaji, viwanda n.k) na siyo duka, kwa mtazamo wangu miye kuwa na duka la kununua na kuuza (UCHUUZI) ni uvivu wa kufikiri tu, hivi uliona wapi Mzungu anauza duka bwn? Hizi ni kazi za Wahindi, ni wavivu wa kufikiri tu. Sisemi Wazungu ndo bora sana ila walio wengi wana mawazo bora, yeye anafikiria akutengenezee SIMU, uwasiliane na jamaa zako, ukishaona umuhimu wake utamtafuta tu ununue kwake na hapo utaona WAVIVU WA KUFIKIRI aka WACHUUZI wanapanga foreni kiwandani kwa Mzalishaji kuweka order ya handsets za simu, JAMAA ANAPIGA HELA. MZALISHAJI anatengeneza kitu BORA kwa kuwa anajua WAVIVU WA KUFIKIRI/WACHUUZI watamsaidia (bila wao kujua) kuuza bidhaa zake.

Ibravo nimesema sikukatishi tamaa ila ningekukubali kama ungekuja hapa na wazo kuwa kwa kuwa umeenda shule basi ungeuliza humu kuwa una mtaji wa hela hiyo (1mil) then unataka kulima Mahindi, Mpunga n.k (kwa kuwa unaonekana una interest na vitu hivyo) then upate sasa mawazo ya GREAT THINKERS. Asikwambie mtu, KILIMO ni moja ya UZALISHAJI na si UCHUUZI, wewe lima tu kitaalamu, vuna mazao yako, utaona WACHUUZI wanakuja wenyewe kutaka kuuza bidhaa zako, we unapiga hela tu unakuna kitambi (unajua tena wabongo kwa vitambi) na nikupe siri, Tsh. 1,000,000/= kuwekeza kwenye kilimo ni mtaji mkubwa mno (kama upo tayari kuondokana na mawazo ya kukaa mjini).
Huku kwetu kukodi heka moja ni Tsh. 30,000 hadi 45,000 kwa mwaka na huku kwetu kwa mwaka tunalima mara mbili (mvua za vuli na masika), kwa hela ulonayo utakuwa na heka za kutosha, sema anza na heka 5 ambayo itakugharimu Tsh. 225,000/= kukodi tu mashamba. kulima kwa tractor kila heka moja ni tsh. 40,000 x 5= 200,000/= zinazobaki fanya matumizi mengine kama palizi, mbolea na matumizi mengine kama hayo, hapa bro unazungumzia miezi mitatu tu kama ume time mvua za vuli tayari utakuwa na magunia yako 5x15= 75 ya mahindi, huku kwetu wakati wa msimu wa mavuno gunia la mahindi linauzwa Tsh. 45,000/= x 75= 3,375,000/=, kumbuka hapa umelima mvua za vuli tu, utaingia tena shambani mwezi Feb ili u-tme mvua za masika, na hakuna tena gharama ya kukodi maana ni ileile ulolipa awali, mwezi wa sita tena unavuna mazao yako unasubiria WACHUUZI tu, unapiga hela. Mkuu ukikomaa ki-jasiriamali baada ya miaka michache nina uhakika mashamba hutakodi tena, utakuwa na ya kwako, utaanza ufugaji, maana kuna uzi wa MALAFYALE Jukwaa la Ujasiriamali unasema 'Kilimo na Ufugaji kwa pamoja vinalipa' nenda kasome pale uone GREAT THINKER wanavyokuwa na mawazo ya ki-GT.
Kwa leo mkuu.

Ushauri mzuri sana mkuu ila nawe ni vyema ukashauriwa kama bado una mawazo mgando. Kwanza nikukatishe katika hizi biashara ulizoziita za uchuuzi zimetoa mabillionea kama Amarcio ortega okay tukiachana na hawa turudi kwa hao wazungu uliowasema haawafanyi kuna huyu mfaransa Benard Arnaut njoo mwana mama Lilliane Bettemcount SIJUI HAWA UTASEMAJE WAMEINGIA FORBES KWA BIASHARA ZA RETAILING (UCHUUZI)

Rudi kwetu Tz Mfugale kaanzia biashara ya duka ndio imemfikisha kuwa billionea kwa hiyo ushauri wako una mikingamo kitu ambacho si kizuri kibiashara million moja inatosha kabisa kuanzisha duka KUFIKIA UMILIONEA HIYO NI AKILI YAKO


NGOJA NIKUCHANGANULIE UONE USIJIUNGE KATIKA HAWA WENGINE WENYE KUDHARAU

Kodi ni elfu 50 kwa mwezi utaitoa ya miezi mitatu 150000
Friji laki tatu kubwa
Shelf za kawaida elfu 80
umashamaliza =530,000 jumla kinachobaki mahitaji na katika mahitaji yako usisahau kuweka maji ya kandoro na barafu vyote viwili mtaji wake hauzidi 40,000 yaani kununua deli elfu 20 na inayobaki materials

Kwa hiyo laki nne utanunua mahitaji ya duka laki tano na 70 ya kodi frij shelf na deli la maji kandoro + barafu

BILLONAIRE WENGI DUNIANI HAWATOKI SEKTA YA KILIMO NI SEKTA YA TECHNOLOGIA BIASHARA NA UWEKEZAJI

NA BADILIKA MKUU ELIMU YA DARASANI HAIHUSIANI NA MAWAZO YA KIBIASHARA/UBUNIFU HAYO NI MTU MWENYEWE anajiongoza kiasi gani

hata uwe na masters doesn't mean utaweza kuyatawala mazingira ELIMU KWA MTU YEYOTE INAONGEZA KUJITAMBUA HICHO NI TOFAUTI NA MAFANIKIO

Kama unabisha hebu soma muda gani Marekani/dunia ilibadilika katika kuamini Elimu at what time world rule changed
obviously its 1973
 
Hii biashara unalipa hasa km utakuwa unakaa mwenyewe dukani! kwani faida yake ni hizo 50 na mia mia...ukimueka mtu kila siku akichukua buku 5 atakuuwa! kaa mwenyewe utaenjoy biashara..pia usiwe na tabia yakufunga funga duka mara kwa mara! hakikisha unafungua duka mapema na unachelewa kufunga! mteja anapenda duka linalofunguliwa mapema utajijengea jina! 10% ndio faida yako
 
Hii biashara unalipa hasa km utakuwa unakaa mwenyewe dukani! kwani faida yake ni hizo 50 na mia mia...ukimueka mtu kila siku akichukua buku 5 atakuuwa! kaa mwenyewe utaenjoy biashara..pia usiwe na tabia yakufunga funga duka mara kwa mara! hakikisha unafungua duka mapema na unachelewa kufunga! mteja anapenda duka linalofunguliwa mapema utajijengea jina! 10% ndio faida yako
Nimeipenda, siri ya biashara yoyote ni kuzingatia muda wa kufungua na kufunga, pili usiwe mambo mengi mara leo upo kesho haupo,, tatu onesha ukali kias kwa anayetaka mazoea ndan ya biashara yako,, nne usibangue mtu yeyote neno ahasante mteja ni zao kuongeza wateja,,, kama unaumwa na umeamua kukaa dukan mteja wako muweke wazi, tano daftari la biashara uiheshim zaid ya pesa uliyoishika andika kila unachotumia toka dukan mwako, itakusaidia kutambua jinsi ya kubana matumizi, KUKATA TAMAA AU KUTOJIHAMIN HUTOWEZA FIKA POPOTE
 
Duh 2milion, unakazi kubwa mana kupiga shelves si chin ya laki sita kwa frem nzuri then jumlisha kodi ya Six month, ununue friji, inabaki tulaki kidogo unless ufungue kiduka mshenzi kama unavijua.

Location ni sehemu yenye makazi mengi ya watu tena wa hali ya kati sio Wale wa super market, au shughuli nyingi za watu.

Kinachopelekea hasara ni matumiz kuzid faida na bidhaa kuisha muda pia kuwa makin na watoto wa kike
 
Duka hilo unaweka mfanyakazi au unauza mwenyewe?
Umewah kufanya hiyo biashara au ndo unaanza?
Changamoto yake kubwa ni kuwa faida ya hiyo biashara imebase kwenye hela ndogondogo unaweza kuta faida kwa kitu ni sh 50,100,200 hivo usipokuwa makini badala ya kuendelea unaweza pata hasara
Mimi pia nina wazo la kufungua duka la namna hii, ila ninampango wa kuajir mtu coz mm ni mtumishi mahali pengine, mtaji wangu ni 5m, nishawah kukaa dukan kwa wazaz, naomba kujua kwa uzoef wako kama hiyo hela itatosha.
 
Pesa hiyo mil 5 inatosha sana cha msingi weka bidhaa zile zinazouliziwa usiende jitwisha mavitu ambayo yatauzika baada ya mwaka mmoja bora uanze kwa kuweka kidogokidogo huku ukiangalia kipi kinatoka haraka na kipi kinauliziwa sana.
 
Mimi pia nina wazo la kufungua duka la namna hii, ila ninampango wa kuajir mtu coz mm ni mtumishi mahali pengine, mtaji wangu ni 5m,nishawah kukaa dukan kwa wazaz ,naomba kujua kwa uzoef wako kama hiyo hela itatosha

Inatosha
 
Vitu vya Msingi

1. Location

Angalia sehemu utaweka hiyo biashara yako kuna watu wa aina/kipato gani hii itakusaidia hata kujua ni bidhaa za aina gani uweke dukani

2. Usimamizi
Nani atakuwa dukani full time
Nani atafanya manunuzi
Nani atakeep records/files zile muhimu 6 ambazo

1.File la mauzo
2.File la Manunuzi
3.File la Gharama za uendeshaji
4.File la Bank
5.File la TRA
6.File la Mikataba/Mengineyo

3.Mahusiano/Mawasiliano
Ili ufanikiwe lazima uwe na Mawasiliano na Kauli nzuri na wateja au jamii inayokuzunguka ukiwa na mahusiano mazuri kwa Upande wa suppliers unaweza pata hata bidhaa on credit

4.Timing
Nature ya biashara hizi zinahitajika kila saa hivyo UKICHELEWA kufunga na UKIWAHI kufungua una nafasi kubwa ya kufanikiwa. Timing vile vile inahusiana na ununuzi wa baadhi ya bidhaa ambazo ni za msimu Ukiziwahi waweza hata kuzinunua kwa half price.

Thank You
 
Mkuu Ibravo,
Kwanza kabisa nikukaribishe humu maana unaonekana umejiunga humu this month hivyo you are still junior member, kwa kifupi humu kuna changamoto nyingi na shauri nyingi ambazo hata nyingine zinaweza kukukatisha tamaa kabisa au hata kujuta kuwa hivi nani alikushauri kuingia humu na ku-post threads za hovyo hovyo (wachangiaji wengine wanaweza kuziona hivyo), leo nikupe changamoto moja juu ya hii thread uloleta hapa:

Ibravo, sina nia ya kukukatisha tamaa juu ya mpango wako wa kuanzisha biashara ya duka hilo kwa capital hiyo ambayo umebahatika kuipata, ila to be honest nimeshangazwa na kusikitishwa na wazo hili kutoka kwako (msomi/graduate mtarajiwa). Naomba niseme wazi kuwa elimu unayosoma haijakusaidia chochote na nadhani ulikuwa unapoteza muda huko au labda ulikosea fani ulokuwa unasomea, wapo vijana wengi wanaenda vyuoni kusoma kwa mkumbo tu bila kujua anakwenda kusomea nini hasa. Lakini nadhani hapa ni uelewa wako tu ndo maana una wazo la kujiajiri, vinginevyo ningekulaumu kwa namna tofauti.
Nina imani watajitokeza wana JF wengi ambao wakisoma mchango wangu huu hawatanielewa, ila acha tu niseme ulonilazimisha kusema hasa baada ya kusoma uzi wako Ibravo.
Hata kama tunasema UJASIRIAMALI, inawezekanaje MSOMI/GRADUATE mtarajiwa unatoka chuoni unapewa mtaji wa mil 1, then unakurupuka na wazo la kufungua duka la kuuza UNGA, MCHELE n.k (UCHUUZI)? hivi hapa tutasema shule/elimu imekusaidia??? Na hapa niseme kuwa kama vijana wengi mnaenda vyuoni mnalipa fees huko miaka 2,3-4 nakuendelea, mnamaliza mnakuja na mawazo ya namna hii huku mitaji ya kiasi hiki mnabahatika kupata then niseme wazi kuwa elimu itakuwa haijawasaidia. Haya ni mawazo MGANDO, mtu unataka kufanya kitu kwa mazoea tu kwa kuwa watu wanafanya, huu si UJASIRIAMALI, ujasiriamali ni uwezo wa kubaini fursa kulingana na mtaji ulionao.
Nafurahia sana na watu wanaokuja humu kuuliza ili wapate mawazo kutoka kwa wachangiaji wanaJF great thinkers, wengine wanaenda mbali zaidi kwa kutamka kiasi (initial capital) alichonacho na anaomba ashauriwe afanye shughuli gani, watu wanatoa ushauri ktk shauri hizo wanasema AKILI YA KUAMBIWA, CHANGANYA NA ZAKO, then unapata shughuli ya kufanya. Ibravo nimesema sina lengo la kukukatisha tamaa ila nakueleza tu ya moyoni, wewe umeleta hapa wazo ambalo tayari unalo kichwani ndo maana watu wameshindwa kukushauri ila nina imani wengi wamekushangaa GRADUATE mtarajiwa unaleta wazo la namna hii hapa. Shughuli unayotaka kufanya hata ambaye hajasoma anafanya tu, ni UCHUUZI huo. Nilitegemea msomo uje na wazo tofauti kabisa kwa mtaji huohuo kwa kuwa kwa mjasiriamali wa kweli mil. 1 ni mtaji tosha tu.
Baada ya kukueleza haya sasa nakupa wazo, unaweza kulichukua au ukaliacha integemea kama umenielewa au utaniona nimeku-dis sana;
Kwanza kabisa kwa kuwa umesoma inabidi uwe na mawazo mchemko si mgando, inabidi uwe tayari kutoka mjini kwa kuwa kwa wazo lako ulilo nalo unaonekana unaishi ama unataka kuishi mjini tu, kwa mjasiriamali hili halimfungi kwa namna yoyote.
Pili inabidi uondokane na mawazo ya biashara hizi za UCHUUZI, jaribu kufikiria mawazo ya ki-uzalishaji zaidi, (kilimo, ufugaji, viwanda n.k) na siyo duka, kwa mtazamo wangu miye kuwa na duka la kununua na kuuza (UCHUUZI) ni uvivu wa kufikiri tu, hivi uliona wapi Mzungu anauza duka bwn? Hizi ni kazi za Wahindi, ni wavivu wa kufikiri tu. Sisemi Wazungu ndo bora sana ila walio wengi wana mawazo bora, yeye anafikiria akutengenezee SIMU, uwasiliane na jamaa zako, ukishaona umuhimu wake utamtafuta tu ununue kwake na hapo utaona WAVIVU WA KUFIKIRI aka WACHUUZI wanapanga foreni kiwandani kwa Mzalishaji kuweka order ya handsets za simu, JAMAA ANAPIGA HELA. MZALISHAJI anatengeneza kitu BORA kwa kuwa anajua WAVIVU WA KUFIKIRI/WACHUUZI watamsaidia (bila wao kujua) kuuza bidhaa zake.
Ibravo nimesema sikukatishi tamaa ila ningekukubali kama ungekuja hapa na wazo kuwa kwa kuwa umeenda shule basi ungeuliza humu kuwa una mtaji wa hela hiyo (1mil) then unataka kulima Mahindi, Mpunga n.k (kwa kuwa unaonekana una interest na vitu hivyo) then upate sasa mawazo ya GREAT THINKERS. Asikwambie mtu, KILIMO ni moja ya UZALISHAJI na si UCHUUZI, wewe lima tu kitaalamu, vuna mazao yako, utaona WACHUUZI wanakuja wenyewe kutaka kuuza bidhaa zako, we unapiga hela tu unakuna kitambi (unajua tena wabongo kwa vitambi) na nikupe siri, Tsh. 1,000,000/= kuwekeza kwenye kilimo ni mtaji mkubwa mno (kama upo tayari kuondokana na mawazo ya kukaa mjini).
Huku kwetu kukodi heka moja ni Tsh. 30,000 hadi 45,000 kwa mwaka na huku kwetu kwa mwaka tunalima mara mbili (mvua za vuli na masika), kwa hela ulonayo utakuwa na heka za kutosha, sema anza na heka 5 ambayo itakugharimu Tsh. 225,000/= kukodi tu mashamba. kulima kwa tractor kila heka moja ni tsh. 40,000 x 5= 200,000/= zinazobaki fanya matumizi mengine kama palizi, mbolea na matumizi mengine kama hayo, hapa bro unazungumzia miezi mitatu tu kama ume time mvua za vuli tayari utakuwa na magunia yako 5x15= 75 ya mahindi, huku kwetu wakati wa msimu wa mavuno gunia la mahindi linauzwa Tsh. 45,000/= x 75= 3,375,000/=, kumbuka hapa umelima mvua za vuli tu, utaingia tena shambani mwezi Feb ili u-tme mvua za masika, na hakuna tena gharama ya kukodi maana ni ileile ulolipa awali, mwezi wa sita tena unavuna mazao yako unasubiria WACHUUZI tu, unapiga hela. Mkuu ukikomaa ki-jasiriamali baada ya miaka michache nina uhakika mashamba hutakodi tena, utakuwa na ya kwako, utaanza ufugaji, maana kuna uzi wa MALAFYALE Jukwaa la Ujasiriamali unasema 'Kilimo na Ufugaji kwa pamoja vinalipa' nenda kasome pale uone GREAT THINKER wanavyokuwa na mawazo ya ki-GT.
Kwa leo mkuu.
Mr/mrs thanks so much bro, umebadili fikra zangu za maisha
 
Hongera sana Mkuu karibu ktk ulimwengu wa fikira tofauti kwa wajasiriamali! vizuri ukifanya mwenyewe research kwa wafanya biashara na wenye maduka mbali mbali! ama kama upo tait nipe tenda hiyo Kampuni yangu inadeal na masoko inaweza kukufanyia kwa bei nafuu kabisa! my kampani ni Tangaza Marketing Solutions(TMs)
karibu sana.
Unapatikana wapi me nipo arusha nataka unifanyie research ya ɓiashara ya mitungi ƴya gas kwa hapa toun hapA nilipo wachawi wamekua wengi.
 
Habari zenu Wana Jamii Forum,

Mimi ni mwanafunzi wa chuo mwaka wa tatu,katika harakati za kujiandaa na kupambana na maisha pindi nitakapohitimu elimu yangu na kurudi mtaani,nimetafuta pesa ikiwa kama mtaji wa biashara milioni moja (1,000,000)hasa ya duka la bidhaa za vyakula.

Tatizo ni kwamba si mzoefu ktk biashara na ni mara ya kwanza kutaka kuifanya hii biashara kwan matarajio yangu ni kujiajiri mwenyewe.

Naomba ushauri kwa yeyote mwenye uelewa kuhusu hili kunipa mchanganuo wa bidhaa muhimu zinazotakiwa kuwepo dukani kama vile unga kiasi gani,mchele n.k kulingana na mtaji huo wa Milioni Moja.

Natanguliza Shukrani zangu.
Kwanza nakupongeza sana kwa wazo lako. Ushauri wangu kwa pesa uliyo nayo lima kilimo cha uyoga. Nenda kwa wataalam wa kilimo wakufunze ukulima huu wa Uyoga kwakua umsomi mafunzo hayatazidi wiki na gharama yake ni nafuu mno sh.20,000' utakua umejifunza ukulima na jinsi ya kudhibiti magonjwa ya Uyoga na wadudu waharibifu wa Uyoga.

Then gharama ya mbegu shilingi elfu 5,vyumba viwili cha giza na cha mwanga utalima humo na kuuza mahotelini na kwa Catering kwa bei nzuri utashangaa unaingiza pesa kiulaini tena ukiwa kivulini. Ni hayo tu.
 
Back
Top Bottom