USHAURI:mvua zimenifanya vibaya kilimo cha matikiti maji

Aventus

JF-Expert Member
Mar 8, 2013
1,914
1,977
Habari za mida hii?
Kama kichwa cha habar kinavojieleza.
Kabla ya kuomba ushauri wacha nitoe habar kamili.

Nilifanya uchunguzi mfupi na kugundua Mkoa wa Simiyu Wilaya ya Bariadi iko na wakulima wachache sana wa kilimo cha umwagiliaji hasa kwenye kilimo cha mboga mboga na matunda.Basi nikacheki nini kinaweza kulipa katika kilimo hicho cha umwagiliaji.kwa ushauri wa watu wa karibu tukaona tikiti maji ndo linalipa.
Kwa target ya haraka ni kulima kipindi cha mwezi wa tano kwenda wa sita ambapo mvua ndo zinaishia.Ili wale wanaolima kwa kutegemea mvua wakivuna na mazao yangu ndo yanakaribia kukomaa.na wale wa kumwagilia ambao wanaanzaga kupanda mvua zinapokwisha wao wakipanda mimi nakuwa niko karibu na mavuno hivo sokon tunakua wachache.pia huo ushauri niliupata toka kwa KILIMO MAARIFA.TAJIRI(namshukuru) kama sikosei.
Asikwambie mtu yale mahesabu na motisha zinazowekwa hapa ni tofauti na ukiingia shamba.tegemea kilimo kitakua na gharama zaid ya unavofikiri.

Kwa kuwa ni kilimo cha kumwagilia nikalima karibu na mto.Kwa bahati mbaya mvua za juzi zilikuwa kubwa mpaka maj yakajaa mto na kutoka nje kuingia mashamban na kuondoka na miche yote.

KILIMO KINA CHANGAMOTO SANA NA CHANGAMOTO ZAKE NDO HIZI ILA SIJAKATA TAMAA..
Nina nia ya kurudia.Gharama zilizopotea ni LAKI 9 NA 40.

sasa naomba ushauri je
Ni sahihi nikipanda mbegu upya kwa kipindi hiki ama nisubiri mpaka mvua zikome kabisa?

Mwanzo nilinunua mbegu za Balton Tanzani nilipanda 3 kila shimo na ziliota kwa 90%.sasa hivi sasa mfuko hauko vyema naweza kutumia mbegu zilizokusanywa kienyej?

Ushauri wowote wenye maslai napokea
 
Pole. Mi nililima eka mbili za nyanya na sasa yote iko mahututi kwa mvua na maji yanayotuama mda wote hayakauki.
 
Pole Ila laki 9 na 40 ni hela ndogo ndugu, ulifanya busara kwa kuanza na ekari chache. Endelea kupambana usikate tamaa, next time utafika hadi stage ya miche kukua halafu utapambana na changamoto ya wadudu, kuna Changamoto ya kupata matikiti machache kuliko ulivyo tegemea na mwisho kuna changamoto ya soko.

Tegemea hayo yote
 
Kilimo cha kisasa kina changamoto zake. Tusikate tamaa.
Nimeandaa kitalu cha nyanya. Nategea kupandikiza mwishoni mwa May.
Mungu anijalie mafanikio nipate mazao mengi na bora.
 
Pole Ila laki 9 na 40 ni hela ndogo ndugu, ulifanya busara kwa kuanza na ekari chache. Endelea kupambana usikate tamaa, next time utafika hadi stage ya miche kukua halafu utapambana na changamoto ya wadudu, kuna Changamoto ya kupata matikiti machache kuliko ulivyo tegemea na mwisho kuna changamoto ya soko.

Tegemea hayo yote

Hongera kwa kuthubutu,usikate tamaa.Kumbuka" the higher the risk the higher the profit" hakuna kazi yoyote duniai inayolipa isiyo na changamoto.Rudia zao hilohilo mahali hapo hapo kwa kuepuka/kupunguza ukubwa wa yaliyotokea.

Wachache sana wataiga kwa kuogopa hasara utatawala soko.Hongera
 
Pole sana but usikate tamaa ,hapo jifunze kuulizia historia ya mahala mwanzo . Rudia tikiti but usitumie Mbegu ambayo sio bora itakutesa kwa kukupa mavuno machache ,utapiga daw nyingi zaidi na haitokulipa vyema . Bora upate mbegu bora upunguze eneo kama mfuko pia hautoshi anza na mazao nafuu kama mahindi ndio uyalime msimu huu. Ahsante sana
 
Usikate tamaa. Suburi mvua zikate kabisa ; piga tuta, panda tikiti tena.
 
Pole Ila laki 9 na 40 ni hela ndogo ndugu, ulifanya busara kwa kuanza na ekari chache. Endelea kupambana usikate tamaa, next time utafika hadi stage ya miche kukua halafu utapambana na changamoto ya wadudu, kuna Changamoto ya kupata matikiti machache kuliko ulivyo tegemea na mwisho kuna changamoto ya soko.

Tegemea hayo yote
Kiukwel laki 9 ni ndogo ila kwa usawa huu wa sizonje hali ngumu sana.thanks umenipa moyo
Kilimo cha kisasa kina changamoto zake. Tusikate tamaa.
Nimeandaa kitalu cha nyanya. Nategea kupandikiza mwishoni mwa May.
Mungu anijalie mafanikio nipate mazao mengi na bora.
Mkuu kukataa tamaa ni kosa kubwa sana kutoka kwenye katiba ya wataftaji.hukumu yake nikuwa maskini na tegemezi daima
Hongera kwa kuthubutu,usikate tamaa.Kumbuka" the higher the risk the higher the profit" hakuna kazi yoyote duniai inayolipa isiyo na changamoto.Rudia zao hilohilo mahali hapo hapo kwa kuepuka/kupunguza ukubwa wa yaliyotokea.

Wachache sana wataiga kwa kuogopa hasara utatawala soko.Hongera
Nafarijika sana mkuu
Pole sana but usikate tamaa ,hapo jifunze kuulizia historia ya mahala mwanzo . Rudia tikiti but usitumie Mbegu ambayo sio bora itakutesa kwa kukupa mavuno machache ,utapiga daw nyingi zaidi na haitokulipa vyema . Bora upate mbegu bora upunguze eneo kama mfuko pia hautoshi anza na mazao nafuu kama mahindi ndio uyalime msimu huu. Ahsante sana
Naufanyia kaz mkuu ushauri wako thabiti.thanks
pole sana mkuu.
ndio kilimo......
Thanks ndugu
 
Habari za mida hii?
Kama kichwa cha habar kinavojieleza.
Kabla ya kuomba ushauri wacha nitoe habar kamili.

Nilifanya uchunguzi mfupi na kugundua Mkoa wa Simiyu Wilaya ya Bariadi iko na wakulima wachache sana wa kilimo cha umwagiliaji hasa kwenye kilimo cha mboga mboga na matunda.Basi nikacheki nini kinaweza kulipa katika kilimo hicho cha umwagiliaji.kwa ushauri wa watu wa karibu tukaona tikiti maji ndo linalipa.
Kwa target ya haraka ni kulima kipindi cha mwezi wa tano kwenda wa sita ambapo mvua ndo zinaishia.Ili wale wanaolima kwa kutegemea mvua wakivuna na mazao yangu ndo yanakaribia kukomaa.na wale wa kumwagilia ambao wanaanzaga kupanda mvua zinapokwisha wao wakipanda mimi nakuwa niko karibu na mavuno hivo sokon tunakua wachache.pia huo ushauri niliupata toka kwa KILIMO MAARIFA.TAJIRI(namshukuru) kama sikosei.
Asikwambie mtu yale mahesabu na motisha zinazowekwa hapa ni tofauti na ukiingia shamba.tegemea kilimo kitakua na gharama zaid ya unavofikiri.

Kwa kuwa ni kilimo cha kumwagilia nikalima karibu na mto.Kwa bahati mbaya mvua za juzi zilikuwa kubwa mpaka maj yakajaa mto na kutoka nje kuingia mashamban na kuondoka na miche yote.

KILIMO KINA CHANGAMOTO SANA NA CHANGAMOTO ZAKE NDO HIZI ILA SIJAKATA TAMAA..
Nina nia ya kurudia.Gharama zilizopotea ni LAKI 9 NA 40.

sasa naomba ushauri je
Ni sahihi nikipanda mbegu upya kwa kipindi hiki ama nisubiri mpaka mvua zikome kabisa?

Mwanzo nilinunua mbegu za Balton Tanzani nilipanda 3 kila shimo na ziliota kwa 90%.sasa hivi sasa mfuko hauko vyema naweza kutumia mbegu zilizokusanywa kienyej?

Ushauri wowote wenye maslai napokea
mkuu km hutojali naomba mchanganuo wa hiyo laki 9 ilikuwa ni nini na nn ?

af nna rafik fb anatumia jina hili,ni ww au
 
mkuu km hutojali naomba mchanganuo wa hiyo laki 9 ilikuwa ni nini na nn ?

af nna rafik fb anatumia jina hili,ni ww au
Shamba 100000
Mbegu 200000
Samadi 168000
Kulima 30000
Mashimo 30000
Kuchanganya samadi 30000
Kupanda 30000
Booster na madawa 200000
Tela repair 60000
Kumwagilia 50000
Nauli kutoka dar simiyu 45000
Fb natumia majina mengine kabisa
 
Shamba 100000
Mbegu 200000
Samadi 168000
Kulima 30000
Mashimo 30000
Kuchanganya samadi 30000
Kupanda 30000
Booster na madawa 200000
Tela repair 60000
Kumwagilia 50000
Nauli kutoka dar simiyu 45000
Fb natumia majina mengine kabisa
nimekupata vyema ninja,shukrani.
 
Pole Ila laki 9 na 40 ni hela ndogo ndugu, ulifanya busara kwa kuanza na ekari chache. Endelea kupambana usikate tamaa, next time utafika hadi stage ya miche kukua halafu utapambana na changamoto ya wadudu, kuna Changamoto ya kupata matikiti machache kuliko ulivyo tegemea na mwisho kuna changamoto ya soko.

Tegemea hayo yote
Mkuu nimeukubali sana ushauri wako, uko straight sana.

Bila kusahau wezi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom