Ndugu habari zenu,
Jamaa yangu wa karibu amepatwa na mkasa huu; nyumbani kwake anaishi yeye, mke, watoto na ndugu wa mke wake jinsia ya kike.
Siku moja alienda safari, kabla ya kurudi alitaka kushonea watoto sare ya kanisani, akampigia mkewe kumuulizia juu ya rangi ya sare, simu ya mkewe ikawa inatumika hivyo akaamua kumpigia yule binti ambaye ni ndugu wa mkewe wanaeishi naye pale nyumbani.
Baada ya kupata rangi ya sare, jamaa alishona zile nguo akaenda nazo nyumbani, alipofika mkewe akamwambia rangi ya nguo siyo inayohitajika kanisani na akahoji ni nani aliyetoa taarifa juu ya rangi ya sare iliyoshonwa, jamaa akasema kuwa ni yule binti, ndugu wa huyo mwanamke.
Mwanamke akahoji tena ni kwanini apigiwe simu huyo binti badala ya yeye(mkewe na jamaa), jamaa akaeleza kuwa alimpigia ila namba yake ikawa inatumika na kwa vile alikuwa na haraka basi akaamua kumpigia huyo binti.
Kuanzia hapo hakuna amani, yule binti(kwa sasa yuko safari)alipigiwa simu na ndugu yake na kuelezwa kuwa hapaswi kurudi pale nyumbani kwa madai kuwa anatembea na jamaa.
Kwa ujumla jamaa anashindwa afanye nini kwa kuwa anasingiziwa kosa ambalo hahusiki kwa namna yoyote ile na anamchukulia yule binti kama sehemu ya familia yake, hivyo anaomba ushauri ili kuondokana na mkasa huu.
Jamaa yangu wa karibu amepatwa na mkasa huu; nyumbani kwake anaishi yeye, mke, watoto na ndugu wa mke wake jinsia ya kike.
Siku moja alienda safari, kabla ya kurudi alitaka kushonea watoto sare ya kanisani, akampigia mkewe kumuulizia juu ya rangi ya sare, simu ya mkewe ikawa inatumika hivyo akaamua kumpigia yule binti ambaye ni ndugu wa mkewe wanaeishi naye pale nyumbani.
Baada ya kupata rangi ya sare, jamaa alishona zile nguo akaenda nazo nyumbani, alipofika mkewe akamwambia rangi ya nguo siyo inayohitajika kanisani na akahoji ni nani aliyetoa taarifa juu ya rangi ya sare iliyoshonwa, jamaa akasema kuwa ni yule binti, ndugu wa huyo mwanamke.
Mwanamke akahoji tena ni kwanini apigiwe simu huyo binti badala ya yeye(mkewe na jamaa), jamaa akaeleza kuwa alimpigia ila namba yake ikawa inatumika na kwa vile alikuwa na haraka basi akaamua kumpigia huyo binti.
Kuanzia hapo hakuna amani, yule binti(kwa sasa yuko safari)alipigiwa simu na ndugu yake na kuelezwa kuwa hapaswi kurudi pale nyumbani kwa madai kuwa anatembea na jamaa.
Kwa ujumla jamaa anashindwa afanye nini kwa kuwa anasingiziwa kosa ambalo hahusiki kwa namna yoyote ile na anamchukulia yule binti kama sehemu ya familia yake, hivyo anaomba ushauri ili kuondokana na mkasa huu.