Ushauri muhimu na wa bure kwa CHADEMA kuhusu muafaka utakaowaunganisha Dr Slaa na Lowassa

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Hakuna anayepinga Dr. Slaa ni nguzo muhimu kwa CHADEMA, amefanya kazi kubwa sana hadi amekifikisha chama kilipo sasa, ambapo ndipo Lowassa alipokikuta na kuchagua kujiunga nacho badala ya vyama vingine.

Na pia, hakuna anaepinga kwamba Lowassa ni kete muhimu kwa CHADEMA kupiga hatua kubwa kutoka ilipo sasa, na huenda hata kuipa historia ya kushika serikali.

Kwa hiyo jambo la kwanza ni kwa CHADEMA kukubali kwamba wote Dr. Slaa na Lowassa ni watu muhimu sana katika kipindi hiki muhimu cha mabadiliko ya sura ya siasa Tanzania.

Hivyo basi, ili CHADEMA lazima iwe na suluhisho linalokubalika kwa Dr Slaa na Lowassa, linalowaenzi wote wawili, na huu hapa ni ushauri wangu;

Mwacheni Lowassa agombee uraisi, na Dr. Slaa ampe support yote. Ila sasa, Lowassa akifanikiwa kushinda uraisi, basi aongoze Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano tu. Hiyo inatosha kama heshima ya kuiweka CHADEMA katika kilele kipya cha siasa Tanzania.

Baada ya miaka mitano, Lowassa apumzike na kujiunga na Mtei kuwa walezi wa CHADEMA. Hapo ndipo Dr. Slaa ateuliwe kuwa mgombea mpya wa uraisi wa CHADEMA ifikapo 2020.

Ila CHADEMA wanapaswa kuwa waangalifu na suala la UKAWA. Inawezekana kabisa washiriki wengine wa UKAWA wakadai kwamba ifikapo 2020 itakuwa zamu yao kutoa mgombea uraisi. Hili litaleta vurugu, na dawa yake ni vyama vinaounda UKAWA kuungana rasmi na kuwa chama kimoja chenye nguvu.
 
Hakuna anayepinga Dr. Slaa ni nguzo muhimu kwa CHADEMA, amefanya kazi kubwa sana hadi amekifikisha chama kilipo sasa, ambapo ndipo Lowassa alipokikuta na kuchagua kujiunga nacho badala ya vyama vingine.

Na pia, hakuna anaepinga kwamba Lowassa ni kete muhimu kwa CHADEMA kupiga hatua kubwa kutoka ilipo sasa, na huenda hata kuipa historia ya kushika serikali.

Kwa hiyo jambo la kwanza ni kwa CHADEMA kukubali kwamba wote Dr. Slaa na Lowassa ni watu muhimu sana katika kipindi hiki muhimu cha mabadiliko ya sura ya siasa Tanzania.

Hivyo basi, ili CHADEMA lazima iwe na suluhisho linalokubalika kwa Dr Slaa na Lowassa, linalowaenzi wote wawili, na huu hapa ni ushauri wangu;

Mwacheni Lowassa agombee uraisi, na Dr. Slaa ampe support yote. Ila sasa, Lowassa akifanikiwa kushinda uraisi, basi aongoze Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano tu. Hiyo inatosha kama heshima ya kuiweka CHADEMA katika kilele kipya cha siasa Tanzania.

Baada ya miaka mitano, Lowassa apumzike na kujiunga na Mtei kuwa walezi wa CHADEMA. Hapo ndipo Dr. Slaa ateuliwe kuwa mgombea mpya wa uraisi wa CHADEMA ifikapo 2020.

Ila CHADEMA wanapaswa kuwa waangalifu na suala la UKAWA. Inawezekana kabisa washiriki wengine wa UKAWA wakadai kwamba ifikapo 2020 itakuwa zamu yao kutoa mgombea uraisi. Hili litaleta vurugu, na dawa yake ni vyama vinaounda UKAWA kuungana rasmi na kuwa chama kimoja chenye nguvu.
Ndg yangu sehemu kubwa umenena vyema, muhimu tusisahau kuwa chadema imejengwa na baadhi ya watu wa ccm akiwemo Lowassa. Mimi na wewe tunaweza kumuona Lowassa mgeni leo chadema, lakini nakuhakikishia yawezekana kupokelewa kwake kumetokana na mchango wake mkubwa ndani ya chadema.

Mwisho nikutoe hofu, ni kwamba hesabu zimezingatiwa. Chadema kuna vichwa vyenye akili zenye Afya njema. Tulia uone, hapa tuna mambo mawili mojawapo litafanyika kwa ufasaha, Kama si mpango wa kuiua Ccm basi ni Chadema.
 
Ndg yangu sehemu kubwa umenena vyema, muhimu tusisahau kuwa chadema imejengwa na baadhi ya watu wa ccm akiwemo Lowassa. Mimi na wewe tunaweza kumuona Lowassa mgeni leo chadema, lakini nakuhakikishia yawezekana kupokelewa kwake kumetokana na mchango wake mkubwa ndani ya chadema.

Mwisho nikutoe hofu, ni kwamba hesabu zimezingatiwa. Chadema kuna vichwa vyenye akili zenye Afya njema. Tulia uone, hapa tuna mambo mawili mojawapo litafanyika kwa ufasaha, Kama si mpango wa kuiua Ccm basi ni Chadema.

Nimekusikia Mkuu. Kwangu mie lolote litakaloleta kasi mpya ya kuwajibika kwa vyama vya siasa ili kutokeza chachu mpya ya maendeleo ya Tanzania, kwangu hilo linakubalika. Ninachoona kwa hatua ya Lowassa ni kichechocheo cha kasi hiyo. Ni vema CHADEMA wakatafakari ni zipi weaknesses zinazotokana na suala zima la Lowassa kujiunga na Chadema, na kuzigeuza hizo weaknesses kuwa strength katika namna ambayo inakubalika kwa kila kiongozi na wanachama karibu wote, na inayoleta sura mpya ya mpambano kati ya CCM na vyama vingine, au chama kingine, ikiwa UKAWA kita-ivolve kuwa chama.
 
Hatumtaki Slaa kwa tabia zake za kususasusa kama mtoto wa mwisho, kama anaona ameonewa kwa kunyimwa nafasi ya kugombea urais na aende, vyama vipo vingi siyo lazima hapa CDM tu hapa tunamtaka Lowasa kwani tumeshakula mahela yake!
 
Unakosea sana kudhani Dr Slaa anahitaji cheo ili aebdelee kuongoza Chadema, Unakosea sana!!

BACK TANGANYIKA
 
Kama ni fedha za lowasa mnataka huo ni utapeli.chadema tuko kimaadili zaidi na hatutaki uchafu wa ccm uendelee kuwepo ikulu. Hata hivyo tunajua kuwa lowasa hawezi kuruhusiwa kuingia ikulu hivyo baada ya uchaguzi atarudi Monduli na kutuachia chama chetu. Ila hao waliomleta ni lazima tuwawajibishe kwani ni mafisadi kama walioko ccm.
 
CHADEMA kunagawiana majukumu siyo vyeo wala ulaji. Fikra za namna hii zitaturudisha nyuma na kuleta malumbano yasiyo na tija.
 
Daima nitakua mwanachama wa chadema na kamwe sitajaribu kuwa mfuasi wa mtu ndani ya chama m4c daima.
 
CONFIRMED: Dkt. Slaa bado yupo Chadema na anaendelea na majukumu yake kama kawaida,kwani muda wa kuchukua fomu hadi unaisha na kuongezwa hakuwahi kwenda kuchukua fomu na wala hakuwahi kuzuiwa kuchukua fomu kwani zinatolewa ofisini kwake.
 
Unakosea sana kudhani Dr Slaa anahitaji cheo ili aebdelee kuongoza Chadema, Unakosea sana!!

BACK TANGANYIKA

Hakuna sehemu niliyosema hivyo. Dr. Slaa hajawa disappointed na Chadema kuwa na mgombea uraisi mbadala, amekuwa disappointed na huyo mbadala kuwa ni Lowassa. Ninachosema ni kwamba aangalie big picture, kwamba bado unaweza kumtumia Lowassa, pamoja na mapungufu yake, kufanikisha long term objectives za Chadema
 
Hatumtaki Slaa kwa tabia zake za kususasusa kama mtoto wa mwisho, kama anaona ameonewa kwa kunyimwa nafasi ya kugombea urais na aende, vyama vipo vingi siyo lazima hapa CDM tu hapa tunamtaka Lowasa kwani tumeshakula mahela yake!

Mtakuwa mnakosea sana kudhani Dr. Slaa anachotaka ni yeye kuwa mgombea Uraisi. Unadhani Dr. Slaa angehuzunika ikiwa Mbowe ndiye angekuwa mgombea uraisi badala yake? Jibu ni hapana. Kwa hiyo kudhani kwamba Dr. Slaa anasikitika kwa ajili ya kuwa na mgombea uraisi Lowassa ni sawa na kumtukana Dr. Slaa, kutomtendea haki kwa hali ya juu kabisa.
 
CHADEMA kunagawiana majukumu siyo vyeo wala ulaji. Fikra za namna hii zitaturudisha nyuma na kuleta malumbano yasiyo na tija.

Huwezi kutofautisha vyeo na majukumu. Cheo kinakupa jukumu. Wasiwasi wa Dr. Slaa ni kwamba Lowassa kama raisi, ataweza kutekeleza jukumu la kile ambacho Chadema imepigania siku zote, au analeta mentality ya CCM ndani ya Chadema?

Niliposema Chadema wamruhusi Lowassa kuwa Raisi kwa miaka mitano tu, lengo langu sio kugawana uraisi kati ya Lowassa na Dr. Slaa, bali kuhakiisha kwamba Dr. Slaa bado atakuwa na nafasi ya kutekeleza long term objectives za Chadema, hata kama itabidi kusubiri miaka mitano ijayo.

Suala pia ni kwamba what is the worst damage Lowassa anaweza kusababisha katika miaka mitano yake ya Uraisi kupitia Chadema? Huenda hiyo five year worst case damage scenario ingefanywa na Magufuri kama Lowassa asingekuja Chadema. Hicho ndicho ambacho namhitaji Dr. Slaa ku-compromise.

Kimsingi, uraisi wa Lowassa kupitia Chadema Dr. Slaa anapaswa kuuona kama maumivu ya kutahiriwa ukubwani; ni maumivu makali lakini yakiisha hayarudi tena, na raha na faida za kutahiriwa zitakuwa ni za kudumu. Kwa hiyo akubali tu.

 
Back
Top Bottom