Ushauri: Mchawi mpe mwanao akulelee, Mh. Raisi mpe majukumu Tundu Lissu

Tanzania Njema Yaja

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
3,042
2,414
Wakuu, napenda kutoa ushauri tu....

Kwa kuwa TL amekuwa mstari wa mbele kupigania haki ya watz kunufaika na rasilimali zetu hasa madini. Nakumbuka kumuona TL kwenye TV miaka ya zamani akitokwa povu la uzalendo hasa kuhusu madini na kwamba tunaibiwa...

Na kwa hivi karibuni, TL amekuwa akitoa ushauri wa nini kifanyike ili sisi kama taifa tuweze nufaika na hali tuliyopo kwa sasa kwa mtego tulio utega wenyewe.

Kwa kuwa TL ni mwanasheria mbobezi na suala la madini analijua vizuri, na kwa kuwa Tz ni yetu sote na kwa kuwa maoni ya TL yanaonekana kama wana CCM hawayapendi, wakati wote na hasa kwa kipindi hiki cha Makinikia, ili kubalance kamati ya majadiliano (negotiation team) na hawa wawekezaji, nashauri TL awe katika wajumbe wa kamati hiyo. Ukweli ni kwamba aliyo kuwa anayapigia kelele TL miaka ile ndo yanayo onekana kwa sasa.... tumpe nafasi atatusaidia..
 
Atajivunjia heshima TL kufanya kazi na hao hayo mambo yalifanywa makusudi na sizonje mda wote alikuwepo kwny baraza la mawaziri
 
CCM bila kuondoka hata malaika akipewa uongozi ndani ya CCM atageuka kuwa mjuzi.
 
Mkuu kama povu la Palamagamba Kabudi leo Ikulu nimelishamgaa.....
Professor leo ameonyesha kazi hizi zilivyokuwa ngumu. Ameungana na bosi wake kuwatakia wazee mapumziko memo na wasibugudhiwe. No wonder baba yule ataendelea kuitwa fisadi wakati mahakama ya mafisadi hayana hata kesi moja. Subiri 2020 ilikaribia uone watakavyo mtukana-amekuwa mtaji wao wa kisiasa. Kwa mwendo huu professor basi tena.
 
Professor leo ameonyesha kazi hizi zilivyokuwa ngumu. Ameungana na bosi wake kuwatakia wazee mapumziko memo na wasibugudhiwe. No wonder baba yule ataendelea kuitwa fisadi wakati mahakama ya mafisadi hayana hata kesi moja. Subiri 2020 ilikaribia uone watakavyo mtukana-amekuwa mtaji wao wa kisiasa. Kwa mwendo huu professor basi tena.
Propesa....
 
Hii nchi ni ajabu sana na hata watu wake ni wa ajabu mno! Hili neno uzalendo ni bora lingesomeka hivi "uza land" ili liakisi hiki kinachoendelea nchini kwa sasa.
Wale wachache wenye upeo na utashi wa kuyaona yanayoendelea kuwakwaza walio wengi kiuchumi wanabezwa na kudhihakiwa kana kwamba wamejipaka kinyeasi! Hawatumiki ipasavyo katika kutetea uchumi na maendeleo ya nchi kwa sababu tu ya itikadi zao kutofautiana na au atawafunika wakubwa!
Lissu usife moyo na usikate tamaa kwani historia itakuandika vema kuliko na hata hao wanakukiri kimoyomoyo kuwa unausema ukweli kwa uzalendo wa kweli!
Umeitendea haki taaluma yako na akili yako kwa faida ya wana wa nchi hii japo kule jimboni kwako wanakunyima hata mgao wa maji safi ili kukuchonganisha na nduguzo wa Ikungi. Waambie hayo maji wanayoyoyapata kwa njia za asili ndio yaliyokukuza na kuusafisha ubongo wako hadi ukawa na akili kuwashinda wao! Mungu ataleta neema kwa kuijaza mito na mabwawa ya Ikungi maji ya kutosha miaka yote.
 
Naunga mkono hojaa..
Vita ni yetu sote.hasa wale walioianza zamanii.bila kuwaacha washangiliajii
 
Hii nchi ni ajabu sana na hata watu wake ni wa ajabu mno! Hili neno uzalendo ni bora lingesomeka hivi "uza land" ili liakisi hiki kinachoendelea nchini kwa sasa.
Wale wachache wenye upeo na utashi wa kuyaona yanayoendelea kuwakwaza walio wengi kiuchumi wanabezwa na kudhihakiwa kana kwamba wamejipaka kinyeasi! Hawatumiki ipasavyo katika kutetea uchumi na maendeleo ya nchi kwa sababu tu ya itikadi zao kutofautiana na au atawafunika wakubwa!
Lissu usife moyo na usikate tamaa kwani historia itakuandika vema kuliko na hata hao wanakukiri kimoyomoyo kuwa unausema ukweli kwa uzalendo wa kweli!
Umeitendea haki taaluma yako na akili yako kwa faida ya wana wa nchi hii japo kule jimboni kwako wanakunyima hata mgao wa maji safi ili kukuchonganisha na nduguzo wa Ikungi. Waambie hayo maji wanayoyoyapata kwa njia za asili ndio yaliyokukuza na kuusafisha ubongo wako hadi ukawa na akili kuwashinda wao! Mungu ataleta neema kwa kuijaza mito na mabwawa ya Ikungi maji ya kutosha miaka yote.
Maneno ya hekima sana haya mkuu...
 
Naunga mkono hojaa..
Vita ni yetu sote.hasa wale walioianza zamanii.bila kuwaacha washangiliajii
Akubali kuwa mkapa na kikwete watakuwa included kwenye kash kash za kuisaka Noah yetu!!!
 
Wakuu, napenda kutoa ushauri tu....

Kwa kuwa TL amekuwa mstari wa mbele kupigania haki ya watz kunufaika na rasilimali zetu hasa madini. Nakumbuka kumuona TL kwenye TV miaka ya zamani akitokwa povu la uzalendo hasa kuhusu madini na kwamba tunaibiwa...

Na kwa hivi karibuni, TL amekuwa akitoa ushauri wa nini kifanyike ili sisi kama taifa tuweze nufaika na hali tuliyopo kwa sasa kwa mtego tulio utega wenyewe.

Kwa kuwa TL ni mwanasheria mbobezi na suala la madini analijua vizuri, na kwa kuwa Tz ni yetu sote na kwa kuwa maoni ya TL yanaonekana kama wana CCM hawayapendi, wakati wote na hasa kwa kipindi hiki cha Makinikia, ili kubalance kamati ya majadiliano (negotiation team) na hawa wawekezaji, nashauri TL awe katika wajumbe wa kamati hiyo. Ukweli ni kwamba aliyo kuwa anayapigia kelele TL miaka ile ndo yanayo onekana kwa sasa.... tumpe nafasi atatusaidia..

Busara ilikuwa kuwaingiza hata kwenye kamati zote... leo tungekuwa tunaimba wimbo mmoja... hili halikutakiwa kuwa swala la kisiasa, tatizo letu hatuwezi kutofautisha siasa na mambo ya msingi yenye maslahi ya taifa, tunaishia kupigana vijembe.
 
Busara ilikuwa kuwaingiza hata kwenye kamati zote... leo tungekuwa tunaimba wimbo mmoja... hili halikutakiwa kuwa swala la kisiasa, tatizo letu hatuwezi kutofautisha siasa na mambo ya msingi yenye maslahi ya taifa, tunaishia kupigana vijembe.
Maneno kuntu haya.. karne hii bado wapinzani wanaonekana ni maadui... sielewi kwa kweli...
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom