Gajungi
JF-Expert Member
- Sep 4, 2011
- 257
- 83
Habari wanajf. Mimi ni kijana wa kiume. Nathubutu kusema nina mpenzi Tanzania-Dar na mimi nipo ughaibuni kwa masomo tangu october 2009 hadi 2013. Huyu mpenzi wangu anasoma Diploma BA Alinitaarifu kufiwa na baba yake. Pia aliniambia kapoteza simu, nilipomuuliza how akanimbia kwa utani we elewa tu nimepoteza simu, nikawa nampigia kupitia simu ya mama yake. Baada ya kuchukua muda mrefu bila simu nilimwambia kaka yangu ampe pesa anunue simu lakini aliniambia kuwa alinunua vitabu na si simu,nikaendelea kumpigia kupitia simu ya mama yake. Kuna muda aliniambia kuwa alipewa ada na kwa bahati mbaya aliipoteza ,hivyo tayari alishanitumia maombi ya ada laki 2,ingawa nilifanikiwa kumwelekeza kuwa kwa kipindi hiki nisingeweza kumsaidia mpaka december. Hivi karibuni nilimpigia mama yake na kunieleza kuwa tayari alishakuwa na simu[kwa nini asingeweza walau kunitumia sms kuwa sasa ana simu?] na nikampigia na kweli niliongea naye akanieleza kuwa sasa anatafuta hostel{hivyo anahitaji pesa toka kwangu}. Sasa kaka yangu aliyemtumia pesa alinishauri niachane naye kwa sababu anapenda sana pesa{ni nusu mchaga) kiasi kwamba hata hakuweza kutoa shukrani kwake.Niliwahi kumpa kazi ndogo ya kunitafutia information pale benki za Dar lakini hakunijibu chochote. Mpaka sasa nafikiri kumpigia simu na kumhoji maswali ambayo yatamwonesha kweli nipo mguu mmoja nje mwingine ndani. Yeye ni mzuri na anafikiri kuwa nimempenda kupindikua labda pia kinachomfanya anitie mashaka juu ya upendo wake kwangu. Ndugu zangu naombeni mnieleze iwapo kwa maelezo haya ninapendwa? au inayopendwa ni pesa yangu nilyonayo? Mimi sioni any kind of care hapo.Kwa hiyo nataka baada ya hapo nitafute kimwana huku na nianze kuishi maisha.