Roller coaster
Senior Member
- Jan 5, 2015
- 194
- 129
Analindwa na hiriziNajua unapenda sana Kushughulika na kuhakikisha kuwa Jambo fulani linatendeka na linaenda unavyotaka Wewe ila kuna maeneo mengine unatakiwa upime au ujipime Kwanza hasa ukizingatia Usalama wako na jinsi Jamii Kubwa ya Watu hasa ' Maadui ' zako ulionao hapa Mkoani Dar es Salaam.
Binafsi nilishangaa sana ile Jana tena ukiwa barabarani na kuna Watu wengi wa kila aina ' ukijiachia ' kwa kutoka katika Gari yako na Kujumuika nao huku ukizunguka huku na kule pasipo na hata Wewe kuwa na jicho la pili kwa ' Usalama ' wako.
Najua unalindwa tena pengine kuliko hata wanavyolindwa ' VIP's ' wengine nchini ila binafsi nadhani kwa hali iliyopo na hasa ' Chuki ' za Watu dhidi yako ( nikimaanisha Maadui ) zako uliowatengeneza hukupashwa ' Kujiachia ' vile kwani lolote lingeweza kutokea Kwako na pengine leo tungekuwa na habari nyingine mbaya.
Mpaka sasa nawaza RC Makonda unajiamini vipi hadi unapenda ' Kujichanganya ' na Watu tena wale ' Changanyikeni Clan ' ambamo ndani yao humo kuna ambao wanakupenda na wasiokupenda pengine kama nia mbaya ingekuwepo dhidi yako jana basi ingekuwa rahisi Kwao ' Kutekeleza ' jambo lao.
Ushauri wangu Kwako Siku zingine kabla ya kwenda mahala hebu jaribu kupima ' Upepo ' Kwanza na ' Kutafakari ' kwa marefu na mapana hasa hasa ukizingatia suala zima la ' Usalama ' wako. Ila ningekuwa ni Mimi GENTAMYCINE jana ile nipo nawe kama sehemu ya ' Ulinzi ' wako kamwe nisingekuruhusu uwe unatokatoka vile katika Gari yako na kuja ' Kujichanganya ' na Watu ambao Kwanza huwajui vyema, akili zao wengine wanazijua wenyewe na wenye kuwa tayari pia kufanya lolote na kuja ' Kujutia ' baadae huku pengine Wewe ukiwa ' Mwaisela ' au ' ICU ' au umeshaungana na ' Mtani ' wangu katika ' Identity ' mpya ya Marehemu fulani.
Acha kujiamini sana na kuwa makini tafadhali. Yangu ni haya tu kwa leo na ukiona nakuambia hivi jua nakupenda na nakutakia maisha marefu na mema pia. Bado wale ' Maadui ' zako hawajalala usingizi na pia huwezi jua sasa wanajipangaje dhidi yako hivyo nawe pia yakupasha muda mwingi kuwa makini na ' Kujilinda ' huku pia ukipunguza sana kupenda ' Kuonekana ' mbele mbele. Kwani ile jana ambapo nawe ulikuwa ' Msafarani ' ungekuwa tu unatoa ' Maelekezo ' wa Watendaji wako hasa wa Kiusalama / Kiitifaki waliokuwepo pale au uliokuwa nao wasingefanya kile ulichokuwa unataka Kifanyike?
Yafanyie Kazi haya maelezo yangu ila ukiona hayakufai basi niachie tu mwenyewe.
Nawasilisha.
Ametumwa huyu jamaa ee...anatuletea Uzi was ajabuajabu hapa...kwani hizi taasisi zilikuwa hazisaidii hapo awali kabla ya Rc....Hongera kwa kujaliwa ujinga na upumbavu kwa wakati mmoja.
Kuna watu ni maarufu kwa kupinga kila kitu ...!! yaani 'pinga pinga' wana mahusiano na mtaa wa ufipa pale k'ndoni ngoja wakuibukie.