Ushauri kwa Wizara ya Elimu: Kuwe na sare za walimu

getrusa

JF-Expert Member
Aug 16, 2013
2,150
1,812
Salaam,wana Jamvi!

Ninatoa wito kwa Wizara ya Elimu kutambulisha sare rasmi kwa walimu wa shule za msingi na Sekondari hapa Nchini.

Kutokana na utafiti usio rasmi niliofanya kwa shule nyingi hapa kwetu Tanzania walimu 8 kati ya 10 walipenda kuwe na vazi rasmi la kazi kwa sababu zifuatazo:

1. Vazi rasmi linapunguza gharama za kununua mavazi mengi, mfano kwa mwalimu wa kike angetamani kuwa nadhifu muda wote awapo kazini, ili kuepusha fedheha ya kurudia mara kwa mara nguo fulani analazimika kuwa na nguo nyingi, katika hali hiyo ina maana pia bajeti yake ya mavazi inaongezeka.

2. Kuweka hali ya Usawa kwa walimu wote izingatiwe kuwa watoto ni wepesi kusoma muonekano wa mavazi ya mwalimu ikiwa na maana mwalimu anayetoka katika familia yenye kipato mavazi yake yanaweza kuwa na thamani kubwa kuliko wenzie.

Hali hii inaondoa usawa wa kifikra kwa walimu na bila shaka unaondoa namna fulani ya kujiamini kisaikolojia hasa kwa walimu wa kike.

3. Kutunza nidhamu na haiba kunapokuwa na vazi maalumu au sare ni rahisi kutunza haiba na muonekano wa mwalimu ambapo ni tofauti na sasa ambapo kila mwalimu huja na vazi ambalo yeye anaona lina mpendeza na limemkaaa, hapa inategemea sana na hekima ya mwalimu wapo wanaovaa nguo ambazo haziko sawa kwa maadili ya watoto japo sio wote.

4. Kama serikali ikiwa na mfumo rasmi hili ni soko tayari kwa viwanda vyetu vya ndani ambapo idadi ya walimu nchi nzima, wakiwa na sare kuna uhakika wa kuuza nguo zinazotengenezwa hapa hapa nchini kwetu.

Mwisho ipo mifano ya nchi ambazo walimu wana vazi lao rasmi mathalani ukitembelea karibu shule zote za serikali Zambia walimu wana vaa makoti Meupe kama yale ya madktari wawapo kazini.

Ama kule Zanzibar kuna shule ambazo wao tayari wana utaratibu wao wa sare za kazi.

Isisahaulike kuwa walimu hawa siku ya maadhimisho ya wafanyakazi wanavaa sare ama katika sherehe mbalimbali kuna sare zinavaliwa hivyo haiwezi kuwa ajabu wao kuwa na vazi ama sare yao maalum inayowatambulisha.

Nawasilisha natumai ushauri huu utazingatiwa karibuni kwa mjadala.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zipo sababu za msingi kabisa zilizo ondoa sare za walimu washuleni ikiwemo na swala la gharama maana anaye takiwa kugharimia sare ni mwajili sasa hebu piga hesabu ya walimu wote tanzania halafu uone serikali itagharamia kiasi gani kwa mwaka

Pia kutokana na kazi yao na aina ya watu wanao shughulika nao ndio maana sare iliondolewa.
 
Hakuna anayekukataza kuwa na mtazamo wako mimi nimetoa maelezo yangu na kile nilichokiona kwa shughuli na mtazamo wangu,
kwa kufanya hivyo kiwango na ubora wa elimu utaongezeka sio......wanafunzi hawatakaa chini tena...vitabu vitakua vingi na bora...kutakua na maabara zenye vifaaa......vyote hivyo havipo kwasababu walimu hawavai sare

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya ni mawazo dhaifu na finyu ya mtu mnyonge asiyejiamini hata kidogo.

Kwa nini umefikiria kazi ya wahudumu wa hoteli kama ya chini isiyopaswa kulinganishwa na kazi ya ualimu?

Hata kama kwenye jamii imedharaulika hivyo,je umeshindwa kufikiri watu kama askari jeshi,polisi,uhamiaji na magereza ambao wanavaa sare nadhifu na zinapendeza?

Basi tuendelee kuamini unavyofikiri(kizembe zembe),tuseme hao askari wanavaa sare kwa sababu kazi zao hazina heshima kama ya ualimu,je vipi kuhusu wauguzi?Au nao sio kazi muhimu?

Basi tuuchukue upuuzi wako kama ndio kweli,nakuuliza swali la mwisho,ukiambiwa leo uchague kazi kati ya ualimu na urubani utachagua ipi?Au ukapata ofa ya mwanao kusomeshwa kati ya ualimu na urubani ambao wanavaa sare kazini,utachagua ofa ipi?

Kama msimamo wako unaendelea kuwa huo mpaka hapa,sitashangaa mwanangu kwenda kusomea kutibu wagonjwa wa afya ya akili,maana wateja bado wapo wengi
Unaonekana umeshiba sana al kasusu mpaka unapata mawazo ya bure kama haya.
Unadhalilisha walimu ,umewachukulia poa sana wakati future ya taifa hili iko mikononi mwao.
Usiwachukulie walimu kama mawaiter aise

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umichukulia kwa mtazamo wa udharirishaji hiyo ni akili yako binafsi nimeongea kwa uzoefu na kile ninacho kiona katika maisha yangu ya kila siku.!
Hivyo usihukumu kwa upeo wa akili yako ukadhani akili yako inaona mbali kuliko wengine
Unaonekana umeshiba sana al kasusu mpaka unapata mawazo ya bure kama haya.
Unadhalilisha walimu ,umewachukulia poa sana wakati future ya taifa hili iko mikononi mwao.
Usiwachukulie walimu kama mawaiter aise

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu binafsi sikuwahi kuwa ufahamu wa hilo kuwa wizara ya Elimu walishawahi kuwa na Sare za walimu,! Pili kidogo ilinipitia mbali kama sare huwa kwa gharama ya muajiri.!

Japo kuna wakati niliambiwa na mhusika kuwa zile tshirt na kofia wanazivaa wakati wa maadhimisho ya mei mosi huwa wanakatwa kwenye mshahara wao! Hivyo wanaji gharamia.

Ukiangalia suala la sare linapunguza mambo mengi sana hasa kwa walimu wa kike.!

Japo ukiamua kulichulia katika namna hasi pia linaweza kuleta mantiki, nimeona faida za kuwa na sare katika Nchi kadhaa nilizo bahatika kutembelea

Hivyo bado naona likifanyiwa tathmini linaweza kuwa wazo sahihi.
Zipo sababu za msingi kabisa zilizo ondoa sare za walimu washuleni ikiwemo na swala la gharama maana anaye takiwa kugharimia sare ni mwajili sasa hebu piga hesabu ya walimu wote tanzania halafu uone serikali itagharamia kiasi gani kwa mwaka

Pia kutokana na kazi yao na aina ya watu wanao shughulika nao ndio maana sare iliondolewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika hili kusimangwa kwa mwalimu kuko wapi?
Hebu fikiri huyu mwalimu anapawa kuwa na nguo ngapi anazoziandaa kwa wiki ili avae aendapo kazini. Vip kwa mwezi atapaswa kuwa nguo ngapi ili asirudie rudie nguo anazo vaa?
Kumbuka wanafunzi ni tofauti sana watu wazima, kuna walimu wamepewa majina kutokana na nguo wanazova mara nyingi wawapo kazini.
"Nakumbuka hata sisi tuliwahi kuwa na mwalimu tulimwita "wakatrouser"! Sabbu alikuaa anarudia suruali ile mara nyingi, naona ni vema kama walimu wataondokana na hizi fedheha ndogo ndogo
Walimu ni sehemu ya watu wanao ongoza kwa kusimangwa kama daraja la chini


Ila mwalimu ni mhimu kuliko mnavyo mchukulia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom