Daniel Muhina
Member
- Jun 16, 2012
- 38
- 12
Nimekuwa msomaji mzuri wa Jamiiforums kwa muda mrefu kidogo kabla sijajiunga kwani ni memba kwenye makundi mengine humu mitandaoni kwa kipindi kirefu kidogo.
Sasa umefika wakati nami nimeona nijiunge rasmi, nimekuwa nikisoma malalamiko mengi leo dhidi ya Mh mwigulu kwa mchango wake alioutoa bungeni jioni, wengi wa wachangiaji wameonyesha kukerwa kwao na hoja zote na hasa kusema kuwa Mwigulu katoa lugha chafu, matusi na mengine mengi kibaya zaidi hata hao nao wamerudia kile kile walichokilalamikia.
Naomba nitoe ushauri mmoja kwakuwa Mwigulu anafanya kazi ya siasa na wote mlimvamia wenye hoja mbalimbali yaonekana pia mwafanya kazi za siasa naomba niwashauri kuwa Mwigulu kafanya kazi yake ya siasa na kautumia vema muda wake leo, sasa ni juu ya wanasiasa wengine na hasa wapinzani wa CCM wawasiliane na wabunge wao ili kabla ya bunge hili la bajeti kwisha waweze kutoa baadhi ya majibu ambayo mh Mwigulu ameyasema hasa ishu ya Gari la Mh Mbowe na mengineyo!
Vingineyo nitaamini kuwa Mwigulu kawashika pabaya leo!
Sasa umefika wakati nami nimeona nijiunge rasmi, nimekuwa nikisoma malalamiko mengi leo dhidi ya Mh mwigulu kwa mchango wake alioutoa bungeni jioni, wengi wa wachangiaji wameonyesha kukerwa kwao na hoja zote na hasa kusema kuwa Mwigulu katoa lugha chafu, matusi na mengine mengi kibaya zaidi hata hao nao wamerudia kile kile walichokilalamikia.
Naomba nitoe ushauri mmoja kwakuwa Mwigulu anafanya kazi ya siasa na wote mlimvamia wenye hoja mbalimbali yaonekana pia mwafanya kazi za siasa naomba niwashauri kuwa Mwigulu kafanya kazi yake ya siasa na kautumia vema muda wake leo, sasa ni juu ya wanasiasa wengine na hasa wapinzani wa CCM wawasiliane na wabunge wao ili kabla ya bunge hili la bajeti kwisha waweze kutoa baadhi ya majibu ambayo mh Mwigulu ameyasema hasa ishu ya Gari la Mh Mbowe na mengineyo!
Vingineyo nitaamini kuwa Mwigulu kawashika pabaya leo!