MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha, kumekuwa na mkwamo wa safari haswa kuanzia Korogwe Mjini ambapo leo 26/10/2019 barabara hiyo imefungwa na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wanaosafirisha huduma, bidhaa na watu.
Hii ni kutokana na kipande cha barabara ya Segera-Korogwe kuwa na maeneo matatu yaliyojaa maji ambayo ni Daraja la Kilole (Korogwe Mjini), Daraja la Mto Mnyuzi (Mpaka wa Korogwe na Handeni kwa njia kuu ya Arusha-Dar) na daraja la Mandera.
Vilevile, njia ya Korogwe-Handeni-Mkata nayo imefungwa kutokana na kujaa maji na kusombwa kwa daraja. Aidha, njia ya mkato ya kuzungukia Korogwe-Mnyuzi/Muheza- Tanga au Korogwe- Mnyuzi-Segera-Chalinze nayo imejaa maji kwa baadhi ya maeneo.
USHAURI:
ALLAH ATULINDE KWA SAFARI ZETU!
Hii ni kutokana na kipande cha barabara ya Segera-Korogwe kuwa na maeneo matatu yaliyojaa maji ambayo ni Daraja la Kilole (Korogwe Mjini), Daraja la Mto Mnyuzi (Mpaka wa Korogwe na Handeni kwa njia kuu ya Arusha-Dar) na daraja la Mandera.
Vilevile, njia ya Korogwe-Handeni-Mkata nayo imefungwa kutokana na kujaa maji na kusombwa kwa daraja. Aidha, njia ya mkato ya kuzungukia Korogwe-Mnyuzi/Muheza- Tanga au Korogwe- Mnyuzi-Segera-Chalinze nayo imejaa maji kwa baadhi ya maeneo.
USHAURI:
- kama huna safari ya lazima sana kwa siku mbili hizi basi unaweza kuahirisha safari kuepuka usumbufu.
- Kama una safari ya lazima unaweza kupitia barabara ya Arusha - Dodoma ambayo huenda kwa wakati huu ipo salama.
- Safiri na fedha ya kutosha kwani kwa kipindi hiki bei za huduma na bidhaa zimepanda kwa baadhi ya wafanyabiashara.
- Kabla ya kuanza safari ni vyema kuwasiliana na viongozi wa usalama barabarani mkoa wa Tanga ama Wilaya ya Korogwe kwa ajili ya kupata uhakika wa safari (ingawa maji hayana muamana maana yanaweza kujaa katika eneo fulani in 30 minutes time pakawa hapapitiki)
- Kwa nia njema, unaweza kuwasiliana kwa nambari ya POLICE KOROGWE ambayo ni 0652449324, ili kuweza kuulizia hali ya usalama barabarani.
ALLAH ATULINDE KWA SAFARI ZETU!