Vijana kwanza nawapongeza kupata udahiri pamoja na mkopo licha ya changamoto zilizopo. Msiopata mkopo poleni sana ila msikate tamaa, mkaripoti kigumu ivyo ivyo kwakuwa kuna nafasi za kukata rufaa(Appealing) ndani ya siku 90 baada ya muhula wa kwanza wa masomo kuanza, fomu za ku-appeal mtapata vyuoni mliko pangwa kwa mshauri wa wanafunzi(dean of students), nina imani mtafanikiwa. Mliopata mkatumie pesa izo vizuri, msinunue simu kali, sabufa, TV, na pamba za bei mbaya. Tulieni, someni kwa bidii, muone mbele zaidi(vision) mkifaulu vizuri na GPA nzuri hamtakumbana na changamoto katika soko la ajira. ASANTENI SANA, NAWATAKIA MAANDALIZI MEMA.