SoC01 Ushauri kwa waliomaliza Kidato cha 6 (baada ya matokeo): Nini cha kusomea Chuo Kikuu Kupambana na Soko la Ajira

Stories of Change - 2021 Competition

Khadija Mtalame

Senior Member
Jul 14, 2021
186
715
Habari wanajukwaa;

Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kunipa afya na wakati mwema Kama huu,ili niweze kutoa upako wa kweli kuhusu hatma ya wanafunzi waliomaliza KIDATO cha 6 kuhusu nini cha kusomea baada ya Necta kutangaza matokeo yao.

Pili na mwisho katika utambulisho,hongereni sana vijana wote mliofanikiwa kufaulu mtihani huo na kufanikiwa kutimiza ndoto zenu.

Mambo yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa katika kuelekea kuchagua masomo ya chuo kikuu,

MOJA,

Vijana wote wanaotaka kufanya maombi ya chuo kikuu wanatakiwa kuhakikisha kwamba WANAISHI NDOTO ZAO, kutokana na kuwepo kwa shida ya ajira ambapo kumekuwa na wahitimu wengi ambao wameshindwa kujiajiri na kuajirika kutokana na namna elimu walivyopata.

Mwanafunzi au mtu yoyote anaetaka kufanya chaguzi ya fani ya kusomea chuo kikuu anatakiwa kwanza kujipima na kuangalia Nini anapenda maishani mwake? Na sio akasomee kitu gani chenye ajira. Mfano, unaweza kukuta kipaumbele Cha serikali ya JMT Ni afya na ualimu sayansi na ukaamua kwenda kusoma katika kada hizo,lakini mwisho wa siku ukamaliza na ukasubiriwa kuajiriwa na endapo hutaajiriwa elimu yako itapotea pia utakuwa umepoteza ndoto zako.

Lakini, endapo mtu ukaamua kusoma kitu unachokipenda moyoni mfano, endapo unapenda kuwa fundi mshonaji wa nguo tangu ukiwa mdogo,Ni lazima uhakikishe kwamba unachagua masomo ambayo ukienda kusoma darasani utakuwa na amani ya moyo na utayapenda sana ,ambapo mwisho wa siku utaelewa na hautakuwa mzigo mtaani Mara utakapomaliza masomo yako.

Hivyo,nawashauri sana vijana muombe vitu ambavyo mnavipenda kutoka moyoni na sio vitu ambayo unahisi au umeshauriwa vina ajira endapo utamaliza,siku hizi hakuna kitu utasoma kitakupa ajira moja kwa moja, hata aliesomea Udaktari anaweza kumaliza na asiajiriwe lakini endapo utasoma Udaktari kwa kupenda hata usipoajiriwa utaweza kujiajiri mwenyewe.

Hivyo napenda kuwaasa, vijana na watanzania wote kwamba ILI TUWEZE KUPAMBANA NA AJIRA KWA WAHITIMU WA VYUO VIKUU,tafadhali tuhakikishe kwamba tuwaambie vijana wetu wakasome vitu wanavyovipenda na sio kitu ambacho anahisi ataweza kuajiriwa endapo akimaliza masomo yake.

PILI, ni ndoto ya kila mwanafunzi anaposoma anakuwa amedhamiria kuwa nani na kwasababu gani. Kwa kuzingatia hilo nipende kuwaambia vijana waliomaliza kidato Cha sita elimu ya chuo kikuu siyo "fashion" kwamba ilimradi nimesoma elimu ya chuo kikuu, jipe nafasi jitafakari angalia mbele miaka 3/4/5 ijayo unataka kuwa nani, hakuna kinachoshindikana, kuamua, kudhamiria na kuchukua maamuzi ni sehemu muhimu katika maisha yenu yote hivyo basi ni vyema kuwa makini zaidi katika wakati wote ambao unajitizama baada ya miaka 3/4 ya kumaliza chuo utakuwa wapi na unafanya nini!

Usikubali kubaki ulipo, usikubali kurudishwa nyuma na marafiki ulionao, amka simama imara chagua kitu kitakachokufanya baada ya miaka 3/4 ya chuo kikuu unakuwa kweli watofauti kubwa.
Ni kweli ajira hakuna hasa zinazotoka serikalini kwa maana ni chache na zina ushindani mkubwa, kama lengo lako hasa ni ukimaliza upate ajira serikalini basi utakuwa hujaamua kuwa nani baada ya miaka ya chuo.

Tuwe na tabia ya kujitizama na kujiwekea malengo makubwa lakini yanayofikika katika maisha yetu ya Chuoni na yakila siku, kwa kuzingatia hili tuwe tayari kuweka mawasiliano sahihi na watu sahihi kwa muda sahihi, tujitahidi kutafakari pale unarudi nyumbani baada ya miaka ya chuo na upo upo tu unaangalia wazazi, tukumbuke suala la kujituma kwa moyo wa dhati liwe kipaumbele chetu kikubwa.

Kumbuka; nyakati zinabadilika Ila mtazamo wa wewe uwe nani baada ya miaka ya chuo unao wewe na wewe ndo kiongozi mkubwa.

Usiende chuo kikuu kwasababu nimechaguliwa kwenda lazima niende, hapa naelezea kidogo jambo, elimu ya chuo kikuu siyo fashion kwamba baada ya miaka 3 ukiona ulichosoma hakifai utarudi tena ukasome kingine, mafanikio yako unayo wewe fanya maamuzi sahihi leo ili kesho ukawe mshindi katika jamii yako na familia yako. Acha kufuata mkumbo.

Leo nakupa kazi ya kufanya kijana uliyechaguliwa kwenda chuo kikuu, tenga saa moja kaa pahala patulivu kuwa na notebook yako na kalamu, zima simu yako, sali kwa imani yako kisha anza kuandika unataka nini baada ya miaka 3 /4 ya chuo kikuu kisha tafakari je ninachoomba kitanifikisha hapo?

Halafu kesho tutaelezeana humu humu kwa comments je tunajionaje baada ya miaka 3/4 ya chuo.

Mwisho kabisa, kumekuwa na wanafunzi wengi waliomaliza michepuo mbalimbali wakiomba ushauri juu ya nini cha kusomea chuo kikuu na ambapo akimaliza ataajiriwa,nawaomba sana tuwaambie wakasome vitu wavipendayo na sio vitu vitakavyowapa ajira ya kuajiriwa wakimaliza masomo yao mfano,Kuna mwalimu wa wito na mwalimu alietaka sehemu ya kuajiriwa tu.

Nawasilisha.
 
Habari wanajukwaa;

Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kunipa afya na wakati mwema Kama huu,ili niweze kutoa upako wa kweli kuhusu hatma ya wanafunzi waliomaliza KIDATO cha 6 kuhusu nini cha kusomea baada ya Necta kutangaza matokeo yao.

Pili na mwisho katika utambulisho,hongereni sana vijana wote mliofanikiwa kufaulu mtihani huo na kufanikiwa kutimiza ndoto zenu.

Mambo yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa katika kuelekea kuchagua masomo ya chuo kikuu,

MOJA,

Vijana wote wanaotaka kufanya maombi ya chuo kikuu wanatakiwa kuhakikisha kwamba WANAISHI NDOTO ZAO, kutokana na kuwepo kwa shida ya ajira ambapo kumekuwa na wahitimu wengi ambao wameshindwa kujiajiri na kuajirika kutokana na namna elimu walivyopata.

Mwanafunzi au mtu yoyote anaetaka kufanya chaguzi ya fani ya kusomea chuo kikuu anatakiwa kwanza kujipima na kuangalia Nini anapenda maishani mwake? Na sio akasomee kitu gani chenye ajira. Mfano, unaweza kukuta kipaumbele Cha serikali ya JMT Ni afya na ualimu sayansi na ukaamua kwenda kusoma katika kada hizo,lakini mwisho wa siku ukamaliza na ukasubiriwa kuajiriwa na endapo hutaajiriwa elimu yako itapotea pia utakuwa umepoteza ndoto zako.

Lakini, endapo mtu ukaamua kusoma kitu unachokipenda moyoni mfano, endapo unapenda kuwa fundi mshonaji wa nguo tangu ukiwa mdogo,Ni lazima uhakikishe kwamba unachagua masomo ambayo ukienda kusoma darasani utakuwa na amani ya moyo na utayapenda sana ,ambapo mwisho wa siku utaelewa na hautakuwa mzigo mtaani Mara utakapomaliza masomo yako.

Hivyo,nawashauri sana vijana muombe vitu ambavyo mnavipenda kutoka moyoni na sio vitu ambayo unahisi au umeshauriwa vina ajira endapo utamaliza,siku hizi hakuna kitu utasoma kitakupa ajira moja kwa moja, hata aliesomea Udaktari anaweza kumaliza na asiajiriwe lakini endapo utasoma Udaktari kwa kupenda hata usipoajiriwa utaweza kujiajiri mwenyewe.

Hivyo napenda kuwaasa, vijana na watanzania wote kwamba ILI TUWEZE KUPAMBANA NA AJIRA KWA WAHITIMU WA VYUO VIKUU,tafadhali tuhakikishe kwamba tuwaambie vijana wetu wakasome vitu wanavyovipenda na sio kitu ambacho anahisi ataweza kuajiriwa endapo akimaliza masomo yake.

PILI, ni ndoto ya kila mwanafunzi anaposoma anakuwa amedhamiria kuwa nani na kwasababu gani. Kwa kuzingatia hilo nipende kuwaambia vijana waliomaliza kidato Cha sita elimu ya chuo kikuu siyo "fashion" kwamba ilimradi nimesoma elimu ya chuo kikuu, jipe nafasi jitafakari angalia mbele miaka 3/4/5 ijayo unataka kuwa nani, hakuna kinachoshindikana, kuamua, kudhamiria na kuchukua maamuzi ni sehemu muhimu katika maisha yenu yote hivyo basi ni vyema kuwa makini zaidi katika wakati wote ambao unajitizama baada ya miaka 3/4 ya kumaliza chuo utakuwa wapi na unafanya nini!

Usikubali kubaki ulipo, usikubali kurudishwa nyuma na marafiki ulionao, amka simama imara chagua kitu kitakachokufanya baada ya miaka 3/4 ya chuo kikuu unakuwa kweli watofauti kubwa.
Ni kweli ajira hakuna hasa zinazotoka serikalini kwa maana ni chache na zina ushindani mkubwa, kama lengo lako hasa ni ukimaliza upate ajira serikalini basi utakuwa hujaamua kuwa nani baada ya miaka ya chuo.

Tuwe na tabia ya kujitizama na kujiwekea malengo makubwa lakini yanayofikika katika maisha yetu ya Chuoni na yakila siku, kwa kuzingatia hili tuwe tayari kuweka mawasiliano sahihi na watu sahihi kwa muda sahihi, tujitahidi kutafakari pale unarudi nyumbani baada ya miaka ya chuo na upo upo tu unaangalia wazazi, tukumbuke suala la kujituma kwa moyo wa dhati liwe kipaumbele chetu kikubwa.

Kumbuka; nyakati zinabadilika Ila mtazamo wa wewe uwe nani baada ya miaka ya chuo unao wewe na wewe ndo kiongozi mkubwa.

Usiende chuo kikuu kwasababu nimechaguliwa kwenda lazima niende, hapa naelezea kidogo jambo, elimu ya chuo kikuu siyo fashion kwamba baada ya miaka 3 ukiona ulichosoma hakifai utarudi tena ukasome kingine, mafanikio yako unayo wewe fanya maamuzi sahihi leo ili kesho ukawe mshindi katika jamii yako na familia yako. Acha kufuata mkumbo.

Leo nakupa kazi ya kufanya kijana uliyechaguliwa kwenda chuo kikuu, tenga saa moja kaa pahala patulivu kuwa na notebook yako na kalamu, zima simu yako, sali kwa imani yako kisha anza kuandika unataka nini baada ya miaka 3 /4 ya chuo kikuu kisha tafakari je ninachoomba kitanifikisha hapo?

Halafu kesho tutaelezeana humu humu kwa comments je tunajionaje baada ya miaka 3/4 ya chuo.

Mwisho kabisa, kumekuwa na wanafunzi wengi waliomaliza michepuo mbalimbali wakiomba ushauri juu ya nini cha kusomea chuo kikuu na ambapo akimaliza ataajiriwa,nawaomba sana tuwaambie wakasome vitu wavipendayo na sio vitu vitakavyowapa ajira ya kuajiriwa wakimaliza masomo yao mfano,Kuna mwalimu wa wito na mwalimu alietaka sehemu ya kuajiriwa tu.

Nawasilisha.
Karibuni tuendelee na mjadala kwa mustakabali mzima wa Taifa letu
 
Fact... Kuna watu wamepona kupitia hili andiko lako... Kura yangu unayo.. pitia na kwangu mkuu
 
Thanks Marjo Mlekwa
Fact... Kuna watu wamepona kupitia hili andiko lako... Kura yangu unayo.. pitia na kwangu mkuu
 
Andiko makini sana

Maana anachomiliki mtu 100% ni akili yake tu na mipango ya kesho yake (ndoto zake), Hivyo wasisome kwa kuangalia vipaumbele vya serikali VINABADILIKA kila leo.
Na bahati mbaya zaidi kila Rais huja na priorities zake
 
Andiko makini sana

Maana anachomiliki mtu 100% ni akili yake tu na mipango ya kesho yake (ndoto zake), Hivyo wasisome kwa kuangalia vipaumbele vya serikali VINABADILIKA kila leo.
Na bahati mbaya zaidi kila Rais huja na priorities zake
Exactly,Mtelengu naomba Kura yako,vile vile naomba uwafikishie wenzako..,Salam waje wauone Uzi huu
 
Habari wanajukwaa;

Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kunipa afya na wakati mwema Kama huu,ili niweze kutoa upako wa kweli kuhusu hatma ya wanafunzi waliomaliza KIDATO cha 6 kuhusu nini cha kusomea baada ya Necta kutangaza matokeo yao.

Pili na mwisho katika utambulisho,hongereni sana vijana wote mliofanikiwa kufaulu mtihani huo na kufanikiwa kutimiza ndoto zenu.

Mambo yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa katika kuelekea kuchagua masomo ya chuo kikuu,

MOJA,

Vijana wote wanaotaka kufanya maombi ya chuo kikuu wanatakiwa kuhakikisha kwamba WANAISHI NDOTO ZAO, kutokana na kuwepo kwa shida ya ajira ambapo kumekuwa na wahitimu wengi ambao wameshindwa kujiajiri na kuajirika kutokana na namna elimu walivyopata.

Mwanafunzi au mtu yoyote anaetaka kufanya chaguzi ya fani ya kusomea chuo kikuu anatakiwa kwanza kujipima na kuangalia Nini anapenda maishani mwake? Na sio akasomee kitu gani chenye ajira. Mfano, unaweza kukuta kipaumbele Cha serikali ya JMT Ni afya na ualimu sayansi na ukaamua kwenda kusoma katika kada hizo,lakini mwisho wa siku ukamaliza na ukasubiriwa kuajiriwa na endapo hutaajiriwa elimu yako itapotea pia utakuwa umepoteza ndoto zako.

Lakini, endapo mtu ukaamua kusoma kitu unachokipenda moyoni mfano, endapo unapenda kuwa fundi mshonaji wa nguo tangu ukiwa mdogo,Ni lazima uhakikishe kwamba unachagua masomo ambayo ukienda kusoma darasani utakuwa na amani ya moyo na utayapenda sana ,ambapo mwisho wa siku utaelewa na hautakuwa mzigo mtaani Mara utakapomaliza masomo yako.

Hivyo,nawashauri sana vijana muombe vitu ambavyo mnavipenda kutoka moyoni na sio vitu ambayo unahisi au umeshauriwa vina ajira endapo utamaliza,siku hizi hakuna kitu utasoma kitakupa ajira moja kwa moja, hata aliesomea Udaktari anaweza kumaliza na asiajiriwe lakini endapo utasoma Udaktari kwa kupenda hata usipoajiriwa utaweza kujiajiri mwenyewe.

Hivyo napenda kuwaasa, vijana na watanzania wote kwamba ILI TUWEZE KUPAMBANA NA AJIRA KWA WAHITIMU WA VYUO VIKUU,tafadhali tuhakikishe kwamba tuwaambie vijana wetu wakasome vitu wanavyovipenda na sio kitu ambacho anahisi ataweza kuajiriwa endapo akimaliza masomo yake.

PILI, ni ndoto ya kila mwanafunzi anaposoma anakuwa amedhamiria kuwa nani na kwasababu gani. Kwa kuzingatia hilo nipende kuwaambia vijana waliomaliza kidato Cha sita elimu ya chuo kikuu siyo "fashion" kwamba ilimradi nimesoma elimu ya chuo kikuu, jipe nafasi jitafakari angalia mbele miaka 3/4/5 ijayo unataka kuwa nani, hakuna kinachoshindikana, kuamua, kudhamiria na kuchukua maamuzi ni sehemu muhimu katika maisha yenu yote hivyo basi ni vyema kuwa makini zaidi katika wakati wote ambao unajitizama baada ya miaka 3/4 ya kumaliza chuo utakuwa wapi na unafanya nini!

Usikubali kubaki ulipo, usikubali kurudishwa nyuma na marafiki ulionao, amka simama imara chagua kitu kitakachokufanya baada ya miaka 3/4 ya chuo kikuu unakuwa kweli watofauti kubwa.
Ni kweli ajira hakuna hasa zinazotoka serikalini kwa maana ni chache na zina ushindani mkubwa, kama lengo lako hasa ni ukimaliza upate ajira serikalini basi utakuwa hujaamua kuwa nani baada ya miaka ya chuo.

Tuwe na tabia ya kujitizama na kujiwekea malengo makubwa lakini yanayofikika katika maisha yetu ya Chuoni na yakila siku, kwa kuzingatia hili tuwe tayari kuweka mawasiliano sahihi na watu sahihi kwa muda sahihi, tujitahidi kutafakari pale unarudi nyumbani baada ya miaka ya chuo na upo upo tu unaangalia wazazi, tukumbuke suala la kujituma kwa moyo wa dhati liwe kipaumbele chetu kikubwa.

Kumbuka; nyakati zinabadilika Ila mtazamo wa wewe uwe nani baada ya miaka ya chuo unao wewe na wewe ndo kiongozi mkubwa.

Usiende chuo kikuu kwasababu nimechaguliwa kwenda lazima niende, hapa naelezea kidogo jambo, elimu ya chuo kikuu siyo fashion kwamba baada ya miaka 3 ukiona ulichosoma hakifai utarudi tena ukasome kingine, mafanikio yako unayo wewe fanya maamuzi sahihi leo ili kesho ukawe mshindi katika jamii yako na familia yako. Acha kufuata mkumbo.

Leo nakupa kazi ya kufanya kijana uliyechaguliwa kwenda chuo kikuu, tenga saa moja kaa pahala patulivu kuwa na notebook yako na kalamu, zima simu yako, sali kwa imani yako kisha anza kuandika unataka nini baada ya miaka 3 /4 ya chuo kikuu kisha tafakari je ninachoomba kitanifikisha hapo?

Halafu kesho tutaelezeana humu humu kwa comments je tunajionaje baada ya miaka 3/4 ya chuo.

Mwisho kabisa, kumekuwa na wanafunzi wengi waliomaliza michepuo mbalimbali wakiomba ushauri juu ya nini cha kusomea chuo kikuu na ambapo akimaliza ataajiriwa,nawaomba sana tuwaambie wakasome vitu wavipendayo na sio vitu vitakavyowapa ajira ya kuajiriwa wakimaliza masomo yao mfano,Kuna mwalimu wa wito na mwalimu alietaka sehemu ya kuajiriwa tu.

Nawasilisha.
teh teh teh..
akubariki Mungu.. kwa kweli umenena mambo ya kweli kabisa..
mimi kama miongoni mwa wahitimu wa kidato cha sita.. nimekuelew vizuli sana dada/mamaangu.. asante kwa ushauri mzuri
 
teh teh teh..
akubariki Mungu.. kwa kweli umenena mambo ya kweli kabisa..
mimi kama miongoni mwa wahitimu wa kidato cha sita.. nimekuelew vizuli sana dada/mamaangu.. asante kwa ushauri mzuri
Thanks Ngotho,

Naomba sambaza Uzi kwa vijana wa f6 waweze kusoma upako huu mtakatifu
 
Back
Top Bottom