Ushauri kwa Vyuo vikuu: Walau nusu ya wahadhiri wawe na PhD

moma2k

JF-Expert Member
Dec 12, 2010
1,061
1,327
TCU ifanye utafiti na kuja na kanuni mpya zenye kuipeleka nchi kwenye uchumi wa viwanda. Vyuo vikuu vyetu havina mchango mkubwa kwa uchumi na maendeleo ya nchi kwasababu hakuna tafiti zenye kubuni mambo mapya. Mfumo wa uchumi wa viwanda unahitaji ugunduzi wa mambo(research).

Kwakuwa kuna idadi ndogo sana ya wahadhiri wenye PhD ktk vyuo vikuu hapa TZ, ni vyema TCU ikaboresha kanuni zake na kuweka sharti la kila chuo kukuu nchini kuwa walao na NUSU YA WAHADHIRI WENYE PhD.

Pia TCU ifute vipengele visivyo na tija kwa taifa kama sharti la kiwango cha GPA 3.8 undergraduate ili mtu aweze kuwa mhadhiri na vigezo vingine ambavyo vimepitwa na wakati na vinachangia kurudisha nyuma maendeleo ya kitaaluma na ya nchi.

Mtu mwenye PhD kama anatakuwa mhadhiri basi aingie darasani kufindisha bila kikwazo.
 
Ni kweli. Tatizo la TCU ni vigezo vyao vya GPA, tena undergraduate..!!! Kwa nini isiwe ili uwe lecturer lazima form four au form six uwe na division 1. Maana kuna watu walitoka high school na division one, wengine three.

Kwenye hao vyuoni, mwenye one kutoka na GPA ya 3.0, na mwenye division 3,katoka na GPA ya 4.2 undergraduate. Hapo hapo, tukaenda wote masters za statistics. Kwenye masters, yule wa GPA ya 4.2, undergraduate akapata GPA ya 3.2 kwenye masters , na mimi mwenye GPA ya 3 undergraduate, masters nikapata GPA 4.4. TCU mtachagua yupi kuwa lecturer?
 
Je, kwa vigezo vyenu TCU, hiki kigezo cha GPA ya 3.8 kiacheni cha undergraduate. Maana huwezi linganisha GPA ya SUA, Udsm, Mzumbe, Tumaini, Arusha University na St Augustin mwanza.
Sio vyuo tu,hata faculty zimetofautiana..
 
Ni kweli. Tatizo la TCU ni vigezo vyao vya GPA, tena undergraduate..!!! Kwa nini isiwe ili uwe lecturer lazima form four au form six uwe na division 1. Maana kuna watu walitoka high school na division one, wengine three.

Kwenye hao vyuoni, mwenye one kutoka na GPA ya 3.0, na mwenye division 3,katoka na GPA ya 4.2 undergraduate. Hapo hapo, tukaenda wote masters za statistics. Kwenye masters, yule wa GPA ya 4.2, undergraduate akapata GPA ya 3.2 kwenye masters , na mimi mwenye GPA ya 3 undergraduate, masters nikapata GPA 4.4. TCU mtachagua yupi kuwa lecturer?
Sifa ya mhadh
Kuna watu wakishavuka daraja, watalichoma moto au kulibomoa ili wengine wapate shida kuvuka. Hatusemi kusiwe na vigezo lakini tuwe na vigezo vyenye mantiki. Kuna shirika la umma lilikuwa linatafuta HRO wakaweka kigezo cha GPA 3.5.
Hao wote hawatafaa kulingana na vigezo vilivyopo. Inahitajika consistence katika ufaulu kwa kila ngazi ya elimu. Nijuavyo mimi ukiomba kazi ya assistant lecturer unatakiwa uwe na GPA isiyopungua 3.8 na masters isiyopungua 4. Ukiajiliwa kama Tutorial assistant unatakiwa uwe na GPA ya undergraduate isiyopungua 3.8 na iwapo utaenda kusoma baada ya kuajiliwa basi ufaulu wako wa masters unatakiwa uwe kuanzia GPA ya 4 vinginevyo unakuwa disqualified kuwa academician. Nafikiri tusitafute kupanua magoli kwani vigezo hivyo nimurua kabisa.
 
Sifa ya mhadh

Hao wote hawatafaa kulingana na vigezo vilivyopo. Inahitajika consistence katika ufaulu kwa kila ngazi ya elimu. Nijuavyo mimi ukiomba kazi ya assistant lecturer unatakiwa uwe na GPA isiyopungua 3.8 na masters isiyopungua 4. Ukiajiliwa kama Tutorial assistant unatakiwa uwe na GPA ya undergraduate isiyopungua 3.8 na iwapo utaenda kusoma baada ya kuajiliwa basi ufaulu wako wa masters unatakiwa uwe kuanzia GPA ya 4 vinginevyo unakuwa disqualified kuwa academician. Nafikiri tusitafute kupanua magoli kwani vigezo hivyo nimurua kabisa.
Jiulize tumetokea wapi tunakwenda wapi. Issue siyo kupanua magoli ni kuwa consistent-lakini haya kila uchao unabadilisha goal post ili wengine wakwame ndio naita kuchoma daraja.
 
Kuna mtendaji mmoja wa serikali aliamua kwa utashi wake mwenyewe kukatisha masomo ya Ph.D kwa wafanyakazi wa chini yake, baada ya kulipiwa na serikali kwa muda wa miaka miwilii. Kisa hiki kilishangaza wafanyakazi wengi sana.
 
TCU inatakiwa waliangalie kwa jicho la haki kwa masilahi ya taifa letu. Mtu ana PhD halafu anakuwa disqualified kuwa mhadhiri. Hapo hapo darasani kuna undergraduate anawafundisha undergraduates eti kwasababu amequalify. Scenario hii ni ngumu sana kuingia akilini. That law is a very bad. Mwisho wa siku wanaoathilika ni watanzania. Huyu wa PhD amespecialize kwenye masters, akafanya superspecialization kwenye PhD ni unqualified. Ndiyo maana wasomi wengi wanakimbilia kwenye siasa. Na kuacha vyuo vyetu vikuu vikifundishwa na undergraduate.
 
3.5 iwe cut-off point
Jiulize tumetokea wapi tunakwenda wapi. Issue siyo kupanua magoli ni kuwa consistent-lakini haya kila uchao unabadilisha goal post ili wengine wakwame ndio naita kuchoma daraja.
umemjibu vizuri sana, GPA haifundishi, upper second class ya 3.5 ni kubwa sana kama ni kupima uwezo wa candidate, cha msingi wahusika waonyeshe uwezo wao katika interview, utakuta mtu ana first class lakini ukimpa dakika 15 za kuwasilisha mada ya kitaalamu utalia kwa kumwonea huruma.Pi GPA kubwa lakini uwezo wa kudeliver ni zero
 
cut off GPA ya TCU ni 3.5, hata hivyo vyuo huwa
vinakuwa na uhuru wa kujiwekea GPA yao ilimradi haiendi chini ya ile ya TCU.
 
cut off GPA ya TCU ni 3.5, hata hivyo vyuo huwa
vinakuwa na uhuru wa kujiwekea GPA yao ilimradi haiendi chini ya ile ya TCU.
naomba ni kuulize swali kidogo, kwa maelezo uliyoyatoa hapo juu, kuna haja ya Serikali /vyuo vikuu vya serikali kuajiri PhD holders kutoka nchi nyingine kwa kigezo cha GPA ya 3.8 undergraduate angali kuna watanzania wenye PhD husika na GPA za 3.5? huku tunalalamika vijana hawana ajira huku nafasi zao za ajira zinajazwa na wageni bila sababu za msingi.
 
siyo sahihi kabisa kuilinganishaGPA yangu ya 3.7 undergraduate BLS SUA na 3.8 undergraduate ya st augustine. Lakini kwa kigezo cha GPA mimi wa SUA tena JEMBE nitaachwa atachukuliwa kilasa.
Unakuwa mzembe shule ile ubebwe na jina la chuo siyo?
Kwani zikitangazwa nafasi si kuna interview?
Acha kuintertain ujinga.
 
TCU inatakiwa waliangalie kwa jicho la haki kwa masilahi ya taifa letu. Mtu ana PhD halafu anakuwa disqualified kuwa mhadhiri. Hapo hapo darasani kuna undergraduate anawafundisha undergraduates eti kwasababu amequalify. Scenario hii ni ngumu sana kuingia akilini. That law is a very bad. Mwisho wa siku wanaoathilika ni watanzania. Huyu wa PhD amespecialize kwenye masters, akafanya superspecialization kwenye PhD ni unqualified. Ndiyo maana wasomi wengi wanakimbilia kwenye siasa. Na kuacha vyuo vyetu vikuu vikifundishwa na undergraduate.
nchi yetu kiujumla tuna udhaifu wakutodhamini rasilimali watu tulizo nazo na hii inasababisha matumizi mabaya ya rasilimali na matokeo yake ni umasikini usioisha. HAINGII AKILI MIAKA ZAIDI YA 50 YA KUANZISHWA KWA ELIMU YA CHUO KIKUU HAPA NCHINI BADO NCHI YANGU INAENDELEA KUWA TEGEMEZI KWA MAMBO MADOGO.
 
ELEWA KABLA YA KUCHANGIA!
Nani kakwambia ukisoma SUA basi uhurumiwe kila sehemu? Kwani wanaofundisha SAUT si wamesomea SUA na wengine vyuo vya maana nje ya Tz na wengine wamekuwa marekecture SUA na hata UDSM kama Baregu na wengineo? Wewe kama hukuweza kupata GPA inayohitajika tulia. Waache waliopata wapambane kufundisha vyuo. Au unataka tuseme kwa kuwa SUA imeanzishwa zamani au MZUMBE au UDSM basi huko ndo wanapaswa kutoka malecture?
 
Cut of iwe 3.5, halafu wawaite wote wafanye usaili ili kuchuja watu wenye uwezo mkubwa wa kuwakilisha mambo kitaalamu
 
Back
Top Bottom