Mabibi na mabwana heshima kwenu.
Hapa ni ushauri wa bure kwao vyama vyote watia nia kuelekea lala salama katika uchaguzi huu.
Zimekuwapo changamoto nyingi katika kufikisha ujumbe kwa wapiga kura. Pana vyama waziwazi vimekuwa vikibebwa na vyombo vya habari (vya umma na hata vya binafsi hali vingine vikiminywa).
Yote kheri, sera zote kwa hakika zimeshawafikia wapiga kura vilivyo. Hayupo mpiga kura ambaye hadi leo kuwa ati hajui chama gani kina simamia nini.
Hakuna asiyejua kuwa vyama vyote vinasimamia maendeleo. Hakipo chama kisichokuwa na neno maendeleo au mipango ya maendeleo katika sera zake.
Hakuna asiyejua kuwa tofauti ya CCM na vyama vingine ipo kwenye masuala ya "haki na uhuru" wengine wakiita haya kuwa ni "bata."
Kwa vile yote haya yanajulikana vilivyo, ilikuwa ni muda sasa kupeleka ujumbe lengwa unakokosekana na mahali unapohusika.
Tuelekeze sasa kampeni kwa tume na wote wanaohusika na usimamizi wa uchaguzi huu.
Vyama na vipaze sauti ya kutosha sasa kwa mamlaka hizi na hasa tume kama sehemu ya kampeni, kuhitaji amani kwa taifa hili. Kazi hii isiachiwe asasi za dini peke yake.
Wanasema waungwana, "Common sense is not so common to everyone" ila amani itakatokana na uchaguzi utakaokuwa "huru na wa haki."
Chama kitakachojikita kwenye kudai uchaguzi huru na wa haki (free, fair and credible election) kwa hakika kitavuna vilivyo.
Watanzania tunataka amani hali tukijua tutavuna tunachopanda.
"Tupande uhuru na haki katika uchaguzi huu tukavune amani na mshikamano kwa taifa letu."
Tunataka amani na mshikamano kama taifa.
Hayo ni matunda ya haki.
Hapa ni ushauri wa bure kwao vyama vyote watia nia kuelekea lala salama katika uchaguzi huu.
Zimekuwapo changamoto nyingi katika kufikisha ujumbe kwa wapiga kura. Pana vyama waziwazi vimekuwa vikibebwa na vyombo vya habari (vya umma na hata vya binafsi hali vingine vikiminywa).
Yote kheri, sera zote kwa hakika zimeshawafikia wapiga kura vilivyo. Hayupo mpiga kura ambaye hadi leo kuwa ati hajui chama gani kina simamia nini.
Hakuna asiyejua kuwa vyama vyote vinasimamia maendeleo. Hakipo chama kisichokuwa na neno maendeleo au mipango ya maendeleo katika sera zake.
Hakuna asiyejua kuwa tofauti ya CCM na vyama vingine ipo kwenye masuala ya "haki na uhuru" wengine wakiita haya kuwa ni "bata."
Kwa vile yote haya yanajulikana vilivyo, ilikuwa ni muda sasa kupeleka ujumbe lengwa unakokosekana na mahali unapohusika.
Tuelekeze sasa kampeni kwa tume na wote wanaohusika na usimamizi wa uchaguzi huu.
Vyama na vipaze sauti ya kutosha sasa kwa mamlaka hizi na hasa tume kama sehemu ya kampeni, kuhitaji amani kwa taifa hili. Kazi hii isiachiwe asasi za dini peke yake.
Wanasema waungwana, "Common sense is not so common to everyone" ila amani itakatokana na uchaguzi utakaokuwa "huru na wa haki."
Chama kitakachojikita kwenye kudai uchaguzi huru na wa haki (free, fair and credible election) kwa hakika kitavuna vilivyo.
Watanzania tunataka amani hali tukijua tutavuna tunachopanda.
"Tupande uhuru na haki katika uchaguzi huu tukavune amani na mshikamano kwa taifa letu."
Tunataka amani na mshikamano kama taifa.
Hayo ni matunda ya haki.