Ushauri kwa Taasisi za Serikali na Benki za Kibiashara hasa Benki za NMB na CRDB

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,991
144,322
Kupitia mtandao huu, napenda nitoe wazo/ushauri kwa Benki za kibiashara, hasa Benki za NMB na CRDB, benki ambazo zinaonekana kushindana kuvutia watumishi wa umma kupitishia mishahara yao katika benki hizo.

Kwa mfano,hizi benki mbili kwa sasa zote zimeanzisha huduma ya salary advance, huduma ambayo licha ya kuwa ni ya kibiashara, bila shaka ina lengo lingine la kuvuti watumishi wa umma kupitishia mishahara yao katika Benki hizo.

Si hivyo tu, hivi sasa mtumishi anaetaka mkopo katika mojawapo ya mabenki haya, moja ya shariti ni mshahara wa mtumishi husika ni lazima kwanza upite katika benki yao na kama haupiti, basi utatakiwa kubadili akaunti ya mshahara kuweza mshahara upite katika benki uliyoombea mkopo.

Leo hii napenda niwape wazo la kibiashara ambalo litawezekana iwapo Benki hizi na Taasisi za serikali(hapa kama waajiri) watakaa pamoja na kukubaliana na kisha kuwashirikisha wafanyakazi.

Nachotaka kusema ni nini hasa?
Kwakuwa kuna baadhi ya Idara na Taasisi za serikali ambazo hutoa malipo(posho kwa kila mwezi) kwa wafanyakazi wake mbali na mishahara, lakini malipo hayo mara nyingi hutoka kwa kuchelewa, mabenki haya yanaweza kutoa malipo hayo kila mwezi katika tarehe iliyokusudiwa ila kwa shariti kwamba mshahara na malipo mengine yote ya mtumishi husika lazima yapite katika benki hiyo. Benki husika itakata fedha fedha zake pale mwajiri anapowasilisha malipo ya wafanyakazi wake katik benki hiyo.

Kinachotakiwa hapa ni mabenki haya kukaa chini na waajiri na wakisha kukubaliana, wanashirikisha wafanyakazi ambapo benki zitaanza kushawishi wafanyakazi kujiunga na benki yao na kufaidika na huduma hiyo hasa kwa waajiriwa wapya na wale watakaokuwa teyari kubadili account zao za mishahara(kwa wale ambao teyari ni waajiriwa).

Ulkweli ni kwamba, hela anayopata katika tarehe ya kuelewaka kila mwezi, ni rahisi kuipangia mipango na matumizi kwani inakuwa ni ya uhakika bila kujali ni ndogo au kubwa mradi unaipata katika tarehe ya kueleweka.

Na leo naomba niipongeze serikali ya Marehemu Magufuli kwa kuwa consistency katika tarehe ya kulipa mishahara ya watumishi wa umma kwani katika hili, wamejitahidi sana na hakika wanastahili pongezi ingawa kwa miaka sita mshahara umebaki ni ule ule(holi ndio tatizo).

Nitoe wito pia kwa Mama Samia kusimamia na kuendeleza utaratibu huu wa kuwa consistency katika tarehe ya kulipa mishahara ya watumishi wa umma kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake, Marehemu Magufuli.

Hivyo, nashauri mabenki kutazama fursa hii kwa lengo la kusaidia watumishi husika kupata malipo yao katika tarehe ile ile kila mwezi na pia mabenki husika nayo kupata faida kwani mtumishi huyu atapoenda kuchukua fedha zake iwe ni kupitia ATM au ndani ya benki, atatozwa gharama na hapo benki nayo itakuwa imefaidika pia.

Vile vile, Vyuo Vikuu na Bodi ya Mikopo(HESLB), wanaweza kufanya jambo kama hili hasa kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaofungua akaunti za kupitishia mikopo yao mara wanapowasili vyuoni kuanza masomo.

Nawaachia wahusika.
 
Kupitia mtandao huu, napenda nitoe wazo/ushauri kwa Benki za kibiashara, hasa Benki za NMB na CRDB, benki ambazo zinaonekana kushindana kuvutia watumishi wa umma kupitishia mishahara yao katika benki hizo.

Kwa mfano,hizi benki mbili kwa sasa zote zimeanzisha huduma ya salary advance, huduma ambayo licha ya kuwa ni ya kibiashara, bila shaka ina lengo lingine la kuvuti watumishi wa umma kupitishia mishahara yao katika Benki hizo.

Si hivyo tu, hivi sasa mtumishi anaetaka mkopo katika mojawapo ya mabenki haya, moja ya shariti ni mshahara wa mtumishi huyo upite katika benki yao.

Leo hii napenda niwape wazo la kibiashara ambalo litawezekana iwapo Benki hizi na Taasisi za serikali(hapa kama waajiri) watakaa pamoja na kukubaliana na kisha kuwashirikisha wafanyakazi.

Nachotaka kusema ni nini hasa?
Kwakuwa kuna baadhi ya Idara na Taasisi za serikali ambazo hutoa malipo ya wafanyakazi wake kila mwezi mbali na mishahara lakini malipo hayo huwa hayatoki katika tarehe zilizokusudiwa(huchelewa), basi mabenki haya yanaweza kutoa malipo hayo kwa kila mwezi katika tarehe iliyokusudiwa (pangwa) kwa shariti kwamba mshahara na malipo mengine yote ya mtumishi husika lazima yapite katika benki hiyo. Benki hiyo itakata fedha husika mwajiri anapowasilisha malipo ya wafanyakazi wake katik benki hiyo.

Kinachotakiwa hapa ni mabenki haya kukaa chini na waajiri na wakisha kukubaliana, wanashirikisha wafanyakazi ambapo benki zitaanza kushawishi wafanyakazi kujiunga na benki yao na kufaidika na huduma hiyo hasa kwa waajiriwa wapya na wale watakaokuwa teyari kubadili account zao za mishahara(kwa wale ambao teyari ni waajiriwa).

Ulkweli ni kwamba, hela anayopata katika tarehe ya kuelewaka kila mwezi, ni rahisi kuipangia mipango na matumizi kwani inakuwa ni ya uhakika bila kujali ni ndogo au kubwa mradi unaipata katika tarehe ya kueleweka.

Na leo naomba niipongeze serikali ya Marehemu Magufuli kwa kuwa consistency katika tarehe ya kulipa mishahara ya watumishi wa umma kwani katika hili, wamejitahidi sana na hakika wanastahili pongezi ingawa kwa miaka sita mshahara umebaki ni ule ule(holi ndio tatizo).

Nitoe wito pia kwa Mama Samia kusimamia na kuendeleza utaratibu huu wa kuwa consistency katika tarehe ya kulipa mishahara ya watumishi wa umma kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake, Marehemu Magufuli.

Hivyo, nashauri mabenki kutazama fursa hii kwa lengo la kusaidia watumishi husika kupata malipo yao katika tarehe ile ile kila mwezi na pia mabenki husika nayo kupata faida kwani mtumishi huyu atapoenda kuchukua fedha zake iwe ni kupitia ATM au ndani ya benki, atatozwa gharama na hapo benki nayo itakuwa imefaidika pia.

Vile vile, Vyuo Vikuu na Bodi ya Mikopo(HESLB), wanaweza kufanya jambo kama hili hasa kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaofungua akaunti za kupitishia mikopo yao mara wanapowasili vyuoni kuanza masomo.

Nawaachia wahusika.
Umeongea kwa niaba ya Bavicha au ni maoni yako binafsi bwashee?
 
Kupitia mtandao huu, napenda nitoe wazo/ushauri kwa Benki za kibiashara, hasa Benki za NMB na CRDB, benki ambazo zinaonekana kushindana kuvutia watumishi wa umma kupitishia mishahara yao katika benki hizo.

Kwa mfano,hizi benki mbili kwa sasa zote zimeanzisha huduma ya salary advance, huduma ambayo licha ya kuwa ni ya kibiashara, bila shaka ina lengo lingine la kuvuti watumishi wa umma kupitishia mishahara yao katika Benki hizo.

Si hivyo tu, hivi sasa mtumishi anaetaka mkopo katika mojawapo ya mabenki haya, moja ya shariti ni mshahara wa mtumishi huyo upite katika benki yao.

Leo hii napenda niwape wazo la kibiashara ambalo litawezekana iwapo Benki hizi na Taasisi za serikali(hapa kama waajiri) watakaa pamoja na kukubaliana na kisha kuwashirikisha wafanyakazi.

Nachotaka kusema ni nini hasa?
Kwakuwa kuna baadhi ya Idara na Taasisi za serikali ambazo hutoa malipo ya wafanyakazi wake kila mwezi mbali na mishahara lakini malipo hayo huwa hayatoki katika tarehe zilizokusudiwa(huchelewa), basi mabenki haya yanaweza kutoa malipo hayo kwa kila mwezi katika tarehe iliyokusudiwa (pangwa) kwa shariti kwamba mshahara na malipo mengine yote ya mtumishi husika lazima yapite katika benki hiyo. Benki hiyo itakata fedha husika mwajiri anapowasilisha malipo ya wafanyakazi wake katik benki hiyo.

Kinachotakiwa hapa ni mabenki haya kukaa chini na waajiri na wakisha kukubaliana, wanashirikisha wafanyakazi ambapo benki zitaanza kushawishi wafanyakazi kujiunga na benki yao na kufaidika na huduma hiyo hasa kwa waajiriwa wapya na wale watakaokuwa teyari kubadili account zao za mishahara(kwa wale ambao teyari ni waajiriwa).

Ulkweli ni kwamba, hela anayopata katika tarehe ya kuelewaka kila mwezi, ni rahisi kuipangia mipango na matumizi kwani inakuwa ni ya uhakika bila kujali ni ndogo au kubwa mradi unaipata katika tarehe ya kueleweka.

Na leo naomba niipongeze serikali ya Marehemu Magufuli kwa kuwa consistency katika tarehe ya kulipa mishahara ya watumishi wa umma kwani katika hili, wamejitahidi sana na hakika wanastahili pongezi ingawa kwa miaka sita mshahara umebaki ni ule ule(holi ndio tatizo).

Nitoe wito pia kwa Mama Samia kusimamia na kuendeleza utaratibu huu wa kuwa consistency katika tarehe ya kulipa mishahara ya watumishi wa umma kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake, Marehemu Magufuli.

Hivyo, nashauri mabenki kutazama fursa hii kwa lengo la kusaidia watumishi husika kupata malipo yao katika tarehe ile ile kila mwezi na pia mabenki husika nayo kupata faida kwani mtumishi huyu atapoenda kuchukua fedha zake iwe ni kupitia ATM au ndani ya benki, atatozwa gharama na hapo benki nayo itakuwa imefaidika pia.

Vile vile, Vyuo Vikuu na Bodi ya Mikopo(HESLB), wanaweza kufanya jambo kama hili hasa kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wanaofungua akaunti za kupitishia mikopo yao mara wanapowasili vyuoni kuanza masomo.

Nawaachia wahusika.

Mkuu wazo lako ni zuri sana japo wengine wanaweza kulifananisha na salary advance lakini ni jambo jema sana kama wakifanikiwa kufanya maana yake mtu anaweza pewa mshahara wake wote ....

Nafikiri ikiwekwa hii basi salary advance inaweza boreshwa ili isifanane nayo ....

Wazo zuri
 
Mkopo kwenye mabenki ni kitu private mwajiri haimuhusu hata siku moja
 
Mkopo kwenye mabenki ni kitu private mwajiri haimuhusu hata siku moja
Kwanza sio kweli kuwa ni siri kwa mwajiri kwani mwajiri ndio huidhinisha mkopo wa mtumishi kwa Benki.

Pia soma uelewe mada inaongelea nini kabla ya kuchangia.
 
Kwanza sio kweli kuwa ni siri kwa mwajiri kwani mwajiri ndio huidhinisha mkopo wa mtumishi kwa Benki.

Pia soma uelewe mada inaongelea nini kabla ya kuchangia.
Mwajiri haidhinishi mkopo anakuandikia tu barua ya utambulisho kuwa wewe ni mfanyakazi wake.Mkopo ben9ki ndio inaidhinisha.Unachanganya mambo
 
Mwajiri haidhinishi mkopo anakuandikia tu barua ya utambulisho kuwa wewe ni mfanyakazi wake.Mkopo ben9ki ndio inaidhinisha.Unachanganya mambo
Bora ukae kimya tu kama jambo hulijui. Kwenye form ya mkopo unayojaza mkopoja kuna section ya mwajiri kujaza na pia mwajiri kupitia maafisa Utumishi ndio huingiza makato ya mkopo kwenye system ili kuwezesha mshahara kukatwa kila mwezi.

Nakushauri uwe msomaji kwa mambo usiyoyajua.

Na mwisho, mada hii wala ilikuwa haingolei swala la mikopo(soma vizuri).
 
salary-slip
Mkuu kibenki huu utaratibu huitwa Finance Program mara nyingi huwa ni mpango unaofanyika kati ya mtoa huduma/ msambazaji na mtumiaji/mnunuzi (supplier and consumer or buyer) mpango huu huwa na kitu kinaitwa discount calculator ( au kikotoo) ambacho mara nyingi hukata tozo ya 1.6% mpaka 2% ya kiwango kitakacholipwa kwa msambazaji. Namna unavyofanya kazi hautofautiani na maelezo yako kwamba mosi ni lazima buyer/consumer aithibitishie banki kwamba anafanya biashara na msambaji na invoice yake inathani hii... na italipwa ndani ya siku kadhaa. Mara nyingi baada ya uthibitisho banki humlipa msambazaji ndani ya siku 5 au 7.

FAIDA: Hii usaidia mzunguko wa fedha na ukuaji wa biashara kwa msambazaji kuwa wenye tija, humpunguzia mzigo wa kuomba mikopo mara nyingine yenye riba kubwa na masharti mengi magumu.

Kwa benki pia huwa ni chanzo kizuri cha kujiingizia faida, mfano kwa kiasi cha Tshs 100,000,000 inayoweza kulipwa ndani ya siku 45-60 banki huingiza kati ya 1.6m - 2m per invoice lets say supplier anakazi nyingi anazopata kwa mwezi maana yake faida kwa banki pia ni nzuri na yenye uhakika.

Nirejee kwenye mada yako, mpango huu kwa wafanyakazi wa serikali, mabenki yanaweza kuuchukua lakini una kuwa na kazi nyingi kwa sababu transaction ni nyingi na ni zenye amount ndogo ndogo na wakati mwingine hazina hakika kwamba zitalipwa kwa wakati.. rejea malimbikizo ya posho za walimu kuna ambao wanaidai serikali kwa miaka 2-10 mpaka sasa. Hivyo kwa benki ya kiabiashara huu sio mpango wanaoweza kurisk fedha zao wakati kuna wafanyabiashara wenye uhakika nje na wanao hitaji fedha nyingi, rejea kampuni za kandarasi nk.

Maafisa masoko wa mabenki huu mpango wanao mezani kitambo na huwa wanawezakuingia na wafanyakazi wa makampuni binafsi ya kimataifa kuliko wafanyakazi wa serikali kuu.
 
Back
Top Bottom