hata mimi
JF-Expert Member
- Oct 17, 2017
- 1,356
- 1,437
Nilisikia majuzi wabunge wanasema serikali inakosa pesa zinazoachwa kwenye akaunti za mitandao ya simu za mkononi wakisema kampuni husika zinavuna pesa hizo. Katika suluhisho waliloliona wao ni kwamba kuwe na utaratibu utakaowezesha fedha hizo zirudishwe serikalini
Binafsi yangu mimi naona hilo siyo sahihi badala yake wangesaidia mfiwa/mrithi wa marehemu apate fedha hiyo kwanza kabla ya kuwaza kuipeleka serikalini
Nilisoma sehemu fulani kwamba ukitaka kuipata fedha iliyopo kwenye simu ya mtu aliyekufa itakubidi upeleke mlolongo wa viambata (wameviorodhesha huko niliposoma) upeleke kwenye (ofisi za) mtandao husika ndipo wakupe PIN ya marehemu
Jambo la ajabu ni kwamba sikuona popote maelezo ya kuhusu wao mtandao wanachukua fedha hiyo iliyoachwa kwa masharti yapi (kwa viambata gani)
Kwahiyo ushauri wangu aangaliwe kwanza mrithi arahisishiwe namna ya kupata fedha hiyo (iwe ndio namba moja) halafu ikitokea sasa salio likawa dogo au hata kubwa ila akaamua kuliacha kwa hiari yake ndipo tuhamie upande wa serikali wachukue zote (serikali wawe ni namba mbili)
Hatahivyo, nakazia kuwa HAKUNA KUWAACHIA HATA SENTI HAWA MITANDAO, yaani ikitokea labda laini ina sh 50.01 (maana yake haihamishiki hata kwenda airtime labda utupie nyingine kwanza) kisha mrirhi akasema ameridhika (akaipuuza) basi serikali ivute hiyo sh 50.01 yote kama ilivyo IKAFANYE MASWALA YA KIMAENDELEO KWA WANANCHI
Binafsi yangu mimi naona hilo siyo sahihi badala yake wangesaidia mfiwa/mrithi wa marehemu apate fedha hiyo kwanza kabla ya kuwaza kuipeleka serikalini
Nilisoma sehemu fulani kwamba ukitaka kuipata fedha iliyopo kwenye simu ya mtu aliyekufa itakubidi upeleke mlolongo wa viambata (wameviorodhesha huko niliposoma) upeleke kwenye (ofisi za) mtandao husika ndipo wakupe PIN ya marehemu
Jambo la ajabu ni kwamba sikuona popote maelezo ya kuhusu wao mtandao wanachukua fedha hiyo iliyoachwa kwa masharti yapi (kwa viambata gani)
Kwahiyo ushauri wangu aangaliwe kwanza mrithi arahisishiwe namna ya kupata fedha hiyo (iwe ndio namba moja) halafu ikitokea sasa salio likawa dogo au hata kubwa ila akaamua kuliacha kwa hiari yake ndipo tuhamie upande wa serikali wachukue zote (serikali wawe ni namba mbili)
Hatahivyo, nakazia kuwa HAKUNA KUWAACHIA HATA SENTI HAWA MITANDAO, yaani ikitokea labda laini ina sh 50.01 (maana yake haihamishiki hata kwenda airtime labda utupie nyingine kwanza) kisha mrirhi akasema ameridhika (akaipuuza) basi serikali ivute hiyo sh 50.01 yote kama ilivyo IKAFANYE MASWALA YA KIMAENDELEO KWA WANANCHI