Ushauri kwa serikali: Huduma za afya bure na Bima ya Afya kwa kila Mtanzania zinawezekana kama serikali itafanya hivi...

Opportunity Cost

JF-Expert Member
Dec 10, 2020
9,035
6,907
Poleni na harakati za kupambana na Uvico 19.

Turudi kwenye mada,kumekuwa na sintofahamu na kusita Kuhusu suala la kutolewa bure kwa huduma za matibabu nchini kwa kila mtanzania kuwa na bima ya Afya.

Ishu kubwa imekuwa ni gharama.Sasa serikali ingeanzisha utaratibu wa kuchangia gharama kwa makundi ya umri kwa kuweka kiwango cha sh.120,000 kwa mwaka kwa kila kaya kwa watu wazima wenye umri Kati ya miaka 25-65.

Watoto kuanzia mwaka 0-18 iwe ni sh.50,000 kwa mwaka na vijana wenye umri kuanzia miaka 19-24 iwe ni sh.80,000.

Kwa upande wa wazee zaidi ya miaka 65 iwe ni bure bila kuchangia chochote.Utaratibu huu utakuwa nafuu kuliko viwango vya sasa vya Bima ya Afya ya hiari.Kuchangia kutungiwe sheria na iwe ni LAZIMA ambako kila mtu atawajibika kulipa kwa mujibu wa sheria.

Uchangiaji huu ni affordable kwa kila rika na vipato endapo tuu utawekewa utaratibu mzuri wa kulipa kwa awamu au kwa mkupuo mmja.Hili likifanyika litamuwezesha kila mtu kuwa na Bima ya Afya na uhakika wa matibabu.

Kwa kuongezekae tuu serikali itakuwa na uhakika wa mapato ya kuendeshea sekta ya Afya.Kwa idadi ya wa watanzania zaidi ya mil.60 hapo unazungumzia wastani wa sh.320,000 kwa mtu mzima mwenye familia ya mtoto 1.Hii ni nafuu kuliko Bima ya hiari ya zaidi ya 480,000 kwa kichwa inayotolewa na NHIF.

Kama itafaa wafikilie kutunga sheria ya hivyo,watakaosema pesa ni kubwa hawatakosekana lakini this is cheapest way of funding universal health insurance.Watu tunalipa kodi za nyumba Kati ya 10,000-500,000 kwa mwezi ni dhahiri hiyo pesa ni ndogo Sana mtu kushindwa kulipa endapo itawekewa mkazo wa kisheria.

Karibuni kwa maboresho zaidi.
 
Unajua hali za watanzania kweli?

Mimi nashauri kila bidhaa iongezwe kodi ya Tsh 100 au 50 na hiyo pesa iende kwenye afya. Huduma zote zitolewe bila malipo kwa hospital zote na kwa rika zote.

Au inaweza kuongezwa kwa percentage let say 0.1% ya bei ya bidhaa zote, afya za watu wetu ndio msingi mkuu wa maendeleo.
 
Poleni na harakati za kupambana na Uvico 19.

Turudi kwenye mada,kumekuwa na sintofahamu na kusita Kuhusu suala la kutolewa bure kwa huduma za matibabu nchini kwa kila mtanzania kuwa na bima ya Afya.

Ishu kubwa imekuwa ni gharama.Sasa serikali ingeanzisha utaratibu wa kuchangia gharama kwa makundi ya umri kwa kuweka kiwango cha sh.120,000 kwa mwaka kwa kila kaya kwa watu wazima wenye umri Kati ya miaka 25-65.

Watoto kuanzia mwaka 0-18 iwe ni sh.50,000 kwa mwaka na vijana wenye umri kuanzia miaka 19-24 iwe ni sh.80,000.

Kwa upande wa wazee zaidi ya miaka 65 iwe ni bure bila kuchangia chochote.Utaratibu huu utakuwa nafuu kuliko viwango vya sasa vya Bima ya Afya ya hiari.Kuchangia kutungiwe sheria na iwe ni LAZIMA ambako kila mtu atawajibika kulipa kwa mujibu wa sheria.

Uchangiaji huu ni affordable kwa kila rika na vipato endapo tuu utawekewa utaratibu mzuri wa kulipa kwa awamu au kwa mkupuo mmja.Hili likifanyika litamuwezesha kila mtu kuwa na Bima ya Afya na uhakika wa matibabu.

Kwa kuongezekae tuu serikali itakuwa na uhakika wa mapato ya kuendeshea sekta ya Afya.Kwa idadi ya wa watanzania zaidi ya mil.60 hapo unazungumzia wastani wa sh.320,000 kwa mtu mzima mwenye familia ya mtoto 1.Hii ni nafuu kuliko Bima ya hiari ya zaidi ya 480,000 kwa kichwa inayotolewa na NHIF.

Kama itafaa wafikilie kutunga sheria ya hivyo,watakaosema pesa ni kubwa hawatakosekana lakini this is cheapest way of funding universal health insurance.Watu tunalipa kodi za nyumba Kati ya 10,000-500,000 kwa mwezi ni dhahiri hiyo pesa ni ndogo Sana mtu kushindwa kulipa endapo itawekewa mkazo wa kisheria.

Karibuni kwa maboresho zaidi.
Wazee na watoto chini ya miaka mitano.ni buree lakini ukienda hospitali utamuona daktari na utafanya vipimo Njoo kwenye dawa hakuna.
 
Unajua hali za watanzania kweli?

Mimi nashauri kila bidhaa iongezwe kodi ya Tsh 100 au 50 na hiyo pesa iende kwenye afya. Huduma zote zitolewe bila malipo kwa hospital zote na kwa rika zote.

Au inaweza kuongezwa kwa percentage let say 0.1% ya bei ya bidhaa zote, afya za watu wetu ndio msingi mkuu wa maendeleo.
Haiwezekani,,,Mfumuko wa bei ni tatizio...pia kama nchi, hatuzalishi vya kutosha,,tunaagiza mzigo toka CHINA kwa forex,,tunabaki na hela yetu ya MADAFU
 
Unajua hali za watanzania kweli?

Mimi nashauri kila bidhaa iongezwe kodi ya Tsh 100 au 50 na hiyo pesa iende kwenye afya. Huduma zote zitolewe bila malipo kwa hospital zote na kwa rika zote.

Au inaweza kuongezwa kwa percentage let say 0.1% ya bei ya bidhaa zote, afya za watu wetu ndio msingi mkuu wa maendeleo.
Mafuta tuu yaliongezwa 100,kelele zake sio za Nchi hii.
 
Back
Top Bottom