Ushauri kwa Serikali: Ajira za mkataba ndiyo suluhisho pekee la uhaba wa ajira nchini

Wabongo tunajisahau sana kijana ukimpa mkataba wa miaka mitano anajisahau mpaka miaka mitano inaisha ndo anang’ang’ana anunue godoro
Akijisahau si inakula kwake na ataikumbuka hio hela akiwa kwenye msoto! Kusema serikali itoe hela bure bure hizo pesa hazitawafikia walengwa!
 
Kila mwaka wanavyuo wengi wana graduate na kurundikana mtaani bila ajira huku wakihangaika kutafuta ajira bila mafanikio. Serikali kama mdau wa ajira nchini inapaswa kuja na wazo la ajira za mkataba kama ifuatavyo;-

1.Kwenye utumishi wa umma:
Mfumo wa ajira za maisha uondolewe yaani nesi, daktari, mwalimu n.k badala ya ajira zao kuwa za maisha ziwe za mkataba wa miaka mitano hadi kumi tena wakilipwa mishahara minono ili mkataba unapoisha mtumishi akajiajiri ili kuendeleza maisha yake! Hii itasaidia serikali kuajiri watumishi wapya wanaotafuta ajira kila siku na kupunguza uhaba wa ajira nchini!

2.Kwenye siasa:
Serikali itunge sheria itakayosimamia vyama vya siasa kutorudia kuteua majina yale yale kwenye uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani kila baada ya miaka mitano. Kuwe na ukomo wa utumishi wa kisiasa kwa miaka mitano mitano ili kuwapa nafasi wengine wenye sifa na vigezo vya kielimu vikichukuliwa kama sifa kuu mojawapo ya uteuzi. Angalau Shahada ya kwanza kwa ubunge na Astashahada kwa udiwani. Hii itatoa fursa kwa wengi kupitishwa na vyama vya siasa kwenye uchaguzi na kusaidia kupunguza tatizo la ajira nchini.

Nawakaribisha kwa mjadala huru na mwenye mawazo mbadala aongezee.
una mawazo mazuri ila umesahau hao unaotaka wastaafu mapema ndo wanaowatunza na kuwahudumia hao wanaotafuta ajira hadi wanafikia hatua ya kupata sifa za kuomba hizo ajira.

Kwa maneno mepesi iwapo wazo lako litatimia litafanya vijana wengi kuishia mtaani kwa kukosa sifa za kuajiriwa. wewe ushukuru umesomeshwa na kupata hizo sifa ila usiharibie wenzako wa baadae.
 
unataka kusema kati ya watanzania milioni 60 ukitoa wapumbavu 300,000 wa serikalini then wanabaki 59,700,000 unataka kusema hawa wamelala hawana kazi wenye kazi ni nyie mabumunda 300,000 pekee yake?

shambani,magengeni,bodaboda,wavuvi,etc unafanya wewe?wewe unadhani hawa watu wamelala hawafanyi kazi?

una matatizo mkuu?
haya basi chukua pointi tatu mkuu!!!
 
Wazo ni zuri ila haliwezi kutekelezeka kwasababu ya sera mbovu ya ajira na hali ya kiuchumi ya sekta nyingi za ajira.Ili kutekeleza hilo inabidi kwanza nchi iwe na sera ya uchumi imara inayoeleweka kuanzia kwenye sekta rasmi hadi binafsi.Pia elimu ya vyuo vyetu ifanyiwe mabadiliko makubwa ili kupatikane watu compitent wakuingia moja kwa moja kazini bila kuhitaji miaka ya uzoefu kitu ambacho kwa hapa bongo bado ni mtihani,Kufanya maboresho ya msingi kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.Lakini pia kurekebisha sheria za ajira ili kuendana na hali na mazingira.Hapo kwa wsnasiasa ni sawa kabisa maana wao hakuhitajiki uzoefu wowote.miaka mitano mitano inawatosga kabisa.
 
Kila mwaka wanavyuo wengi wana graduate na kurundikana mtaani bila ajira huku wakihangaika kutafuta ajira bila mafanikio. Serikali kama mdau wa ajira nchini inapaswa kuja na wazo la ajira za mkataba kama ifuatavyo;-

1.Kwenye utumishi wa umma:
Mfumo wa ajira za maisha uondolewe yaani nesi, daktari, mwalimu n.k badala ya ajira zao kuwa za maisha ziwe za mkataba wa miaka mitano hadi kumi tena wakilipwa mishahara minono ili mkataba unapoisha mtumishi akajiajiri ili kuendeleza maisha yake! Hii itasaidia serikali kuajiri watumishi wapya wanaotafuta ajira kila siku na kupunguza uhaba wa ajira nchini!

2.Kwenye siasa:
Serikali itunge sheria itakayosimamia vyama vya siasa kutorudia kuteua majina yale yale kwenye uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani kila baada ya miaka mitano. Kuwe na ukomo wa utumishi wa kisiasa kwa miaka mitano mitano ili kuwapa nafasi wengine wenye sifa na vigezo vya kielimu vikichukuliwa kama sifa kuu mojawapo ya uteuzi. Angalau Shahada ya kwanza kwa ubunge na Astashahada kwa udiwani. Hii itatoa fursa kwa wengi kupitishwa na vyama vya siasa kwenye uchaguzi na kusaidia kupunguza tatizo la ajira nchini.

Nawakaribisha kwa mjadala huru na mwenye mawazo mbadala aongezee.
Haya tumeyasema mda mkuu, hakuna sababu serikali kutoa ajira za maisha kwa watumishi wkt kuna lundo la watu wenye sifa mtaani, waweke ajira za mikataba serikalini na kwamba wale the best wawe wanaongezewa mikataba, iwe mkataba wa miaka mitano tu, hapo mtu anatoka anaingia mwengine, yule aliyetoka anakuwa tayari ameshakuwa expert anayeweza kujitafutia maisha sehemu nyingine, lkn pia anakuwa tayari na mtaji wa kutosha incase inatokea anakosa pa kujishikiza anakuwa anafanya mambo yake.


Hii itasaidia kurudisha nidhamu kwa watumishi kwani mtu atajituma ili apate kuongezewa mkataba, lkn pia itafanya watumishi wawe makini na matumizi ya hovyo cz watajipanga mapema kuliko kumuacha mtu amejisahau kazini matokeo yake anastaafu akiwa hana kitu.
 
Sio kusaga rumba! Unapewa miaka 5 ya kulipwa vizuri tu hili wazo nilishakujaga nalo jamaa ameamua kulianzishia uzi pia too good kumbe kuna mtu alikuwa na maono sawa na mimi tu!

Chukulia mfano mtumishi alipwe 5M kila mwezi bila kujali cadre! Kuwe na kiwango fixed kwamba kulingana na uchumi wa sasa we need to pay atleast 5M itampa nafasi ya kila mtumishi kuishi na ku save kiasi flani kila mwezi nje ya pension yake anayokatwa na NSSF! Chukulia mfano una save million kila mwezi tu..after 12 months utakuwa na million 12...after 5 years una million 60! Ukijumlisha na yale makato ya NSSF hamna hamna una 85M hivi kwa hii pesa mtu hajapata pa kuanzia tu?

Ikifika miaka mitano mkataba unaisha unaondoka na mtaji wa kutosha kabisa usiopungua 50M! Utashindwa kujiajiri kweli?
Hakuna haja ya kulipana mishahara mikubwa, hii hii inatosha na watu watajipanga mapema, hakuna pesa inayotosha isipokuwa ni nidhamu ya pesa tu, mtu akilipwa one milion huku akijua miaka mitano hana chake basi hyo one milion itafanya mengi kuliko ilivyo sasa.
 
Mkuu nina miaka nane sasa kama muajiriwa wa serikali!!watumishi tunakaa kazini muda mrefu sana vimishahara vidogo hadi tustaafu ni bora tuajiriwe kwa miaka michache tupate hela nyingi tufanye ujasiria mali mwingine kuliko kuajiriwa hadi tuchoke kabisa ndio tupewe hela!!!
Uongo..

Kwa miaka 8 basi tayari mfumo unaoshauri unakutaka ujiajiri...
Haya jiajiri kama unavyoshauri
 
Uongo..

Kwa miaka 8 basi tayari mfumo unaoshauri unakutaka ujiajiri...
Haya jiajiri kama unavyoshauri

Umenichekesha Kate, wanaongea kama vile kila mtu anaweza kujiajiri,,,,,mwingine Anadai Fresh graduates hawawezi kujiajiri watashindwa sasa mtu unajiuliza baada ya Miaka mitano ndani ya office huyu graduate ambae mwanzo alikua hajui kujiajiri anakua transformed baada ya miaka 5 na kujua kujiajiri, The question is HOW? watuambie labda tutaweza kufika muafaka
 
Umenichekesha Kate, wanaongea kama vile kila mtu anaweza kujiajiri,,,,,mwingine Anadai Fresh graduates hawawezi kujiajiri watashindwa sasa mtu unajiuliza baada ya Miaka mitano ndani ya office huyu graduate ambae mwanzo alikua hajui kujiajiri anakua transformed baada ya miaka 5 na kujua kujiajiri, The question is HOW? watuambie labda tutaweza kufika muafaka
Wanadai issue ni kipato/mtaji
 
Umenichekesha Kate, wanaongea kama vile kila mtu anaweza kujiajiri,,,,,mwingine Anadai Fresh graduates hawawezi kujiajiri watashindwa sasa mtu unajiuliza baada ya Miaka mitano ndani ya office huyu graduate ambae mwanzo alikua hajui kujiajiri anakua transformed baada ya miaka 5 na kujua kujiajiri, The question is HOW? watuambie labda tutaweza kufika muafaka
Atleast ataachwa na kitu mkononi! Knowing thats your last bullet in hand itampa ujasiri wa kujaribu mishe kadhaa maana mtaji anao.

Kuisha kwa mkataba ukiwa na 70M mkononi inaweza kuwa sawa na kukabidhiwa cheti cha degree bila sent 5 kisha uambiwe jiajiri?
 
kwa hio kila baada ya miaka mitano serikal ianze tena kuwafubdisha maana walr wenye uzoefu watakua wamesitishiwa mkataba.idea yako is pointress
Training inachukuaga miaka mitano kwani? Probation si huwa miezi mitatu mpaka 6!

Mbona mnaongea kama vile majuha?
 
Yaani baada ya kila miaka 5 watu wapya kazini
Huko kazini kutakua mchaka mchaka watu ni kuwaza kufanikisha mambo yao tu ubunifu utakua hakuna
Kwani hio miaka 60 kuna ambaye hawazii mambo yake binafsi? Wengi si wapigaji tu tena ubaya wa hii miaka 60 mtu akishapata mkataba wa Utumishi tu ana relax maana anajua follow ups huwa sio rahisi na kufukuzwa ni ngumu serikalini hata akivurunda! Ndio maana mtu yupo radhi aache mshahara wa million private company akimbilie laki 8 ya serikalini😅
 
MNHHHHH ugumu wa kijana aliyemaliza chuo kufanya biashara ni upi? Na urahisi wa mtu aliyekua ofisini kufanya biashara ikasimama ni upi?? Toa evidence tukuelewe maanake ni kama unasema watanzania wote tuingie kwenye ujasiriamali jambo ambalo ni ngumu haliko practical,,,,
We unaonekana unamenya serikalini wewe ndio maana hutamani ajira yako ikatishwe kwa mkataba! Mi nina hakika 80% ya waajiriwa ikatokea waambiwe ajira basi imetosha mpishe wengine basi kuna wengi tutawazika kwa presha.

Ugumu wakujiajiri uko pale pale ila utofauti utakuwa kwamba mwenye mtaji mkubwa ana chance kubwa yakutoboa mfano wewe umemeki 70M! Ukianza biashara ya 2M ikaanguka, ukarudia tena ikaanguka mpaka itakapokubali kuwork out you stand a chance by far!

Imagine graduate kafanya the same kwa 2M tu biashara imemkataa! Hela imepoteaa anarudishaje tumaini?
 
Back
Top Bottom