Ushauri kwa Serikali: Ajira za mkataba ndiyo suluhisho pekee la uhaba wa ajira nchini

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,454
17,263
Kila mwaka wanavyuo wengi wana graduate na kurundikana mtaani bila ajira huku wakihangaika kutafuta ajira bila mafanikio. Serikali kama mdau wa ajira nchini inapaswa kuja na wazo la ajira za mkataba kama ifuatavyo;-

1.Kwenye utumishi wa umma:
Mfumo wa ajira za maisha uondolewe yaani nesi, daktari, mwalimu n.k badala ya ajira zao kuwa za maisha ziwe za mkataba wa miaka mitano hadi kumi tena wakilipwa mishahara minono ili mkataba unapoisha mtumishi akajiajiri ili kuendeleza maisha yake! Hii itasaidia serikali kuajiri watumishi wapya wanaotafuta ajira kila siku na kupunguza uhaba wa ajira nchini!

2.Kwenye siasa:
Serikali itunge sheria itakayosimamia vyama vya siasa kutorudia kuteua majina yale yale kwenye uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani kila baada ya miaka mitano. Kuwe na ukomo wa utumishi wa kisiasa kwa miaka mitano mitano ili kuwapa nafasi wengine wenye sifa na vigezo vya kielimu vikichukuliwa kama sifa kuu mojawapo ya uteuzi. Angalau Shahada ya kwanza kwa ubunge na Astashahada kwa udiwani. Hii itatoa fursa kwa wengi kupitishwa na vyama vya siasa kwenye uchaguzi na kusaidia kupunguza tatizo la ajira nchini.

Nawakaribisha kwa mjadala huru na mwenye mawazo mbadala aongezee.
 
Kila mwaka wanavyuo wengi wana-graduate na kulundikana mtaani bila ajira huku wakihangaika kutafuta ajira bila mafanikio.

Serikali kama mdau wa ajira nchini inapaswa kuja na wazo la ajira za mkataba kama ifuatavyo;-

1. KWENYE UTUMISHI WA UMMA
Mfumo wa ajira za maisha uondolewe yaani nesi,daktari,mwalimu n.k badala ya ajira zao kuwa za maisha ziwe za mkataba wa miaka mitano hadi kumi tena wakilipwa mishahara minono ili mkataba unapoisha mtumishi akajiajiri ili kuendeleza maisha yake. Hii itasaidia Serikali kuajiri watumishi wapya wanaotafuta ajira kila siku na kupunguza uhaba wa ajira nchini!

2. KWENYE SIASA
Serikali itunge sheria itakayosimamia vyama vya siasa kutorudia kuteua majina yale yale kwenye uchaguzi mkuu wa wabunge na madiwani kila baada ya miaka mitano!!!Kuwe na ukomo wa utumishi wa kisiasa kwa miaka mitano mitano ili kuwapa nafasi wengine wenye sifa na vigezo vya kielimu vikichukuliwa kama sifa kuu mojawapo ya uteuzi. Angalau Shahada ya kwanza kwa ubunge na Astashahada kwa udiwani. Itatoa fursa kwa wengi kupitishwa na vyama vya siasa kwenye uchaguzi na kusaidia kupunguza tatizo la ajira nchini.

Karibuni kwa mjadala huru na mwenye mawazo mbadala aongezee.
 
Halafu mkataba ukiisha anarudi mtaani kusaga na rumba??Basi sawa✊
Sio kusaga rumba! Unapewa miaka 5 ya kulipwa vizuri tu hili wazo nilishakujaga nalo jamaa ameamua kulianzishia uzi pia too good kumbe kuna mtu alikuwa na maono sawa na mimi tu!

Chukulia mfano mtumishi alipwe 5M kila mwezi bila kujali cadre! Kuwe na kiwango fixed kwamba kulingana na uchumi wa sasa we need to pay atleast 5M itampa nafasi ya kila mtumishi kuishi na ku save kiasi flani kila mwezi nje ya pension yake anayokatwa na NSSF! Chukulia mfano una save million kila mwezi tu..after 12 months utakuwa na million 12...after 5 years una million 60! Ukijumlisha na yale makato ya NSSF hamna hamna una 85M hivi kwa hii pesa mtu hajapata pa kuanzia tu?

Ikifika miaka mitano mkataba unaisha unaondoka na mtaji wa kutosha kabisa usiopungua 50M! Utashindwa kujiajiri kweli?
 
katika kazi kama ya udaktari ambayo inahitaji mtu mwenye experience hio idea yako haitakua applicable..

Daktari kafanya kazi miaka mitano anajua magonjwa yote ya watoto, akielezewa tu shida ya mtoto kashapata jibu juu ya nini kinamsumbua mtoto, daktari mwingine ameshazoea kufanya upasuaji bila hofu yoyote, leo hii umfukuze kazi umlete Daktari anayeanza na zero? SIO KWELI.
 
katika kazi kama ya udaktari ambayo inahitaji mtu mwenye experience hio idea yako haitakua applicable..

Daktari kafanya kazi miaka mitano anajua magonjwa yote ya watoto, akielezewa tu shida ya mtoto kashapata jibu juu ya nini kinamsumbua mtoto, daktari mwingine ameshazoea kufanya upasuaji bila hofu yoyote, leo hii umfukuze kazi umlete Daktari anayeanza na zero? SIO KWELI.
Msamehe mawazo yake ya kichuochuo
 
Acha kudharau mawazo yake. Ana point ya msingi.

Exeption chache kama hizo za madaktari zinaweza kuwekwa.

Ila hii itapunguza sana suala la watu kujisahau makazini.
Unajiona umetoa bonge la coment unafkr ni kada ya udaktar tu?

Ningekuona wa maana ungemrekebisha umri wa kustaafu apo sawa
 
Ile option ya Experience required itafanya ku-recycle walewale ambao mkataba umekwisha...., Nothing beats Experience...

Tatizo tumeacha ku-base kwenye utendaji bali tuna-base kwenye kipato..., yaani jinsi ya ku-share kipato kidogo kilichopo..., I wish mentality zetu zingebadilika badala ya kugombania kidogo kilichopo tungejitahidi kutengeneza kingi zaidi
 
Miaka ya kustaafu ipunguzwe 45 mwisho mtu aachie ngazi sasa wazee wamekaza eti mpaka miaka 60 ni mingi sana 45 tu astaafu akiwa a nguvu zake akaanzishe mradi ili awaajir wengine na wengine warithi nafasi yake. pia ajira za mkataba n sawa sasa sirikali inaangaika mbowe tu
 
We unazungumza haya sababu ujapata tu ajira!!!..

Kaa vizur na sis watumishi wa Tz!!!!

Tutakupa habar nzur Zaid:
 
Sio kusaga rumba! Unapewa miaka 5 ya kulipwa vizuri tu hili wazo nilishakujaga nalo jamaa ameamua kulianzishia uzi pia too good kumbe kuna mtu alikuwa na maono sawa na mimi tu!

Chukulia mfano mtumishi alipwe 5M kila mwezi bila kujali cadre! Kuwe na kiwango fixed kwamba kulingana na uchumi wa sasa we need to pay atleast 5M itampa nafasi ya kila mtumishi kuishi na ku save kiasi flani kila mwezi nje ya pension yake anayokatwa na NSSF! Chukulia mfano una save million kila mwezi tu..after 12 months utakuwa na million 12...after 5 years una million 60! Ukijumlisha na yale makato ya NSSF hamna hamna una 85M hivi kwa hii pesa mtu hajapata pa kuanzia tu?

Ikifika miaka mitano mkataba unaisha unaondoka na mtaji wa kutosha kabisa usiopungua 50M! Utashindwa kujiajiri kweli?

Haiko realistic..
Waajiri wakuu nchini ni Sekta Binafsi..Na huko unalipwa kadri ya unavyozalisha..sasa ..
Hata ikiapply serikalini tu,kamwe tatizo la ajira halitakwisha naana hawawezi kuajiri watu wengi kama sekta Binafsi..
Walau hoja ya pili . (Vikomo vya madaraka ya kisiasa) inamake sense
 
We unazungumza haya sababu ujapata tu ajira!!!..

Kaa vizur na sis watumishi wa Tz!!!!

Tutakupa habar nzur Zaid:
kwakweli. Mleta mada akipata ajira serikalini sidhani kama atabakiwa na ili wazo
 
Back
Top Bottom