Ufisadi,Mikataba Mibovu,Umaskini..

mwanamichakato

JF-Expert Member
Mar 20, 2015
887
705
Mikataba mibovu katika sekta ya nishati,madini,manunuzi,na ujenzi wa miundombinu kitita ni chanzo kikuu cha umaskini uliokithiri katika taifa letu.Umaskini husika umetokana kwa kiasi kikubwa na ulaghai,rushwa kubwa,Ufisadi,Ubinafsi,matumizi mabaya ya madaraka,ujasiliamali wa kisiasa na ubovu wa katiba na udhaifu wa sheria zetu.

Maridhiano ya kitaifa kupitia tume maalumu yangelazimisha wote walioifisidi nchi,ilaghai nchi,ifitini nchi,Walioingia mikataba ya ulaghai,Mikataba mibovu,waliotengeneza mikataba ya kimangungo..ikiwemo ya uchimbaji madini,gesi,uvunaji misitu,Usafirishaji..

Tume ya maridhiano itawalazimisha wote wanaoguswa na kusababisha hasara kubwa kwa nchi kwa namna moja au nyingine na kuwataka waungame,watubu, kukiri madudu walioyafanya na kurejesha mali zote walizojirimbikizia kupitia mihamala yenye kuliangamiza taifa.Watapaswa kukiri siri zenye uovu ndani zenye chemuchemu isababishao umaskini,mateso,unyonyaji na uharamia wa rasilimali za taifa Tanzania...
 
Mikataba mibovu katika sekta ya nishati,madini,manunuzi,na ujenzi wa miundombinu kitita ni chanzo kikuu cha umaskini uliokithiri katika taifa letu.Umaskini husika umetokana kwa kiasi kikubwa na ulaghai,rushwa kubwa,Ufisadi,Ubinafsi,matumizi mabaya ya madaraka,ujasiliamali wa kisiasa na ubovu wa katiba na udhaifu wa sheria zetu.

Maridhiano ya kitaifa kupitia tume maalumu yangelazimisha wote walioifisidi nchi,ilaghai nchi,ifitini nchi,Walioingia mikataba ya ulaghai,Mikataba mibovu,waliotengeneza mikataba ya kimangungo..ikiwemo ya uchimbaji madini,gesi,uvunaji misitu,Usafirishaji..

Tume ya maridhiano itawalazimisha wote wanaoguswa na kusababisha hasara kubwa kwa nchi kwa namna moja au nyingine na kuwataka waungame,watubu, kukiri madudu walioyafanya na kurejesha mali zote walizojirimbikizia kupitia mihamala yenye kuliangamiza taifa.Watapaswa kukiri siri zenye uovu ndani zenye chemuchemu isababishao umaskini,mateso,unyonyaji na uharamia wa rasilimali za taifa Tanzania...

Umeongea kila kitu lakini tatizo vijana wa Lumumba hawaelewi,waandishi wa hiyo mikataba na akina JPM walikuwepo wakikubaliana kulidhoofisha TAIFA kwa kujilimbikizia mali.

Hivyo hakika tunahitaji TUME ya MARIDHIANO,Taifa letu sote na sisi watanzania bila kujali ITIKADI zetu ndiyo wajenzi wa TAIFA siyo JPM wala CCM tu.Tusidanganywe na akina Polepole na JPM
 
Mh Rais nafahamu nia ya maamuzi yako ya kuzuia mchanga unaotokana na madini ni kujaribu kuzuia wizi na ujanja wa wawekezaji wa uchimbaji madini, ni vizuri kujiuliza je Tanzania imeshafikia uwezo wa kuwa na viwanda vya kuchambua mchanga huo maana kurundikana kwa tani nyingi za makontena ya mchanga bandarini hakutatuletea tija.

je zuio hilo halivunji moja ya vipengele vya mikataba na wawekezaji? kama zuio lako linakiuka mkataba basi sasa ili kupata kinga ya kisheria za mashtaka dhidi ya uvunjaji huo ambapo nchi inaweza kukabiliwa na kesi hiyo na kujikuta katika malumabno ya sheria za kimataifa za mikataba, jambo ambalo wawekezaji hao ndipo wanapotegea kwa hamu

nakushauri kwa kutumia Waziri wa Madini na Nishati na Ofisi ya Mwanasheria mkuu wa Serikali wawasilishe mapema bungeni hoja ya kupitia upya mikataba ya madini nchi nzima, kuna maswali ya kujiuliza kwann wasafirishe mchanga wetu nje ya nchi?

je mbona hatupati mrejesho baada ya hapo? vilevile Mh Rais mikataba hiyo ipo katika sura kimataifa zaidi ili wawekezaji waweze kujikinga na uvunjaji wa vipengele katika mkataba, aidha dhumuni lao ni kupata haki kutushitaki katika mahakama zao za kinyonyaji na kutukandamiza hivyo kujikuta tunawalipa bilions ya dollar kama faini, hivyo basi ni vizuri na haraka kipengele cha kusafirisha mchanga unaotokana na madini kifutwe ili rasmi mchanga usisafirishwe nje kwaajili ya uchakataji
 
Siyo kupitia mikataba ya madini tu, bali muswada utamke kuwa mikataba yote kuhusu rasilimali za Taifa itakuwa wazi!
 
Tume za kuchunguza michanga zisingeitajika kama mikataba ya madini ingejadiliwa bungeni mubashara
 
Hii bandika bandua haitosaidia mtu hata akija malaika kuwa waziri bado tutaendelea kuwa na matatizo kwa sababu msingi unaotuongoza (Katiba yetu ya 1977) pamoja na sheria na taratibu haziruhusu kuwepo kwa checks and balances matokeo yake system nzima inakuwa imeoza na hakuna transparency.

Pengine mchakato wa kuwachuja kwa kigezo cha Tabia, tunaotaka kuwakabidhi madaraka makubwa haujakaa sawa sawa. Kwamba hata mwenye tabia za Ukorofi, kiburi, majivuno, ujuaji n.k, naye anaweza kuwa kiongozi mkubwa.

Hivi mshajiuliza kwa nini idara za manunuzi za serikali haziweki wazi kwenye tovuti zao michakato ya tender board minutes za vikao vyao kwenye tovuti ili tujue kampuni yenye scandal za ufisadi kama China Merchants ilipata vipi tenda kubwa Bandari ya Dar na ilishinda kwa vigezo vipi na vikao vya bodi walikaa akinanani..... hii ni jambo dogo sana lakini impact yake ni kubwa na itaondoa usiri uliogubika idaya hii nyeti ya ununuzi/ procurement inayoongoza kwa rushwa na ufisadi kwenye kila sekta ya serikali

Je hili nalo linahitaji katiba mpya au amri toka kwa rais?

Lazima tukubali bila katiba mpya na transparency serikalini bado tutaendelea kufukuza watu wakati tunajua mfumo ndio tatizo na hata akija malaika itabidi afanye kazi within the rotten system

Karibuni kwa mjadala mpana
 
Hii bandika bandua haitosaidia mtu hata akija malaika kuwa waziri bado tutaendelea kuwa na matatizo kwa sababu msingi unaotuongoza (Katiba yetu ya 1977) pamoja na sheria na taratibu haziruhusu kuwepo kwa checks and balances matokeo yake system nzima inakuwa imeoza na hakuna transparency.

Pengine mchakato wa kuwachuja kwa kigezo cha Tabia, tunaotaka kuwakabidhi madaraka makubwa haujakaa sawa sawa. Kwamba hata mwenye tabia za Ukorofi, kiburi, majivuno, ujuaji n.k, naye anaweza kuwa kiongozi mkubwa.

Hivi mshajiuliza kwa nini idara za manunuzi za serikali haziweki wazi kwenye tovuti zao michakato ya tender board minutes za vikao vyao kwenye tovuti ili tujue kampuni yenye scandal za ufisadi kama China Merchants ilipata vipi tenda kubwa Bandari ya Dar na ilishinda kwa vigezo vipi na vikao vya bodi walikaa akinanani..... hii ni jambo dogo sana lakini impact yake ni kubwa na itaondoa usiri uliogubika idaya hii nyeti ya ununuzi/ procurement inayoongoza kwa rushwa na ufisadi kwenye kila sekta ya serikali

Je hili nalo linahitaji katiba mpya au amri toka kwa rais?

Lazima tukubali bila katiba mpya na transparency serikalini bado tutaendelea kufukuza watu wakati tunajua mfumo ndio tatizo na hata akija malaika itabidi afanye kazi within the rotten system

Karibuni kwa mjadala mpana
Tatizo ni CCM
 
Inawezekana ni kweli kabisa katiba ni tatizo kwenye huu wizi.......ila wajameni, CCM ndio Kansa.........hichi chama ndio malikia wa wizi........Watanzania tumuue huyu malikia basi huo mtandao wote utakuwa umekwisha.
 
tatizo na hata akija malaika itabidi afanye kazi within the rotten system
Hata huyo malaika akija ataambiwa atushukie huku JF bora asije,hii rotten system inataka maombi na hivi mwezi mtukufu ndo unapiga hodi ni mwendo wa kufunga na maombi.
 
Hii bandika bandua haitosaidia mtu hata akija malaika kuwa waziri bado tutaendelea kuwa na matatizo kwa sababu msingi unaotuongoza (Katiba yetu ya 1977) pamoja na sheria na taratibu haziruhusu kuwepo kwa checks and balances matokeo yake system nzima inakuwa imeoza na hakuna transparency.

Pengine mchakato wa kuwachuja kwa kigezo cha Tabia, tunaotaka kuwakabidhi madaraka makubwa haujakaa sawa sawa. Kwamba hata mwenye tabia za Ukorofi, kiburi, majivuno, ujuaji n.k, naye anaweza kuwa kiongozi mkubwa.

Hivi mshajiuliza kwa nini idara za manunuzi za serikali haziweki wazi kwenye tovuti zao michakato ya tender board minutes za vikao vyao kwenye tovuti ili tujue kampuni yenye scandal za ufisadi kama China Merchants ilipata vipi tenda kubwa Bandari ya Dar na ilishinda kwa vigezo vipi na vikao vya bodi walikaa akinanani..... hii ni jambo dogo sana lakini impact yake ni kubwa na itaondoa usiri uliogubika idaya hii nyeti ya ununuzi/ procurement inayoongoza kwa rushwa na ufisadi kwenye kila sekta ya serikali

Je hili nalo linahitaji katiba mpya au amri toka kwa rais?

Lazima tukubali bila katiba mpya na transparency serikalini bado tutaendelea kufukuza watu wakati tunajua mfumo ndio tatizo na hata akija malaika itabidi afanye kazi within the rotten system

Karibuni kwa mjadala mpana
Weee vipi? Mfumo gani unataka? Kujenga smelter na refinery ilipitishwa 2009.
 
Back
Top Bottom