issac77
JF-Expert Member
- Apr 26, 2013
- 2,948
- 4,715
Mimi ni msichana nina miaka 23,baba yangu ni mfanyabiashara maarufu sana na ni miongoni mwa matajiri wakubwa sana.mwaka wa jana mwezi wa kumi na mbili nilifiwa na dada yangu ambaye ni wa kwnza kuzaliwa,baba alikuwa anampenda sana dada na siku alipofariki baba alilia sana kiasi cha kupoteza fahamu mara kadhaa kitu kilichopelekea akimbizwe hosptal.
week iliyopita baba aliniita chumbani kwake kitu ambacho sio kawaida,kufika akaniambia kwamba utajiri wake wote aliupata kwa mganga wa kienyeji na alipewa sharti la kufanya mapenzi na bintiye ili kuufanya utajiri wake uendelee kuwepo.Aliendelea kuniambia kwamba kwa kipindi chote alikuwa anafanya mapenzi na marehemu dada yangu na ndo maana alizidi kuwa tajiri,
sasa kwa kuwa dada amefariki aliniambia inatakiwa mimi ndio niwe nafanya naye mapenzi ili kutimiza masharti ya utajiri la sivyo utajiri wake wote utapukutika.
Mimi nimechanganyikiwa kwa kweli naombeni ushauri wenu Tafadhali share na wengine ili apate ushauri zaidi