Ushauri kwa mdogo wangu: Alioa akiwa na umri wa miaka 23 sasa anamkataa mkewe akidai yeye bado mdogo

Cosovo

JF-Expert Member
Jul 8, 2018
667
1,795
Mdogo wangu umri miaka 23,mwaka jana tu alimuomba mzee na marafiki kumuandalia harusi ili aweze kuaga ukapera.

Wazazi na marafiki wakafanya michango na kuandaa harusi kubwa tu na dogo akaoa.

Mchumba wake wamesoma naye hadi kidato cha nne shule moja na hivyo wanafahamiana kila kitu.

Miezi 6 tu imepita tangu aoe lakini cha ajabu ameanza kumkataa mke wake.

Sababu ambayo ametoa ni kuwa "YEYE NI MDOGO ,UMRI WAKE NI MDOGO ,AMEFANYA MAKOSA KUOA KWA SASA ,HATAKI HUYO MWANAMKE BADO HAJAKUA"

Tulipohitaji kujua kama alijua hivyo awali kwa nini aoe? Amejibu "HAJUI ILIKUWAJE AKAWA NA WAZO LA KUOA ,KWA KIFUPI HAJAWA TAYARI KUISHI NA MWANAMKE"

Huyu kijana apewe ushauri gani?
 
Mwanaume unaoa 23 ili iweje labda, unawahi nini? Utapigiwa stress huko ndoani hadi ukumbuke kwenu....kula ujana wako kwanza.
Mkuu eva inategemea unaoa mwanamke wa aina gani, je? ukiwa mjanja sana tulia oa wife material yaani kuna mwanamke wewe kama mwanaume inabidi umpange akifika tu 37 au 35 hapo asha kuzalia ww watoto wawil au watatu, unatulia zako tu yaani wapo wanawake wanyonge mi ndio ninao wataka hao sasa, yaaani ukishaweza kumtawala mwanamke basi, oa ambaye hana maisha afu wale ambao sio maslay
 
Mwanaume unaoa 23 ili iweje labda, unawahi nini? Utapigiwa stress huko ndoani hadi ukumbuke kwenu....kula ujana wako kwanza.
Oa mkuu hawa hawa mafundi cherehani wauza mboga niwashamba, mpaka aje kuwa mjanja ana 40 au 45 hapo ashazaa watoto 3 sasa jifanye unataka wale wa viatu virefu uone, yaani hawa wa kitaa akija gheto haruki
 
oa mkuu hawa hawa mafundi cherehani wauza mboga niwashamba, mpaka aje kuwa mjanja ana 40 au 45 hapo ashazaa watoto 3 sasa jifanye unataka wale wa viatu virefu uone, yaani hawa wa kitaa akija gheto haruki
Washamba ndio choices unazopenda? Au unaoa tu ilimradi unaoa? afu mkeo umuwekee ndani kama utumbo, uanze kusumbua wake za wenzio waliovaa viatu virefu?
 
mkuu eva inategemea unaoa mwanamke wa aina gani, je? ukiwa mjanja sana tulia oa wife material yaani kuna mwanamke wewe kama mwanaume inabidi umpange akifika tu 37 au 35 hapo asha kuzalia ww watoto wawil au watatu, unatulia zako tu yaani wapo wanawake wanyonge mi ndio ninao wataka hao sasa, yaaani ukishaweza kumtawala mwanamke basi, oa ambaye hana maisha afu wale ambao sio maslay
Anyway inategemea....ila mimi kama mimi umri huo hapana
 
Back
Top Bottom