Ushauri kwa huyu ndugu yetu kwa hali aliyonayo

ELX

JF-Expert Member
Jan 3, 2010
328
379
Mahusiano ni jambo linalopelekea mtu kuwa mwema au kuwa na roho mbaya. Katika mizunguko yangu juzi nilikuwa sehemu nikakutana na dada mmoja wa makamo mwenye watoto 3(aliniambia). Kwa mtizamo alikuwa ana mawazo, tukawa tunapiga stori kawida, kunakitu aljifuza kwangu kutoana na mazungumzo, akaomba nimshauri. Alinieleza kuwa aliolewa na akapata mtoto 1 na bwana wake wa 1 bahati mbaya akafariki na kumuacha mpweke. Alikaa kitambo bila kuwa na mahusiano na mwanaume yeyote. Baadae akapata mwanaume na kuishi nae na kubahatika kuzaa watoto 2, baadae yule bwana akawa anamnyanyasa sana ikapelekea mahusiano yao kuvunjika na kupeana talaka. Kutokana na misukosuko aliyoipata kwa mumewe huyo, alijenga hali ya kuchukia wanaume wote na hana imani na yeyote anayekuja mbele yake.

Kutokana na upweke huo kuna rafiki yake alimshauri kuepuka adha ya wanaume inabidi ajiridhishe mwenyewe kwa kutumia mashine kujichua. Mwanzo aliona sawa na kasha kuwa anafanya hivyo kwa zaidi ya mwaka na nusu, anacho sema kwa sasa hana hisia yeyote na mwanaume, ila akiweka wazo kwenye mashine yake hiyo anaridhika na kujisikia amani.

Anataka kuacha hali hiyo arudi kawaida, na alijaribu kukutana na mwanaume mara 1 miezi kadhaa iliyopita alipata maumivu sana, sasa afanyeje? Hataki kutendwa tena na huo mchezo anataka kuuacha. Anaomba mbinu za kujinasua na huo mchezo.

Nilimshauri mawazo yake ayaweke kwenye kazi na watoto wake, na atupe hicho kifaa anachotumia ili hata akiwaza anajikuta hana cha kusaidia kutimiza haja yake. Na asiwachukie wanaume bali amusome anaye mfuata kwa mahusiano ya kweli. Swali likaja atamtambuaje mkweli?

Wadau sikutarajia kusikia hayo kwa dada yule, naamini hapa JF ni suluhu ya Mambo, TUMSHAURI
 
Mwambie atunze watoto, umri ushaenda na yeye

Hilo nilimshauri, alisema sawa ila anataka kuwa kama wengine, aliolewa mdogo kutokana na mila zao, kwa sasa ana umri wa miaka 30
 
Hilo nilimshauri, alisema sawa ila anataka kuwa kama wengine, aliolewa mdogo kutokana na mila zao, kwa sasa ana umri wa miaka 30
kama wewe ni mwanaume anza kumsaidia kumaliza tatizo lake kwa kumpa hiyo huduma ya kijamii lakini kwa makubaliano maalum
 
Tehetehe Mokoyo, sipo kihivyo na sitegemei kufanya hivyo. Na si busara kwa mtu kufunguka kueleza tatizo wewe uchukulie mteremko, utaonekana mtu wa ajabu na binafsi nafsi yangu itanisuta, hivyo napenda niwe na amani. Tumshauri tu, ili atakaye kutana asijue tatizo alilokuwa nalo au aamue yeye kumueleza
 
Last edited by a moderator:
Habari wadau, maoni yenu, tumsaidie huyu ndugu yetu.
 
hee kashaathilika psychological...hebu wadau waseme njia ya kuepukana na hili janga.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom